|  | |
| Waziri wa Nishati Medard Kalemani akizungumza kabla ya kuwasha umeme katika vijiji vya Matare na Nkuhi vilivyopo jimbo la Singida Mashariki,kulia kwake ni Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu na kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo. | 
|  | 
| Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu akizungumza katika ziara ya Waziri wa Nishati Medard Kalemani jimboni humo. | 
|  | 
| Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani akitoa maagizo kwa wakandarasi wa umeme akiwa katika ziara wilayani Ikungi ambapo aliwasha umeme katika vijiji viwili vya Matare na Nkuhi. | 
|  | 
| Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu akizungumza mbele ya Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani na Mkuu wa wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo. | 
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani amewasha umeme 
katika vijiji viwili vya Matare na Nkuhi vilivyopo jimbo la Singida 
Mashariki Mkoani Singida na hivyo kufanya jumla ya vijiji 19 kati ya 50 
sawa na asilimia 38 kupata huduma ya umeme jimboni humo.
Ili
 kukamilisha ahadi ya serikali ya kuhakikisha wanafikisha umeme vijijini
 Dkt Kalemani ametoa agizo kwa Shirika la Umeme Nchini(TANESCO) 
kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja wanaweka umeme kwenye vijiji vingine 11
 vilivyopo katika jimbo hilo
Dkt
 Kalemani ametoa maagizo hayo wilayani Ikungi akiwa katika ziara ya 
kukagua miradi ya umeme ambapo pia ameagiza TANESCO Singida kumsimamia 
mkandarasi aanze kusimika nguzo mapema katika Tarafa ya Mungaa 
Lighwa,Ntuntu,Misughaa na Kikio ili umeme uwashwe kwenye Vijiji kabla ya
 mwezi June mwaka huu
"Nampongeza
 Sana Mbunge wenu Mhe Miraji Mtaturu, kwani anafuatilia sana miradi ya 
wananchi wake,tangu amechaguliwa na kuapishwa ni miezi mitano tu lakini 
mnaona mambo yalivyo, leo tu tumewasha vijiji viwili je angekaa miaka 
minne hali ingekuwaje?,"alihoji Dkt Kalemani.
Ili
 kuharakisha kazi hiyo amesema," Ndugu zangu Ugonjwa huu wa homa kali ya
 mapafu(COVID 19)usikwamishe kazi za kuunganishia umeme wananchi ila 
mfanye kazi kwa tahadhari,Rais Dkt John Magufuli ameidhinisha sh Bilion 
40 kwa Mkoa wa Singida ili kutekeleza miradi hii hivyo ni lazima 
tuisimamie,"alisema Dkt Kalemani.
Pamoja
 na hayo Dkt Kalemani amesisitiza wananchi kutolipishwa nguzo na gharama
 za kuunganishiwa umeme amesema ni sh 27,000 tu na sio vinginevyo.
"Katika
 hili niagize hapa mkandarasi wa Cyba Contractors Ltd ya jiji Mbeya 
aliyelalamikiwa kuwatapeli wananchi baada ya kuchukua pesa zao na 
hajafanya wiring mpaka sasa atafutwe,"aliagiza Dkt Kalemani.
Awali
 akizungumza katika ziara hiyo,Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo 
amesema katika kata 28 zilizopo wilayani humo,ni kata 18 tu ndio 
zimefikiwa na umeme hivyo kumuomba waziri aendelee kuwasaidia.
"Mh
 Waziri kwanza nikupongeze na kukushukuru kwa kazi nzuri ya kusimamia 
miradi ya umeme,wilaya ya Ikungi tulipewa Vijiji 30 na 
vimeshaunganishiwa umeme,lakini waswahili wanasema kushukuru ni kuomba 
tena,mh waziri naomba uendelee kutusaidia wananchi wa Ikungi tupate 
umeme katika maeneo yote,"aliomba mkuu wa wilaya hiyo.
Amesema
 katika wilaya hiyo viongozi wa serikali,chama na wabunge wote wawili 
wanafanya kazi kwa ushirikiano hali inayopelekea kurahisisha upelekaji 
wa maendeleo kwa wananchi.
Kwa upande wake mbunge Mtaturu amemshukuru
Rais 
 Magufuli kwa dhamira yake ya dhati ya kuwaletea wananchi maendeleo 
kwani aliahidi kuwafikishia umeme wananchi na utekelezaji wa ahadi hiyo 
unaonekana.
"Sisi 
wananchi wa Singida Mashariki na Ikungi kwa ujumla tunatoa shukrani za 
pekee kwake,miradi mingi tunaiona inatekelezwa,na tunaahidi kumpa kura 
za kishindo katika uchaguzi mkuu ujao,"alishukuru mbunge huyo.
Amempongeza Dkt Kalemani kwa kumsaidia Rais Magufuli kusimamia sekta ya Nishati kwani miradi inaenda vizuri nchi nzima.
"Pamoja
 na shukrani hizo mh waziri Tarafa ya Ikungi kwenye vijiji vya 
Manjaru,Tumaini,Ng'ongosoro, Matongo,Kimbwi,Unyang'ongo na Mbwanjiki 
vipo barabarani havina umeme kwa muda mrefu pamoja na miundombinu kuwepo
 jirani,"aliongeza Mtaturu.
Nae
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Wilaya ya Ikungi Mika Likapakapa 
ameipongeza serikali kupitia Rais Dkt Magufuli kwa kuendelea kutekeleza 
Ilani ya uchaguzi ya chama hicho vizuri na kuomba Vijiji vilivyosalia 
vikamilishiwe kuwekewa umeme.
 
No comments:
Post a Comment