Waziri
 wa Maliasili na Utalii,  Dkt. Hamisi Kigwangala amewataka Watanzania 
kuondokana na dhana iliyojengeka miongoni mwao kuwa watumishi wa Wizara 
hiyo hususan  wahifadhi wa  wanyamapori na Misitu  ni watu katili  
wanaowatesa Wananchi.
Kauli
 hiyo ameitoa leo wakati akifungua mkutano wa 26 wa Baraza la 
Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika katika Chuo cha Taaluma ya 
Wanyamapori Pasiansi jijini Mwanza.
Amesema
 watumishi hao ni watu wenye utu na weledi wa hali ya juu na 
wanaozingatia  sheria katika kutimiza majukumu yao na hulazimika kutumia
 nguvu wakati wakipambana na majangili wanaokutwa katika maeneo ya 
hifadhi wakifanya vitendo vya ujangili.
‘’
 Ulinzi wa Rasilimali za nchi ni jukumu letu sote, wizara imepewa 
dhamana ya kusimamia na kuongoza kwa niaba ya watanzania, kama kuna 
watumishi wa Wizara hii wanaowanyanyasa wananchi naomba walete ushahidi 
kwetu ili tuwachukulie hatua’’ amesema Dkt. Kigwangala.
Waziri
 Kigwangala amesikitishwa na idadi ya watumishi walipoteza maisha kwa 
ajali na wengine kuuwawa na majangili wakati wakipambana nao katika 
maeneo yote ya hifadhi  nchini na kutoa wito kwa wananchi wote wenye 
taarifa au ushahidi juu ya vitendo vyovyote vya kihalifu kuziwasilisha 
katika mamlaka zinazohusika.
Amesema
 kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua wale wote wanaojihusisha na 
vitendo vya ujangili na uhalifu katika maeneo ya hifadhi na wale wote 
wanaoshirikiana na makundi ya watu wenye nia ovu ya kukwamisha juhudi za
 uhifadhi wa rasilimali za Taifa.
Ametoa
 wito kwa wananchi kuheshimu sheria za uhifadhi na kuepuka kuvamia 
maeneo ya hifadhi kwa shughuli za kijamii na ufugaji akitoa wito kwa 
viongozi mbalimbali wa Siasa kuunga mkono juhudi za wizara za ulinzi wa 
maeneo ya hifadhi kwa kuwaelimisha wananchi wanaowaongoza kujiepusha na 
vitendo vya uvamizi wa maeneo ya hifadhi badala ya kuwatetea.
Kwa
 upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof.Adolf 
Mkenda akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho amesema kuwa jumla 
ya watumishi 23 walifariki dunia  wakati wakitekeleza majukumu ya 
uhifadhi   na   5 walijeruhiwa na majangili wakiwa kazini.
Prof.
 Mkenda amesema kuwa waliofanya vitendo hivyo  hawaitakii mema Tanzania 
na ni maadui wa shughuli za uhifadhi nchini akiongeza kuwa Serikali 
itaendelea kusimama na kuwatetea watumishi na askari wa wanyamapori 
wanaotimiza majukumu yao kwa kuzingatia sheria.
 Katibu
 Mkuu wa  Maliasili na Utalii Prof, Adolf Mkenda akizungumza na 
watumishi wa Wizara hiyo (hawapo Pichani) wakati wa ufunguzi wa baraza 
la 26 la Wafanyakazi wa Wizara hiyo liliofanyika  leo Jijini Mwanza.
 Waziri
 wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala akisisitiza jambo  wakati
 akizungumza na Watumishi wa Wizara hiyo kuhusu umuhimu wa kutekeleza 
maagizo kwa wakati yanayotolewa na Viongozi wa Wizara hiyo katika kikao 
cha Baraza la 26 la  Wafanyakazi wa Wizara hiyo  kilichofanyika leo 
Jijini Mwanza.
 Naibu
 Waziri wa  Maliasili na Utalii Mhe,Constantine Kanyasu akizungumza na 
Watumishj wa Wizara  hiyo katika kikao cha Baraza la 26 la  Wafanyakazi 
kilichofanyika leo Jijini Mwanza.
 Waziri
 wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla, Naibu Waziri  wa 
Wizara, Mhe, Constantine Kanyasu wakiwa wameshikana na watumishi 
wengine  hukuwakiimba wimbo wa mshikamano Daima katika Kikao cha Baraza 
la 26 la Wafanyakazi kilichofanyika leo jijini Mwanza.
 Waziri
 wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa ameambatana na 
Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Constantine Kanyasu wakati akikagua 
gwaride la Jeshi Usu katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Pasiansi.
Wafanya
 kazi wa  Maliasili na Utalii wakiimba wimbo wa mshikamano Daima katika 
Kikao cha Baraza la 26 la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo 
jijini Mwanza.







No comments:
Post a Comment