Matokeo chanyA+ online




Monday, May 8, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Organ Troika, SADC Troika na Nchi zinazochangia Vikosi vya Jeshi katika Force Intervention Brigade (FIB)

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama pamoja na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wakati Wimbo wa Taifa wa Namibia pamoja na ule wa SADC ukiimbwa kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Dharura wa Wakuu hao wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Organ Troika, SADC Troika na Nchi zinazochangia Vikosi vya Jeshi katika Force Intervention Brigade (FIB) Windhoek nchini Namibia tarehe 08 Mei, 2023.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Organ Troika, SADC Troika na Nchi zinazochangia Vikosi vya Jeshi katika Force Intervention Brigade (FIB)




NUKUU UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA YA KILIMO 2022/2023











 

Saturday, May 6, 2023

RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIONGOZA KIKAO CHA VIONGOZI MBALIMBALI WA SERIKALI KINACHOHUSU KUANZA KWA MCHAKATO WA KATIBA MPYA IKULU CHAMWINO MKOANI DODOMA







 

MAKAMU WA RAIS AKIWASILI BUJUMBURA BURUNDI MEI 06 2023


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Melchoir Ndadaye uliopo Bujumbura nchini Burundi na kupokelewa na Makamu wa Rais wa Burundi Mheshimiwa Prosper Banzombaza leo tarehe 06 Mei 2023. Makamu wa Rais anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 11 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Mpango wa Amani, Usalama na Ushirikiano kwaajili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Ukanda wa Maziwa Makuu unaofanyika Bujumbura nchini Burundi.


Kamishna wa Idara ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. David Kafulila, akizungumza wakati akifunga rasmi kikaokazi kati ya Serikali na Wataalam kutoka Taasisi ya Benki ya Dunia inayojihusisha na utoaji wa mikopo na misaada ya kiufundi kwa Sekta Binafsi - International Finance Corporation (IFC), kilicholenga kupitia na kujadili miradi ya kimkakati ambayo Serikali inataka itekelezwe kwa njia ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), kilichofanyika kwa siku 5 katika Ukumbi wa Hazina Ndogo, jijini Dar es Salaam.


Afisa Mwandamizi wa Uwekezaji na Huduma za Ushauri wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) kutoka Taasisi ya Benki ya Dunia inayojihusisha na utoaji wa mikopo na misaada ya kiufundi kwa Sekta Binafsi - International Finance Corporation (IFC) Bi. Ramatou Magagi, akifundisha namna ya kuandaa miradi ya PPP, manunuzi Pamoja na namna ya kuandaa mikataba bora ya miradi ya ubia, kwa wataalam wa kitanzania kutoka TANESCO, TPA, DART, TRC, TANROADS, Wizara ya Madini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Vyuo vikuu vya Mzumbe na UDSM, TGDC na TPDC wakati wa kikaokazi kinachoendelea katika Ofisi Ndogo za Hazina Jijini Dar es Salaam, kikihusisha Serikali na Wataalam hao kutoka IFC.

Afisa Mwandamizi wa Uwekezaji Sekta ya Kimataifa ya Nishati kutoka Taasisi ya Benki ya Dunia inayojihusisha na utoaji wa mikopo na misaada ya kiufundi kwa Sekta Binafsi - International Finance Corporation (IFC) Bw. Stefan Rajaonarivo, akifundisha namna bora ya kuandaa miradi ya nishati kupitia njia ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) kwa wataalam wa kitanzania kutoka TANESCO, TPA, DART, TRC, TANROADS, Wizara ya Madini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Vyuo vikuu vya Mzumbe na UDSM, TGDC na TPDC wakati wa kikaokazi kinachoendelea katika Ofisi Ndogo za Hazina Jijini Dar es Salaam, kikihusisha Serikali na Wataalam hao kutoka IFC.
Mtaalam wa masuala ya Ubia kutoka Taasisi ya Benki ya Dunia inayojihusisha na utoaji mikopo na misaada ya kiufundi kwa Sekta Binafsi - International Finance Corporation (IFC) Bi. Caroline Eric, akifundisha namna ya kuandaa miradi bora na yenye sifa ya kuvutia mitaji kutoka sekta binafsi (PPP) kwa wataalam wa kitanzania kutoka TANESCO, TPA, DART, TRC, TANROADS, Wizara ya Madini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Vyuo vikuu vya Mzumbe na UDSM, TGDC na TPDC wakati wa kikaokazi kinachoendelea katika Ofisi Ndogo za Hazina Jijini Dar es Salaam, kikihusisha Serikali na Wataalam kutoka IFC.

