Waziri
 wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba 
Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa
 Rwanda, Dkt. Richard Sezibera. Katika mazungumzo yao,Sezibera 
alimpongeza  Prof. Kabudi kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na 
Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt.
 Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Ernest Mangu na
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na 
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo. Sezibera yupo 
nchini kwa ajili ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Rwanda,  Paul Kagame. 
Balozi
 wa Rwanda nchini Tanzania,  Eugene Kayihura (kulia) na Afisa Ubalozi wa
 Rwanda wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Kabudi na  Dkt. Sezibera 
(hawapo pichani). 
 Waziri
 wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba 
Kabudi akimwelezea jambo Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Dkt. Richard 
Seziberawakati wa mazungumzo hayo. 
 
Kutoka
 kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa 
Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini 
Rwanda,  Ernest Mangu pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Bw. 
Wilbroad Kayombo wakiwa kwenye Mazungumzo. 
Waziri
 wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Prof. Palamagamba 
Kabudi (katikati) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda,  Dkt. 
Richard Sezibera (wapili kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja 
na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika 
Mashariki,  Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda,
 Ernest Mangu (wa kwanza kulia) na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, 
Eugene Kayihura (wa kwanza kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo 
yao. 
No comments:
Post a Comment