Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya
 Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza  na  Balozi  wa  Kuwait 
nchini, Mubarak Mohamed Alsehaijan (kulia),  juu  ya  kubadilishana 
 uzoefu katika Udhibiti  wa  Mipaka. Mazungumzo hayo yamefanyika leo, 
Ofisi Ndogo ya wizara, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Balozi wa Kuwait nchini, Mubarak 
Mohamed Alsehaijan, akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Mhandisi Hamad Masauni   juu ya kubadilishana  uzoefu  katika 
 Udhibiti wa Mipaka.Mazungumzo hayo yamefanyika leo, Ofisi  Ndogo  ya 
 wizara, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Balozi wa Kuwait Nchini, Mubarak 
Mohamed Alsehaijan  akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili Ofisi 
Ndogo ya Wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi, jijini Dar es Salaam. Kushoto
 ni  Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya
 Nchi,  Mhandisi  Hamad  Masauni, akiagana na Balozi wa Kuwait nchini, 
Mubarak Mohamed Alsehaijan (kulia), baada ya kumaliza mazungumzo 
yaliyohusu kubadilishana uzoefu katika Udhibiti wa Mipaka.Mazungumzo 
 hayo  yamefanyika leo, Ofisi  Ndogo ya wizara, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Serikali ya Tanzania na Nchi ya 
Kuwait ziko katika mpango maalumu wa kubadilishana uzoefu juu ya 
udhibiti wa mipaka ikiwa ni juhudi za Tanzania kuimarisha ulinzi katika 
mikoa yote nchini iliyopo mipakani
Hayo yamebainishwa na Naibu 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa 
mazungumzo na Balozi wa Kuwait Nchini, Mubarak Mohamed Alsehaijan ikiwa 
ni mpango wa nchi hizo kubadilishana uzoefu katika kudhibiti uhalifu 
katika mikoa ya mipakani
“Kama Serikali tuna vipaumbele 
katika kudhibiti  mipaka yetu kutokana na uhalifu unaotokea ikiwemo 
wahamiaji haramu,usafirishaji wa binadamu, uingiaji wa 
silaha,utoroshwaji wa madini na biashara yamagendo, ndio maana 
tumekutana leo kujadili ushirikiano wa nchi hizi mbili katika kudhibiti 
uhalifu huo”alisema Masauni
Akizungumza katika kikao hicho 
Balozi wa Kuwait Nchini, Mubarak Mohamed Alsehaijan alisema Tanzania ni 
nchi salama na wameamua kubadilishana uzoefu katika usimamiaji na 
udhibiti  wa mipaka.
“Tuna uhusiano mzuri baina ya 
Kuwait na Tanzania,tumekubaliana kubadilisha uzoefu ili kuweza 
kuimarisha sekta ya ulinzi kwa kutumia teknolojia itakayorahisisha 
udhibiti wa mipaka hapa nchini Tanzania” alisema Balozi Mubarak
Katika mazungumzo hayo pia 
walijadili juu ya teknolojia ya udhibiti wa majanga ikiwemo moto na 
ajali ambapo pia ni eneo ambalo nchi hizo mbili zilishaanza kushirikiana
 katika shughuli za uokozi.
No comments:
Post a Comment