Wadau mbalimbali wa masuala ya Ubia kutoka taasisi mbalimbali za Serikali wakimsikiliza kwa umakini Kamishna wa Idara ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. David Kafulila akifunga rasmi kikaokazi kilichofanyika kwa siku 5 kati ya wataalam hao wa Serikali na Wataalam kutoka Taasisi ya Benki ya Dunia inayojihusisha na utoaji wa mikopo na misaada ya kiufundi kwa Sekta Binafsi - International Finance Corporation (IFC), katika Ofisi Ndogo za Hazina Jijini Dar es Salaam, kikihusisha Serikali na Wataalam hao kutoka IFC.


 

KATIKA KUDHIBITI KELELE NA MITETEMO HAYA HAPA MAELEKEZO YA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ALIYOYATOA TAREHE 6 MEI 2023 KUONDOA UTATA WA MADHEHEBU YA DINI NA MAMLAKA YA UDHIBITI WA MAZINGIRA NEMC JUU YA JAMBO HILO













 

Friday, May 5, 2023

MSD YAFANYA MABORESHO UPATIKANAJI BIDHAAA ZA AFYA NCHINI

 KatibuTawala  Mkoa wa Singida, Dk.Fatma Mganga akifungua mkutano wa wadau wa Bohari ya Dawa (MSD) uliofanyika Mei 3, 2023 mjini Singida. Kulia ni Meneja wa MSD Kanda ya Kati, John Sipendi na kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk.Victorina Ludovick. 

Na Dotto Mwaibale, Singida 

BOHARI ya Dawa (MSD) imefanya maboresho katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuingia mikataba ya muda mrefu na wazalishaji ili kurahisisha upatikanaji wa bidhaa za afya nchini. 

Hayo yamesemwa na Meneja wa MSD Kanda ya Kati, John Sipendi wakati akimkaribisha mgeni rasmi KatibuTawala wa Mkoa wa Singida, Dk.Fatma Mganga kufungua mkutano wa wadau wa MSD uliofanyika mjini hapa hivi karibuni na kuhudhuriwa na Mganga Mkuu wa mkoa, Waganga Wakuu wa Wilaya,Wafamasia,Wataalam wa maabara na viongozi wa MSD.

Sipendi alisema ili kufikia dira na kutimiza dhima na malengo yake, MSD inadumisha na kusimamia mfumo wenye tija wa ununuzi, utunzaji na usambazaji wa bidhaa za afya kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya vya umma nchini na baadhi ya binafsi vilivyoidhinishwa na Wizara ya Afya. 

Alitaja kazi nyingine ni kutumia ujuzi, weledi, mbinu, taratibu na ushauri wa kitaalamu katika kusimamia na kudhibiti utunzaji na usambazaji wa bidhaa za afya. 

Alitaja eneo lingine ni kufuatilia mahitaji ya bidhaa za afya na kusimamia usambazaji wake katika vituo vya kutolea huduma za afya, huduma za afya katika vituo vya umma na kuboresha pale inapobidi na kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa za afya zinapatikana kwa wakati. 

Sipendi aliongeza kuwa ili kuhakikisha hayo  yote yanafanikiwa, MSD imefanya maboresho kwa kukasimu  baadhi ya madaraka na majukumu kwa kanda ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu katika eneo hilo.

Aidha, MSD imeanza kusambaza bidhaa za afya mara sita kutoka mara nne ya awali na kuwezesha kuboresha mifumo ya ndani ya utendaji, kuboresha huduma na mawasiliano na wateja.

Alisema kutokana na serikali kutenga na kuleta fedha za kununulia bidhaa za afya kama ilivyopanga, upatikanaji wa bidhaa za afya umepanda kutoka asilimia 54 iliyokuwepo mwishoni mwa mwaka jana na kufikia asilimia 76 sasa, kuongeza wataalamu ili kuweza kuwa na fani mbalimbali kuendana na majukumu ya MSD.

