Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masula ya Sera, Bunge, 
Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akihutubia 
vijana wakati wa mdahalo wa miaka 20 ya kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwl. 
Julius Kambarage Nyerere uliofanyika kwenye ukumbi wa Sea View, Mkoani 
Lindi.

Baadhi
 ya Vijana wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu 
anayeshughulikia masula ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye 
Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa mdahalo wa miaka
 20 ya kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere 
uliofanyika Mkoani Lindi.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akizungumza wakati wa mdahalo huo.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akizungumza wakati wa mdahalo huo.
Sehemu
 ya viongozi wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa 
mdahalo wa miaka 20 ya kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage 
Nyerere uliofanyika kwenye ukumbi wa Sea View, Mkoani Lindi. Katikati ni
 Katibu Mkuu, Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally.

Mama Gertrude Mongela akiwasilisha mada kuhusu Miaka 20 bila Baba wa Taifa wakati wa mdahalo huo uliofanyika Mkoani Lindi.

Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masula ya Sera, Bunge, 
Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akifuatilia 
mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Mama Gertrude Mongela kuhusu Miaka 20 
bila Baba wa Taifa wakati wa mdahalo huo. (Wa pili kutoka kushoto) ni 
Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Ali Abeid 
Karume na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) 
Mhe. Anthony Mavunde. Kulia ni Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis 
Mutungi.

Baadhi
 ya washiriki kwenye mdahalo huo wakifuatailia mada zilizokuwa 
zinawasilishwa. Kulia ni Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania 
(TBC) Dkt. Ayub Rioba. (Wa pili kutoka Kushoto ni Mjukuu wa Mwalimu 
Julius Kambarage Nyerere
Mjukuu
 wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Bi. Ngusekera Nyerere akitoa salamu
 wakati wa mdahalo huo wa  kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa 
Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere uliofanyika Mkoani Lindi.
Mjukuu
 wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Bi. Ngusekera Nyerere akitoa salamu
 wakati wa mdahalo huo wa  kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa 
Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere uliofanyika Mkoani Lindi.
Wawasilishaji
 Mada wakisikiliza hoja zilizokuwa zikichangiwa na baadhi ya washiriki 
wakati wa mdahalo huo wa kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa
 Mwl. Julius Kambarage Nyerere uliofanyika kwenye ukumbi wa Sea View, 
Mkoani Lindi.

Kijana mmoja wapo aliyeshiriki mdahalo huo akichangia mada kuhusu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)
Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, 
Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewataka 
vijana nchini kuenzi na kuziishi fikra na mitazamo za Baba wa Taifa, 
Mwl. Julius Kambarage Nyerere kwa kuendeleza umoja uliopo nchini.
Akizungumza
 wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kumbukizi ya Miaka 20 ya Kifo cha 
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lililofanyika Mkoani 
Lindi Oktoba 13, 2019, Waziri Mhagama alisema kuwa vijana wanapaswa 
kuendeleza mambo mema yote aliyoyafanya Baba wa Taifa enzi za uhai wake 
ili waendelee kujivunia juu ya misingi ya amani na umoja iliyopo nchini.
“Vijana
 mna kila sababu ya kujivunia amani na umoja ulipo katika taifa letu kwa
 kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi aliyewapenda watu wote bila 
kujali imani zao wala itikadi zao, alikuwa mzalendo na alitaka 
watanzania wote waishi kwa umoja,” alisema Mhagama.
Aidha 
alifafanua kuwa, Amani na umoja zilikuwa ni miongoni mwa tunu na falsafa
 kuu za Baba wa Taifa ambayo ndiyo matokeo ya umoja na mshikamano wa 
taifa uliopo sasa.
Aliongeza
 kuwa miongoni mwa mambo muhimu ambayo Baba wa Taifa alikuwa akisisitiza
 katika kuwaunganisha watanzania ni pamoja na kulijengea uhuru taifa na 
watu watu wake, kudumisha amani, upendo, umoja, uzalendo, mshikamano na 
 kuandaa sera za kukabiliana na ujinga, umaskini na maradhi.
Pamoja
 na hayo alisisitiza pia vijana na wananchi kumuunga mkono Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa 
kazi kubwa anayoifanya kuendeleza maono ya Baba wa Taifa ikiwemo mageuzi
 ya kiuchumi yenye manufaa kwa taifa.
Akitolea
 mfano sekta ya elimu ambayo serikali ya awamu ya tano imekuwa ikitoa 
elimu bure ilikuwa ni falsafa ya Mwalimu katika kuwajenga watanzania 
fikra ya kujitegemea ili waweze kuukabili umasikini.
Waziri
 Mhagama alitumia fursa hiyo pia kuwahimiza wananchi kuendeleza maudhui 
ya Mwenge wa uhuru ambao umesaidia kwa kiasi kikubwa kuwaunganisha 
watanzania na kuwahamasisha kufanya kazi kwa bidii ili wajiletee 
maendeleo.
Kwa 
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi alisema kuwa 
Mwalimu Julius Nyerere ataendelea kukumbukwa na Watanzania kwa mchango 
wake aliojitolea katika kulijenga taifa.

No comments:
Post a Comment