NA MWAMVUA MWINYI,CHALINZE
Mbunge
wa Jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete amekabidhi mabati 1,000 kwa
halmashauri ya Chalinze ,pamoja na tanki za maji na mabeseni Tisa vyote
vikiwa na gharama ya milioni 13.9.
Kati
ya mabati hayo 600 yataelekezwa katika miradi ya halmashauri ya sekta
ya elimu na afya na 400 yatapangiwa kazi na matakwa ya mfuko wa jimbo.
Akizungumzia
kuhusu msaada huo ,Ridhiwani alieleza kuwa , shule ya sekondari
Changarikwa inapatiwa mabati 90,Msata 90,Chamakweza mabati 90,nyumba ya
mwalimu sekondari ya Lugoba mabati 30 na shule ya msingi Magome mabati
60, Msolwa 60,Kidogozero mabati 90 na Ruvu Darajani.
Alisema,matanki ya maji yanakwenda katika vituo vya afya,zahanati ili kujikinga na janga la ugonjwa wa corona.
Ridhiwani
alieleza ,kwasasa jamii inapaswa kujihadhali na ugonjwa huo hivyo
akaona umuhimu wa kutafuta mdau Shubash Patel ambae alitoa matanki tisa
aina ya Kiboko pamoja na mabati kwa ajili ya kuezeka miradi ya afya na
elimu jimboni hapo .
"Kuna
maeneo ya mkusanyiko mahitaji bado ni makubwa ya ndoo za maji kwaajili
ya wananchi kunawa maji ,kama pale mnada wa Bwilingu ,nilitembelea wiki
iliyopita mahitaji ni makubwa " alisema Ridhiwani.
Kutokana
na hilo pia amempata mdau mwingine ambae atamsaidia kuleta ndoo 30 kwa
ajili ya kulinda na corona pamoja na makopo ya rangi na gymsum:;anasema
Ridhiwani.
No comments:
Post a Comment