Matokeo chanyA+ online




Thursday, August 27, 2020

AMSHA AMSHA YA UHURU FM KUELEKEA DODOMA, YAKUTANA NA MGOMBEA UBUNGE WA CHALINZE

 


 Mgombea Ubunge wa Jimbo la chalinze Ridhiwani Kikwete (njano) akizungumza jambo na Kikosi kazi cha Amsha Amsha ya Uhuru FM maeneo ya Chalinze wakati kikielekea jijini Dodoma leo.

Na Pius Ntiga-Chalinze

Mgombea Ubunge wa Jimbo la chalinze Ridhiwani Kikwete ametaja mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika Jimbo Hilo kwa kuainisha mafanikio hayo ikiwemo kuanzisha kwa viwanda vikubwa vitatu.

Katika mahojiano na Uhuru FM kupitia kampeni yake ya AMSHA AMSHA Dodoma ikiwlekea mikakati mikubwa ya maendeleo, Ridhiwani amesema kuptia viwanda hivyo kumeleta tija ya kupatikana kwa ajira kwa zaidi ya asilimia 80 ya wananchi wakiwemo vijana wa chalinze ambao nao wamefurahia upatikanaji wa ajira hizo.

Kuhusu matibabu zaidi ya asilimia 40 ya wazee wamepatiwa vitambulisho vya bima ya Afya AMBAYO vinawasaidia katika kupata matibabu kuptia Hospitali ya kisasa iliyopo katika Jimbo la chalinze na maeneo mengine.

Mwaka 2015 amesema kulikuwa na changamoto ya vifo kwa Akina mama vinavyotokana na uzazi ambapo sasa ndani ya miaka mitano chini ya serikali ya awamu ya tano Hali hiyo haipo Tena  kwani Kuna kituo kitubwa Cha afya kipo miono na lugoba ambapo sasa Kuna asilimia 3 tu ndio inayotoka na vifo vya Akina mama wajawazito.

Kutokana na mafanikio hayo AMBAYO pia yamejielekeza katika sekta ya Afya na utalii Ridhiwani amewaomba wananchi wa chalinze kumchagua ili aendeleze mafanikio makubwa yaliyopatikana na.kuhakikisha aliyopatikana maendeleo yanaendelea,Pia amewaomba wananchi wamchague Rais John Magufuli kwa kumpigia Kura za ndio katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment