Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta
Nditiye,akizungumza wakati wa kufungua kikao kazi cha wadau wa TEHAMA
kutoka sekta ya Umma,Binafsi na Taasisi za Elimu ya Juu wa Ufundi
kilichofanyika leo kwenye ukumbi wa ndaki ya TEHAMA Chuo Kikuu cha
Dodoma (UDOM)
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Dkt.Jim Yonazi
akitoa taarifa wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha wadau wa TEHAMA
kutoka Sekta ya ya Umma,Binafsi na Taasisi za Elimu ya Juu wa Ufundi
kilichofanyika leo kwenye ukumbi wa ndaki ya TEHAMA kilichopo Chuo Kikuu
cha Dodoma (UDOM)
Mwakilishi kutoka sekta binafsi Bw.Mugeta Mujungu akitoa taarifa katika kikao kikao
kazi cha wadau wa TEHAMA kutoka Sekta ya ya Umma,Binafsi na Taasisi za
Elimu ya Juu wa Ufundi kilichofanyika leo kwenye ukumbi wa ndaki ya
TEHAMA kilichopo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Baadhi ya wadau kutoka sekta mbalimbali wakifuatlia mada zilizokuwa zikitolewa katika
kikao kazi cha wadau wa TEHAMA kutoka sekta ya Umma,Binafsi na Taasisi
za Elimu ya Juu wa Ufundi kilichofanyika leo kwenye ukumbi wa ndaki ya
TEHAMA Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na
Mawasiliano,Atashasta Nditiye akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa
TEHAMA kutoka Sekta binafsi,Taasisi za Utafiti na Elimu ya Juu na
Ufundi.
Serikali imesema kuwa
idadi ya watumiaji wa Internent imeongezeka kutoka 520,000 mwaka 2009 na
kufikia zaidi ya watu milioni 23 kwa mwaka 2018 hii ni kutokana na
jitahidi za wadau mbalimbali katika sekta ya tehama.
Hayo yamebainishwa leo
jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na
Mawasiliano,Atashasta Nditiye wakati akifungua kikao cha wadau wa
Tehama kutoka sekta binafsi,taasisi za utafiti na elimu ya juu na ufundi
amesema kuwa juhudi za Serikali zimepelekea kuongezeka kwa watumaji wa
internent kutoka 520,000 kwa mwaka 2009 hadi kufikia zaidi ya
watu milioni 23 kwa mwaka 2018.
Naibu Waziri amesema kuwa watumaaji hao ni zaidi ya lengo walilojiwekea la kufikia watumiaji milioni 20 ifikapo mwaka 2020.
Aidha amesema kuwa
katika kutekeleza sera ya Taifa ya tehama Serikali imeendelea kutekeleza
program mbalimbali pamoja na ujenzi wa mkongo wa Taifa,ujenzi wa kituo
cha kimataifa cha kukusanya data,pamoja na kuanzisha huduma za seriakli
mitandao.
Nditiye amesema kuwa
Serikali inatambua jitihada zinazofanywa na sekta binafsi katika kukuza
mawasiliano ikiwemo ujezni wa mkongo wa taifa ambao umeongeza mchango
katika pato la taifa.
Hata hivyo amesema kuwa
mkongo huo uliojengwa nchini wenye zaidi ya kilomita 26,000, Serikali
pekee imejenga kilomita 7560 ambapo kilomita zingine zimejengwa kwa
mchango wa sekta binafsi.
Kaimu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Dk Jimmy Yonazi amesema lengo
la mkutano huo ni kushirikiana katika kuelewa sera ya tehama
inachangiaje katika uchumi wa viwanda.
“Kutambua na
kushirikiana na sekta binafsi,kupokea maoni ya wadau ili kubaini maeneo
ya kufanya marejeo na kutafuta utaratibu wa kushirikiana kati ya
serikali na sekta binafsi,”amesema Dkt. Yonazi.
Naye Mwakilishi wa sekta
binafsi,Mugeta Mujungu amesema kuwa changamoto kubwa wanayokutana nayo
ni sekta binafsi kutoshirikishwa wakati wa uandaaji wa sera mbalimbali.Picha na Alex Sonna-Fullshangweblog
No comments:
Post a Comment