Matokeo chanyA+ online




Monday, February 13, 2023

WAKULIMA RUVUMA WAINGIZA BILIONI 644 BAADA YA KUUZA KAHAWA NA KOROSHO

Shehana ya kahawa iliyokobolewa na nyingine ikiendelea kukobolewa katika kiwanda cha kukoboa kahawa cha DAE LTD mjini Mbinga



Katikati mwenye tabasamu ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas alipotembelea na kukagua kiwanda cha kukoboa Kahawa cha DAE LTD mjini Mbinga

Wakulima Ruvuma waingiza bilioni 644 kwa kahawa na korosho

Wakulima mkoani  Ruvuma waingiza zaidi ya shilingi bilioni 644 baada  kuuza mazao ya kahawa na korosho kwenye  misimu mitano mfululizo.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema Mkoa wa Ruvuma kwa vipindi vya misimu ya kilimo mitano mfululizo kutoka msimu wa kilimo 2017/2018  hadi kufikia msimu 2020/2021 jumla ya kilo 77,664,927.75 za kahawazilikusanywa.

Amesema kilo hizo  ziliuzwa kwa watani wa bei sh. 4,638 na kuwapatia wakulima  wa kahawa zaidi ya shilingi bilioni  353.

Amebainisha kuwa kati ya fedha hizo,msimu wa mwaka 2016/2017  zilinunuliwa kilo  15,393.500 zilizowaingizia wakulima zaidi ya shilingi bilioni 66 na kwamba msimu wa 2017/2018 zilinunuliwa kilo 20,162,900 na kuwaingizia  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 74.

Kwa mujibu wa Kanali Thomas katika msimu wa mwaka 2018/2019 zilinunuliwa kilo 15,675,100 zilizowaingiza  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 64,msimu wa mwaka 2019/2022 zilinunuliwa kilo 12,676,844 zilizowaingiza wakulima zaidi ya shilingi bilioni 50  na kwamba mwaka 2020/2021  zilinunuliwa kilo 15,756,583.75 na kuwaingiza  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 97. 

 

No comments:

Post a Comment