Matokeo chanyA+ online




Tuesday, March 3, 2020

ZIARA YA DPP SINGIDA YAWAWEKA HURU WASHTAKIWA 99

 Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Biswalo Mganga, Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk Rehema Nchimbi (katikati, na wajumbe wa Jukwaa la Haki Jinai mkoa wa Singida, muda mfupi baada ya mkuu wa mkoa kulizindua rasmi.

Idadi ya waliofutiwa Mashtaka na Ofisi ya Mashtaka ya Taifa kwa makosa mbalimbali kwenye magereza ya wilaya za Manyoni na Iramba mkoani hapa sasa imefikia 99.
Watuhumiwa 85 walioachiwa kwenye gereza la Manyoni ni wale wenye makosa yanayohusiana na kesi za uhujumu uchumi, udanganyifu na rushwa, huku 14 wa gereza la Iramba Kiomboi ni wale wa makosa mchanganyiko.

Akiwa kwenye ziara ya kutembelea wadau wa ‘Haki Jinai’, mkoani hapa, hivi karibuni, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Biswalo Mganga, alisema baada ya kutembelea magereza husika, kuangalia mwenendo mzima wa upelelezi na wapelelezaji, na kupata fursa ya kusikiliza mahabusu mbalimbali na kujiridhisha ndipo alipoamua kufuta kesi hizo.
“Nimefuta kwa wale ambao nimejiridhisha kwamba kesi zao hazina sababu ya kukaa gerezani, na hawa wengine wa uhujumi uchumi ni ambao waliingia kwenye hifadhi ya Rungwa wakiwa na mitambo na kuchimba madini, baada ya kukiri mbele yangu kwamba ni kweli wamefanya hayo makosa na ukiangalia gereza limejaa nikaona na wenyewe niwapatie nafasi ya mwisho,” alisema Mganga.
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, Biswalo Mganga (kushoto) akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk Rehema Nchimbi na Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt. Angelina Lutambi muda mfupi baada ya hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Haki Jinai ngazi ya Mkoa.
Na Godwin Myovela, Singida

Alisema, lengo hasa la ziara yake kwa wadau ilikuwa ni kufanya ukaguzi wa kesi zinazohusiana na rushwa na udanganyifu, kukagua kama kesi hizo zinaendeshwa na kupepelezwa ipasavyo, na kama kuna tija na matokeo tarajiwa, lakini pia kama kuna changamoto.


No comments:

Post a Comment