Pia Sipendi alisema MSD imeweza kufanikisha kusambaza vifaa vya uzazi pingamizi wa mama na mtoto (CEmONC), vifaa vya maabara na mashine za kusafisha damu kwa baadhi ya hospitali kama vile Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dk.Mganga alisema mkutano huo umelenga kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba na kujadili changamoto  zinazovikabili vituo vya afya vya kutolea huduma ili ziweze kupangiwa maazimio na mikakati ambayo itamsaidia mteja au mwananchi kupata huduma iliyo bora. 

“Mheshimiwa Rais wetu Dk.Samia Suluhu Hassan ametoa kipaumbele kikubwa katika sekta ya afya kwa kutoa fedha nyingi za kujenga Hospitali za  Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati , tumejenga majengo ya wagonjwa mahututi (ICU) majengo ya kupata huduma ya dharura ambayo ni ya kisasa,” alisema Dk.Mganga.

Alisema Serikali imefanya yote hayo ili kuwawezesha wananchi kupata huduma bora na za uhakika.

Aidha, Dk.Mganga  alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais Samia kwa kufanya kipengele chake na kilichobakia ni kwa wadau, MSD na wafanyakazi kuboresha pale ambapo amekomea na wanalojukumu la kuhakikisha mgonjwa anapata matibabu bora.

Aliongeza kuwa kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi  wanapoambiwa dawa hakuna na jambo ambalo linatokana na madaktari kukalili dawa aina moja wakati magonjwa yaliyo mengi yanatibiwa zaidi ya dawa moja.

"Dawa inaweza kutolewa kama mbadala na kuondoa dhana ya wananchi kuichukia Serikali yao pale wanapoambiwa dawa hakuna, madaktari nawaomba  kabla ya kumuandikia mgonjwa dawa mjue akiba za dawa zilizopo ili kuondoa malalamiko ya wananchi.

SWEDEN YAONESHA NIA YA UWEKEZAJI KWENYE BIASHARA NCHINI

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa pili kushoto), akizungumza jambo wakati wa Mkutano wake na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Charlotta Ozaki Macias, uliofanyika jijini Dodoma.
Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Charlotta Ozaki Macias, akiipongeza Serikali kwa juhudi mbalimbali za maendeleo, wakati wa mkutano na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani), jijini Dodoma.
 


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akieleza kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na Sweden, wakati wa Mkutano kati yake na Balozi wa nchi hiyo nchini Tanzania, Mhe. Charlotta Ozaki Macias, jijini Dodoma.



Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameishukuru Sweden kwa misaada mbalimbali iliyoweka alama chanya katika maendeleo ya kiuchumi katika sekta ya nishati, elimu na masuala ya demokrasia.

 Amesema hayo jijini Dodoma, wakati wa mkutano wake na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Charlotta Ozaki Macias, ulioangazia ushirikiano wa maendeleo kati ya nchi hizo mbili.

Alisema kuwa misaada inayotolewa na nchi hiyo kwa upande wa mazingira, mabadiliko ya tabia nchi, usawa wa kijinsia, elimu na nishati vinaenda sambamba na ajenda ya Taifa ya maendeleo ikiwemo Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025.

“Utakumbuka kabla ya changamoto ya Covid 19 na Vita ya Rusia na Ukraine, uchumi wa Tanzania ulikuwa unakua kwa takribani asilimia saba, ukuaji huo ulitokana na juhudi zilizofanywa na Serikali ya Tanzania na Washirika wa Maendeleo ikiwemo Sweden, hivyo nchi yako imeweka alama katika kuinua maisha ya watanzania”, alisema, Dkt. Nchemba. 

Amesema Tanzania katika kukabiliana na changamoto za kiuchumi baada ya Covid 19 na Vita ya Risia na Ukraine, imechukua hatua kadhaa ikiwemo kutoa ruzuku kwenye mafuta na kwenye sekta kilimo.

Alisema juhudi zinazoendelea kufanywa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, hadi mwaka 2027 uchumi wa Tanzania unatarajia kukua kwa asilimia saba. 

Kwa upande wake Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Charlotta Ozaki Macias aliipongeza Serikali kwa kuchochea ukuaji wa uchumi, akieleza kuwa licha ya kuwepo kwa mabadiliko ya viongozi na Sera lakini bado kumekuwepo na ushirikiano ambao ni imara katika kupunguza umasikini na ujenzi wa miundombinu nchini.

