Matokeo chanyA+ online




Monday, August 10, 2020

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA KUU LA WANAWAKLE TANZANIA (UWT)

 



Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza hilo uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jijini Dodoma leo Agostui 10,2020. 

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimtunuku Tuzo Maalum Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kwa kutambua mchango wake na kuwawakilisha Wanawake Vizuri katika majukumu yake, wakati  wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT uliofanyika leo Agosti 10,2020 katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jijini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema kuwa jukumu la kulainisha mitambo ya uchaguzi kwa upande wa Chama cha Mapinduzi imekabidhiwa kwa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) 

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akihutubia Baraza kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika ukumbi wa White House mjini Dodoma, amesema kuwa jukumu la kampeni ni jukumu zito.

"Jukumu hili ukilichambua kiundani ni jukumu zito sana kujitoa na kujitolea kwa sababu kazi tunayokwenda nayo kuanza ya kampeni si kazi nyepesi" Makamu wa Rais

Makamu Rais amesema kuwa inahitaji uadilifu na umakini mkubwa  kwani Chama Cha Mapinduzi ni kikubwa na kinahitaji ushindi mkubwa.

No comments:

Post a Comment