Naibu 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas 
Ndumbaro akiwasilisha pendekezo la Kiswahili kutumika katika ukanda wa 
maziwa makuu mjini Brazzaville jana

Naibu 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas 
Ndumbaro akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola, Vicente 
Muanda wakiwa katika ukumbi wa mikutano, mjini Brazzaville jana

Balozi
 wa Tanzania Nchini DRC Luteni. Jen. Paul Mella akimueleza jambo balozi 
wa sudan wakati wa mkutano wa ukanda wa maziwa makuu mjini Brazzaville 
jana

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu wakifuatilia mkutano ulifanyika jana Brazzaville jana

Mawaziri
 wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu wakiwa 
katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kongo, Bwn. Clement 
Mouamba jijini Brazzaville jana
…………………….
Na Mwandishi wetu, Brazzaville,
Katika
 jitihada za kukuza lugha ya Kiswahili barani Afrika, Tanzania imeziomba
 nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu kuanza kutumia lugha ya 
Kiswahili kama lugha rasmi na lugha ya kazi
Wito 
huo umetolewa katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi 
wanachama wa ukanda wa maziwa makuu, uliofanyika mjini Brazzaville leo 
na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt.
 Damas Ndumbaro 
“Tumewaomba
 wenzetu wa maziwa makuu wakubali lugha ya Kiswahili kutumika kama lugha
 rasmi na lugha ya kazi katika nchi zote za maziwa makuu. Pia nchi sita 
ambazo zipo hapa na hazijaridhia mabadiliko ya mkataba wa Afrika 
kuruhusu Kiswahili kutumika kama lugha rasmi katika Afrika (AU) nchi 
hizo zimetuhakikishia kuwa zitaridhia mabadiliko hayo ili kuhakikisha 
kuwa Kiswahili kinaanza kutumika kama lugha rasmi ya kazi,” Alisema Dkt.
 Ndumbaro
Kwa 
mujibu wa Waziri Ndumbaro, matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ukanda 
huo ni fursa ambayo italeta umoja wa kitaifa, na katika ukanda wa maziwa
 makuu lakini pia umuhimu wa Kiswahili kwamba ni lugha pekee ambayo 
haina uhusiano na ukoloni barani afrika. 
“Tunatumaini
 kwamba tutazipata sahihi za nchi sita na tukisha zipata tutabakiwa na 
sahihi ya nchi moja tu ili Kiswahili kiwe rasmi lugha ya kazi katika 
mikutano itakayo kuwa inafanyika barani Afrika,” aliongeza Dkt. 
Ndumbaro 
Nchi 
sita ambazo hazijaridhia mabadiliko ya mkataba wa Afrika kuhakikisha 
kuwa Kiswahili kinatumika kama lugha rasmi ya kazi ni pamoja na Angola, 
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sudani, Uganda na Zambia. 
Kwa 
sasa hivi ni lugha rasmi lakini siyo lugha ya kazi kwa hiyo tumekwenda 
vizuri kwenye Kiswahili tunaamini ni fursa nzuri ya kuanza kukuza lugha 
ya Kiswahili katika bara la Afrika
Wakati
 huo huo, Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa, katika mkutano huo nchi 
wanachama waliweza kuongelea agenda kuu za nchi wananchama wa ukanda wa 
maziwa makuu ambazo ni Amani, Utulivu na Usalama hususani katika eneo la
 mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Sanjari
 na hilo, nchi nyingi zimeusifu uongozi wa Rais wa DRC, Felix Tshisekedi
 kuwa tangu alipoingia madarakani amejitahidhi kuhakikisha kuwa kuna 
kuwa na amnai ndani ya DRC pamoja na majirani zake. Pia Uganda, Rwanda 
pamoja na Angola zimesifiwa kufanikisha kusaini makubalianao ya kuleta 
amanai kati ya Uganda na Rwanda.
Akiongea
 awali wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje Mgeni 
rasmi ambae alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kongo, Bwn. Clement 
Mouamba alisema kuwa mkutano wa leo, umelenga kuisaidia nchi ya DRC 
katika changamoto inazopitia hasa katika ukanda wa mashariki.
“Nawapongeza
 sana kwa kazi ambayo mmekuwa mkiifanya kwa kushirikiana na wadau 
mbalimbali katika kuhakikisha kuwa ugonjwa wa ebola unatokomezwa, kwani 
naamini kuwa umoja wetu tunaweza,” alisema Mouamba.
Aliongeza
 kwa kuzitaka nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu kuendelea kulinda
 amanai na umoja walionao ili kuweza kuendelea na shughuli mbalimbali za
 maendeleo kwani bila amani ni vigumu sana kwa umoja huo kuendelea.
Kwa 
upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianao wa Jamhuri ya Kongo, 
ambae pia alikuwa mwenyekiti wa mkutano huo Mhe. Jean Claude Gakosso 
aliwasisitiza mawaziri wa nchi wanachama kuwa amani na umoja katika 
ukanda huo ni nguzo muhimu sana na hivyo waendelee kuishika amani hiyo.
Pia 
aligusia ugonjwa wa ebola na kuwataka nchi wanachama kutokata tama ya 
kupambana na ugonjwa huo licha ya changamoto zinazojitokeza. 
“Juhudi
 mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali ya DRC hadi sasa kwa 
kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) pamoja na wadau wengine 
katika kupambana na ugonjwa huo ni kutoa chanjo ya kinga ya ugonjwa huo 
na elimu kwa wananchi wa maeneo yaliyoathirika na ugionjwa huo” alisema 
Waziri Gakosso.
Mkutano
 wa leo ulitanguliwa na mikutano miwili ambayo ilianza tarehe 11 hadi 14
 Oktoba 2019, jijini Brazzaville ambapo pamoja na mambo mengine 
ilijadiliwa suala la ugonjwa wa ebola na hali ya amani katika maeneo 
yenye mlipuko wa ugonjwa huo.
Nchi 
wanachama wa ukanda wa maziwa makuu ni pamoja na Angola, Burundi, 
Jamhuri ya Kati, Demokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kongo, Kenya, Rwanda, 
Sudan, Sudani Kusini, Tanzania, Uganda na Zambia.
Mwezi 
Augusti, 2019 Umoja wa Maendeleo ya Nchi za Ukanda wa Kusini mwa Africa 
(SADC) ulifanyika Tanzania Jijini Dar es Salaam nchi wananchama 
waliridhia na kuipitisha kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne ya Umoja huo 
baada ya Kiingereza, Kireno na Kifaransa.

 
No comments:
Post a Comment