Pia, Mch. Hananja ameeleza kuwa Serikali ya awamu ya sita imefanya kazi kubwa kwa kuongeza bajeti ya tiba, ujenzi wa vituo vya afya ya akili na huduma za tiba mbadala kwa waraibu.
Aidha, ametoa wito kwa wazazi, viongozi wa dini, walimu na jamii nzima kushirikiana katika kutoa elimu ya mapema kwa vijana kuhusu madhara ya dawa hizo, akibainisha kuwa kinga ni silaha madhubuti kuliko tiba. “Hatupaswi kusubiri vijana wetu waanguke kwenye janga hili ndipo tuingilie kati elimu, maombi, na ufuatiliaji wa karibu ni njia muhimu ya kuzuia,” amesisitiza.
Mch. Hananja amehimiza ushirikiano baina ya taasisi za dini, mashirika ya kiraia na Serikali katika kuhakikisha Taifa linaibuka na kizazi salama, kisichoathirika na matumizi ya dawa za kulevya.
Kauli mbiu: "Wekeza kwenye Kinga na Tiba dhidi ya dawa za kulevya"
No comments:
Post a Comment