Matokeo chanyA+ online




Thursday, March 19, 2020

JIJI LA DODOMA LIMETUMIA MAPATO YA NDANI KUIMARISHA UDHIBITI WA UJENZI HOLELA

Halmshauri ya jiji la Dodoma limetumia kiasi cha Sh milioni 345 kutoka kwenye mapato yake ya ndani kwa ajili ya kununua vitendea kazi ambavyo ni magari matatu ili kuimarisha Kitengo cha udhibiti wa ujenzi holela chini ya Idara ya Ardhi, Mipango miji na Rasimali.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya  jiji la Dodoma Godwin Kunambi akiongea katika hafla ya kukabidhi magari matatu yaliyonunuliwa na Halmashauri hiyo.

Akikabidhi magari hayo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt  Binilith Mahenge  amelipongeza jiji hilo kwa kutekeleza agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa la kuhakikisha wanatekeleza Mpango kabambe wa jiji hilo uliozinduliwa hivi karibuni.

Amesema mpango huo ulipangwa na kupitishwa na baraza la madiwani, na Mkurugenzi wa jiji na Menejimenti yake wameteleza kwa haraka ni hatua kubwa.

"Waziri Mkuu aliagiza kusimamia utekelezaji wa mpango kabambe wa jiji hili na muda mfupi baada ya kutolewa agizo hilo nyinyi mmetekeleza mara moja kwa kununua vitendea kazi ambavyo ilikuwa ni moja ya maelekezo, nawapongeza kwa kutumia kiasi hicho cha fedha kutoka mapato yenu ya ndani,"alisema Dkt Mahenge.
Moja ya gari lililonunuliwa na Halmashauri ya jiji la Dodoma kwa mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuimarisha kitengo cha udhibiti wa ujenzi holela.

Ameongeza kusema“Kwa kuwa na vitendea kazi hivi hatutegemei kuona tena ujenzi holela Dodoma,hatutegemei kuona X maana hiyo alama inaonyesha kuwa huyo mtu hakutembelewa kabla,hatutegemei kabisa kabisa kuona ujenzi kwenye maeneo yalihofadhiwa,”alisema dkt Mahenge.

Amewataka wananchi kuzingatia  taratibu na sheria pindi wanapotaka kuanza ujenzi ili kulipanga vyema jiji hilo.
 
Awali Mkurugenzi wa Jiji hilo Godwin Kunambi amesema magari hayo wamenunua kutokana na ushirikiano mzuri uliopo baina yao na baraza la madiwani.

“Haya magari matatu,double cabin mbili ni sh mil 92,nah ii Toyota hard top ni sh milioni 160,fedha hizi ni mapato ya ndani na jambo hili linafanyika kwa jiji hili tu,zamani ilikuwa mpaka uombe serikali kuu lakini sasa tumenunua kwa mapato yetu wenyewe,”alisema Kunambi.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge akijaribu moja ya gari lililonunuliwa na Halmashauri ya jiji la Dodoma kwa ajili ya kuimarisha Kitengo cha udhibiti wa ujenzi holela.
Amesema jiji limeona liimarishe kitengo chao cha udhibiti wa ujenzi holela kwa kununua vitendea kazi hivyo wakiwa wanaamini kuwa vitawarahisishia katika utendaji wa kazi kwenye Idara ya Ardhi, kutekeleza Mpango kabambe wa jiji la Dodoma, lengo likiwa ni kuendelea kupima kwa haraka maeneo yanayokua kwa kasi.

“Jiji la Dodoma lina km za mraba 2,700 yaani mkoa wa Dar es salaam unaingia mara mbili kwa jiji la Dodoma kwa kuwa una km za mraba 2,500 hapo hapo bahari na nchi kavu,lakini jiji la Dodoma ndio pekee limepangwa kwa asilimia 100,lina mpango kabambe unaoonyesha hakuna sehemu ambayo haijapangwa,”alisema Mkurugenzi huyo.

No comments:

Post a Comment