Matokeo chanyA+ online




Tuesday, March 17, 2020

KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA YATEMBELEA MRADI WA RELI YA KISASA NA MRADI WA KUFUA UMEME KINYEREZI

Muonekano wa mradi wa reli ya kisasa (SGR) katika eneo la Pugu jijini Dar es Salaam
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu akiongozana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Sadiq Murad wakati wa ziara ya kukagua mradi wa reli ya kisasa (SGR) eneo la Pugu jijini Dar es Salaam  kukagua uzingatiaji wa sheria ya mazingira ambapo alisema aliupongeza mradi huo na ksuema kuwa umekidhi vigezo vyote vya mazingira walivyopewa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu akizungumza wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ilipotembelea mradi wa kufua umeme wa Kinyerezi jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Sadiq Murad akizungumza wakati Kamati anayoingoza ilipokutana na uongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua mradi wa reli ya kisasa (SGR) eneo la Pugu jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa akitoa maelezo kuhusu mradi wa reli ya kisasa (SGR) katika eneo la Pugu jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira

Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani akitoa maelezo kuhusu mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi wa Kinyerezi I extension ambapo alisema Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kila mwaka hutenga sh. milioni 50 kwa ajili ya shughuli za mzingira huku akiongeza kuwa wizara hiyo inawapa ushirikiano wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).
PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

1 comment: