Matokeo chanyA+ online




Monday, February 6, 2023

BILIONI 14 ZAJENGA SHULE MPYA 11 NA VITUO VYA AFYA 12 RUVUMA







 SERIKALI ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu

Hassan imetoa zaidi ya shilingi bilioni 14 kujenga shule mpya za sekondari

11 na vituo vya afya 12 mkoani Ruvuma.

 

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema Mkoa

umefanikiwa kujenga shule hizo mpya katika Halmashauri zote nane za

Mkoa wa Ruvuma kwa gharama ya shilingi Bilioni 7.7.

 

“Ujenzi huu unajumuisha shule ya Mkoa ya Wasichana inayojengwa eneo

la Migelegele Kata ya Lwinga katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

kwa gharama ya shilingi bilioni nne’’,alisema Kanali Thomas.

Hata hivyo amesema Mkoa umefanikiwa kujenga vyumba vya madarasa

792 elimu msingi na sekondari yakijumuisha madawati, viti na meza kwa

gharama ya Shilingi Bilioni 14.93

 

Kwa mujibu wa Kanali Thomas,Mkoa umefanikiwa kujenga mabweni

matano ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kwa gharama ya

shilingi Milioni 640 na kwamba Mkoa ulipokea fedha kiasi shilingi milioni

400 kwa ajili ya ukamilishaji wa Maabara 23 za Shule za Sekondari kupitia

fedha za Tozo na Serikali Kuu.

Akizungumzia kuhusu sekta ya Afya na Ustawi wa Jamii,Kanali Thomas

amesema Mkoa wa Ruvuma umefanikiwa kujenga Vituo vya Afya 12

kupitia fedha za Tozo na Serikali Kuu kwa gharama ya zaidi ya shilingi

bilioni 7.8.

Ameongeza kuwa Mkoa umefanikiwa kujenga nyumba tisa za watumishi

wa Afya kwa gharama ya shilingi Milioni 856 na kwamba Mkoa

 

umefanikiwa kujenga majengo matatu ya huduma za dharura (EMD) Kwa

gharama ya Shilingi Milioni 900.

 

Kulingana na Kanali Thomas Mkoa wa Ruvuma umefanikiwa kujenga jengo

moja la wagonjwa mahututi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa

gharama ya shilingi milioni 250 na kujenga zahanati 21 kwa gharama ya

zaidi ya shilingi bilioni moja.

 

Hata hivyo amesema Mkoa wa Ruvuma unaendelea na ujenzi wa Hospitali

tano za Wilaya ya Nyasa, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Halmashauri

ya Madaba na Halmashauri ya Songea kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.4

 

Amesema serikali pia inatekeleza mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya

Mkoa awamu ya kwanza katika eneo la Mwengemshindo Manispaa ya

Songea kwa gharama ya shilingi bilioni 2.7.

 

Amesema ujenzi wa hospitali hiyo unahusisha jengo la wagonjwa wa nje

(OPD), jengo la mionzi na nyumba ya mtumishi na kuongeza kuwa hali ya

upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi katika vituo vya kutolea

huduma za afya upatikanaji umeongezeka na kufikia asilimia 96.

 

 

No comments:

Post a Comment