Matokeo chanyA+ online




Wednesday, March 25, 2020

MTANDAO WA BARABARA ZA MIKOA KWA KIWANGO CHA LAMI UMEFIKIA KILOMETA 1,808

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema kuwa  ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami unaendelea  zikiwemo barabara kuu, barabara za mikoa na wilaya ambapo hadi Desemba 2019 mtandao wa barabara kuu umefikia km 8,67.



Amesema hayo jijini Dodoma na kuongeza  kuwa  mtandao wa barabara za mikoa umefikia kilometa 1,808 ambapo  barabara ya njia nane kutoka Kimara hadi Kibaha ya kilometa  19 ujenzi wake umefikia asilimia 63 ameongeza kuwa  ujenzi wa Ubungo Interchange ujenzi wake  umefikia asilimia 65.

Akizungumzia ujenzi wa madaraja amesema kuwa Serikali imeanza maandalizi ya ujenzi wa daraja la Kigongo – Busisi  Mkoani Mwanza lenye urefu wa mita 3,200 na upana wa mita 28.45 ambapo malipo ya awali ya shilingi bilioni 61.4 yamefanyika.

Waziri Mpango amesema kuwa ujenzi wa daraja jipya la Selander unaendelea na umefikia asilimia 25, ambapo  ujenzi wa madaraja  ya Mfugale na Mlalakuwa Dar es Salaam, daraja la Magufuli katika mto Kilombero mkoani  Morogoro ambapo madaraja menginge ni daraja la  Momba mkoani Rukwa, daraja la Sibiti mkoani Singida, Mara mkoani Mara, daraja la Ruhuhu Ruvuma, ambapo madaraja mengine ni daraja la  Msingi mkoani Singida, daraja la Lukuledi mkoani Lindi na daraja la Kavuu mkoani Katavi.
 
Aidha, amesema kuwa ujenzi unaendelea wa madaraja ya Mangara mkoani Manyara ujenzi wake umefikia asilimia 94, New Wami mkoani Pwani asilimia 35, na Kitengule mkoani kagera Kagera ambalo ujenzi wake umefikia  asilimia 42.

Aidha, Waziri Mpango amesema kuwa  jumla ya shilingi trilioni 3.60 zimetolewa katika kipindi cha Novemba 2015 hadi Januari 2020 kugharamia miradi ya barabara  na madaraja ikijumuisha shilingi bilioni 703.6 zilizotolewa katika kipindi cha Julai 2019 hadi Januari 2020.


No comments:

Post a Comment