 |
Waziri wa Nishati Dkt
Medard Kalemani (katikati), akimwagiza Mkandarasi kutoka Kampuni ya Namis
Corporate Ltd), anayetekeleza mradi wa Umeme wa Peri-Urban katika Mtaa wa
Bombambili, wilayani Ilala, mkoani Dar es Salaam, kuhakikisha anawaunganishia
umeme wananchi wote waliolipia ifikapo mwisho wa mwezi huu (Machi, 2020). Alitoa
maagizo hayo Machi 12 mwaka huu, akiwa katika ziara ya kazi. |
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ameonesha
kukerwa na tabia ya wakandarasi wanaorundika nguzo za umeme katika maeneo
mbalimbali kwa muda mrefu pasipo kuzisimika ili kuwaunganishia umeme wananchi.
Hali hiyo ilidhihirika Machi 12 mwaka huu
aliposhuhudia rundo la nguzo zikiwa chini katika mtaa wa Viwege, Kata ya
Majohe, wilayani Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam, akiwa katika ziara ya kazi.
Kufuatia hali hiyo, Dkt Kalemani alimwagiza Mkandarasi
anayetekeleza mradi wa umeme pembezoni mwa miji (Peri-Urban) katika eneo hilo
(kampuni ya Namis Corporate Ltd) kuziondoa nguzo hizo mara moja na kuzisimika
kisha kuwaunganishia umeme wananchi husika.
 |
Waziri wa Nishati Dkt
Medard Kalemani (mwenye miwani-kulia), akimwagiza Mkandarasi kutoka Kampuni ya
Namis Corporate Ltd), anayetekeleza mradi wa Umeme wa Peri-Urban katika Mtaa wa
Viwege, Kata ya Majohe, wilayani Ilala, mkoani Dar es Salaam, kuziondoa nguzo
zilizorundikwa chini na kuzisimika mara moja kisha awaunganishie wananchi
husika umeme. Alitoa maagizo hayo Machi 12 mwaka huu akiwa katika ziara ya
kazi.
“Asipotekeleza agizo langu kufikia kesho asubuhi,
nawaomba Diwani na Mwenyekiti wa Mtaa mnipigie simu na kunijulisha ili
nimchukulie hatua mara moja,” alisisitiza Waziri.
Aidha, alisema agizo hilo liwafikie wakandarasi wote
wanaotekeleza miradi mbalimbali ya umeme nchini kote kwamba hawatakiwi
kurundika nguzo chini pasipo sababu ya msingi, wakati wananchi wakiendelea
kulalamika kutounganishiwa huduma hiyo kwa wakati.
Sambamba na agizo hilo, Waziri pia alimwagiza
Mkandarasi huyo kuhakikisha anawaunganishia umeme wananchi wote waliolipia
huduma hiyo katika maeneo anakotekeleza mradi yakihusisha Kivule Bombambili,
Viwege, Majohe na Dondwe kabla ya mwisho wa mwezi huu wa Machi, 2020 vinginevyo
hatua kali za kimkataba zitachukuliwa dhidi yake.
| |
 |
Mafundi wakifunga
Mashine Umba (Transfoma) katika eneo la Dondwe, wilayani Mkuranga, Mkoa wa Pwani,
wakati Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani na Ujumbe wake, walipotembelea
eneo hilo kujionea maendeleo ya kazi husika, Machi 12 mwaka huu. |
“Nawaahidi mimi mwenyewe nitarudi hapa ifikapo mwisho
wa mwezi ili kujiridhisha endapo maagizo yangu yametekelezwa. Ikitokea
nikashindwa kuja mimi, nitamtuma mwakilishi aje kukagua na kuniletea mrejesho.”
Akiwa katika ziara hiyo ya siku moja, Waziri alikataa
kuwasha umeme katika Mtaa wa Bombambili kutokana na idadi ndogo ya wateja
waliounganishwa na kueleza kuwa atarudi kufanya kazi hiyo baada ya mkandarasi
kutekeleza maagizo yake ya kuwaunganishia umeme wateja wote watakaokuwa
wamelipia ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.
 |
Waziri wa Nishati Dkt
Medard Kalemani (mwenye miwani-mbele), akikagua utekelezaji wa Mradi wa Umeme
wa Peri-Urban katika Mtaa wa Bombambili, wilayani Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam,
akiwa katika ziara ya kazi, Machi 12 mwaka huu. |
Veronica Simba – Dar es Salaam
Kufuatia utekelezaji duni wa mradi husika katika maeneo
hayo, Waziri aliagiza Fundi Mchundo kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),
anayesimamia mradi huo katika maeneo husika, kuondolewa katika nafasi hiyo na
ateuliwe mwingine mara moja.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Diwani wa Kata ya
Tengerea, Shabani Manda, alimshukuru Waziri kwa kufanya ziara hiyo pamoja na
maagizo aliyoyatoa akisema anaamini wananchi wa maeneo hayo watanufaika na
huduma hiyo ya umeme kwa kuanzisha biashara mbalimbali zitakazowasaidia
kuwainua kiuchumi.
Katika ziara hiyo, Waziri alifuatana na viongozi na
wataalamu mbalimbali kutoka wizarani, TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini
(REA), akiwemo Kamishna Msaidizi wa Umeme, Mhandisi Innocent Luoga.
No comments:
Post a Comment