Alisema kuwa nchi yake itaendeleza ushirikiano wa maendeleo hususani kwenye eneo la biashara kati ya nchi hizo mbili kwa kuwa wamefanya utafiti na kugundua kwa kiasi kikubwa mazingira ya kibiashara Tanzania  ni mazuri.

Alisema anauzoefu mkubwa katika masuala ya kibiashara kupitia nchi nyingine kwenye kutumia usafiri wa umma katika kusaidia uchumi hususani katika miji ambayo inamsongamao wa watu na ongezeko la watu.

UJUMBE KUTOKA DRC WATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Mkurugenzi wa Forodha na Ushuru wa bidhaa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayesimamia majimbo ya Haut Katanga, Lualaba, Tanganyika na Lomami, Bw. René Kalala Masimango na ujumbe wake upo nchini kwa ziara ya kikazi ambapo tarehe 04 Mei 2023 ulikutana na Uongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar Es Salaam.

 

Akizungumzia kuhusu ziara hiyo, Balozi wa Tanzania nchini DRC, Mhe. Said Mshana alisema ubalozi wake umeiandaa kwa lengo la kuwakutanisha wadau wa Tanzania na DRC ili wajadili na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazokwamisha biashara kati ya nchi hizo mbili.

 

Wakati wa kikao na uongozi wa TPA, Bw. Masimango alisema Bandari ya Dar es Salaam ni muhimu sana kwa mizigo ya Congo na inahudumia mizigo mingi, hivyo ziara yake ni kujionea utendaji kazi wa Bandari na ameridhika kuwa kazi zinazofanywa na mamlaka hiyo ni nzuri na zimepangiliwa vizuri.

 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw. Plasduce Mkeli Mbossa ameahidi kuwa Menejimenti yake ipo tayari kutatua changamoto zozote zitakazojitokeza katika kuhudumia shehena ya mizigo inayoenda na kutoka Congo kupitia Bandari za Tanzania kwa lengo la kulinda uhusiano mzuri na wa muda mrefu wa kidiplomasia na biashara kati ya nchi hizi mbili. 


“Menejimenti ya TPA itaendelea kuzifanyia kazi changamoto zozote katika kuhudumia shehena ya Congo na kuimarisha uhusiano ili shughuli zinazofanywa na TPA katika bandari zake ziwe na manufaa kwa DRC.” Alisema Bw. Mbossa. 


Naye Balozi wa DRC nchini Tanzania, Mhe. Jean Pierre Massala amesema ziara hiyo ni muhimu kwa uhusiano kati ya DRC na Tanzania na muhimu ni kufanya kazi kwa pamoja kwa faida ya nchi hizi mbili. 


Ujumbe huo wa DRC unaendelea na ziara yake nchini na leo tarehe 05 Mei 2023 umepanga kutembelea Bandari Kavu ya Kwala na Reli ya Kisasa ya SGR.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mkeli Mbossa akitoa maelezo kwa ujumbe wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ukiongozwa na Mkurugenzi wa Forodha na Ushuru wa bidhaa  anayesimamia majimbo ya Haut Katanga, Lualaba, Tanganyika na Lomami, Bw. René Kalala Masimango ulipotembelea bandari ya Dar Es Salaam 


Balozi wa Tanzania nchini DRC, Mhe. Said Mshana (kushoto) akizungumza wakati wa kikao baina ya ujumbe wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ukiongozwa na Mkurugenzi wa Forodha na Ushuru wa bidhaa anayesimamia majimbo ya Haut Katanga, Lualaba, Tanganyika na Lomami, Bw. René Kalala Masimango na uongozi wa TPA. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mkeli Mbossa 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mkeli Mbossa (wa nne kulia) na Balozi wa Tanzania nchini DRC, Mhe. Said Mshana (katikati) katika picha ya pamoja na ujumbe wa DRC uliotembelea Bandari ya Dar Es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mkeli Mbossa akiwapitisha maeneo mbalimbali ya Bandari ya Dar Es Salaam  ujumbe wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ukiongozwa na Mkurugenzi wa Forodha na Ushuru wa bidhaa anayesimamia majimbo ya Haut Katanga, Lualaba, Tanganyika na Lomami, Bw. René Kalala Masimango ulipotembelea bandari hiyo