Serikali
imekamilisha ujenzi wa meli mpya ya MV Mbeya yenye uwezo wa kubeba abiria 200
na mizigo tani 200 katika Ziwa Nyasa mkoani Mbeya.
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango wakati akiwasilisha
mapendekezo ya serikali ya mpango wa
maendeleo wa taifa
na
ya kiwango na ukomo wa bajeti ya
serikali kwa mwaka 2020/21 mjini Dodoma
Waziri
Mpango amesema kuwa kwa sasa ujenzi wa meli mpya yenye uwezo wa kubeba abiria
1,200 na tani 400 za mizigo katika Ziwa Victoria utekelezaji wake umefikia asilimia 52 na ujenzi wa chelezo
umefikia asilimia 80.
Aidha, amesema kuwa ukarabati wa meli ya MV Victoria umefikia asilimia 75 na MV
Butiama asilimia 70 ambapo awamu ya
kwanza ya upanuzi wa maegesho ya Magogoni - Kigamboni umekamilika.
Akizungumzia jengo la abiria na ofisi ya kivuko cha Lindi
– Kitunda amesema umekamilika na kukabidhiwa.
Aidha, Waziri Mpango amesema kuwa vivuko vya MV
Kigamboni, Kigongo – Busisi na MV Utete pia vimekamilika ambapo kwa sasa ujenzi
wa vivuko vipya vya Nyamisati - Mafia umefikia asilimia 28, Bugolora - Ukara (asilimia
40), Chato - Nkome na Kayenze Bezi umefikia asilimia 98.
Akitaja
shughuli nyingine ni kununuliwa kwa
kivuko kipya chenye uwezo wa kubeba tani 170 Magogoni - Kigamboni kuendelea
na ukarabati wa vivuko vya MV Sengerema ambao umefikia asilimia 70 na MV
Misungwi umefikia asilimia 20.
Ambapo
jumla ya shilingi bilioni 81.5
zimetumika kugharamia ujenzi na ukarabati wa meli na vivuko ikijumuisha
shilingi bilioni 38.8 zilizotolewa katika kipindi cha Julai 2019 hadi Januari
2020.
No comments:
Post a Comment