Kupitia kitengo maalum cha Anti-Drugs Unit (ADU), Jeshi la Polisi limekuwa likishirikiana na DCEA katika oparesheni za kitaifa ambazo zinajumuisha ukamataji wa watuhumiwa, uteketezaji wa dawa haramu na upelelezi wa kina katika kanda zote zilizoundwa na mamlaka hiyo. Wakuu wa upelelezi wa makosa ya jinai pia wamepewa maelekezo maalum ya kushirikiana kwa karibu na DCEA ili kuhakikisha mtandao wa usambazaji wa dawa hizo unavunjwa kwa ukamilifu.
Aidha, Jeshi la Polisi limekuwa mstari wa mbele kutoa elimu kwa jamii kwa kuonesha kwa uwazi sampuli za dawa hizo haramu ili wananchi wazitambue, waweze kutoa taarifa, na kuchukua tahadhari mapema. Dawa hizo ni pamoja na heroin, cocaine, bangi, mirungi, methamphetamine, nk
Ushirikiano huu madhubuti unalenga kujenga jamii inayotambua hatari za dawa za kulevya na kujiwekea kinga dhidi ya janga hili, huku serikali ikidhamiria kuacha historia mpya isiyo na nafasi kwa biashara na matumizi ya dawa hizo hatari.
Kauli mbiu: "Wekeza kwenye Kinga na Tiba dhidi ya dawa za kulevya"
No comments:
Post a Comment