Serikali imegawa pikipiki 448 kwa maafisa tarafa nchini
ili kurahisisha utendaji kazi wao ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais
Dkt John Magufuli aliyoitoa kwao mwaka jana.
Akikabidhi
pikipiki hizo kwa baadhi ya wakuu wa mikoa Machi 18 jijini Dodoma,
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo amesema pikipiki hizo zimegaiwa kwa mikoa
24 kutokana na mkoa wa Songwe na Pwani kuwa walishapewa.
![]() |
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akijaribu pikipiki mojawapo zilizotolewa kwa maafisa tarafa nchini. |
Amesema
hatua hiyo itaondoa kero ya vitendea kazi na serikali imeendelea
kuzipatia ufumbuzi kero zingine kadri mapato ya serikali yanavyoimarika.
"Tuna
maafisa tarafa 570 lakini wengine walishapata pikipiki,Mhe Rais kupitia
serikali Imempendeza kutoa sh bilioni moja kwa ajili ya kununua
pikipiki hizi 448 hivyo kuondoa kero,niwatake maofisa tarafa kutotumia
pikipiki hizi kama kitega uchumi kwa kubeba abiria,"alisisitiza Waziri
Jafo.
Kwa upande wake,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Kapteni George Mkuchika amesema pikipiki hizo
zitarahisisha utendaji kazi kwa Maofisa hao hususan kipindi cha Uchaguzi
Mkuu.
"Nikushukuru
Waziri kwa hatua hii,tunajua maafisa hawa ndio kiungo kikubwa cha
utendaji kazi,wakati mwingine tunawatuma huku na kule walete taarifa hii
na ile,hivyo kwa kutumia usafiri huu itakuwa rahisi kwao,"alisema
Waziri Mkuchika.
Naye,
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dokta Rehema Nchimbi na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Dokta BIinilith Mahenge wameishukuru serikali kwa kutatua kero ya
usafiri kwa Maofisa hao huku wakiahidi kutunza vyombo hivyo.
SAKINA ABDULMASOUD,DODOMA.
No comments:
Post a Comment