Matokeo chanyA+ online




Sunday, June 29, 2025

MKEMIA MKUU WA SERIKALI NDIYE SHAHIDI MKUU WA KITAALAMU KATIKA KESI ZINAZOHUSISHA DAWA ZA KULEVYA

Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) imeendelea kuwa mhimili mkuu katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini kwa kutoa ushahidi wa kitaalamu wa kisayansi unaotumika mahakamani kuhakikisha haki inatendeka. Kupitia maabara zake za kisasa, GCLA hupokea na kuchunguza sampuli zote za dawa za kulevya zinazokamatwa katika oparesheni mbalimbali zinazoendeshwa na DCEA ikishirikiana na Jeshi la Polisi, Uhamiaji na taasisi nyingine za usalama.

Mkemia Mkuu wa Serikali ndiye shahidi mkuu wa kitaalamu katika kesi nyingi zinazohusisha dawa za kulevya, ambapo hutumia ripoti za maabara kuthibitisha aina na kiwango cha kemikali zilizokamatwa, jambo ambalo huongeza uzito na uhalali wa ushahidi mbele ya vyombo vya sheria na mahakama. Ushahidi huu umesaidia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza idadi ya mashauri yaliyomalizika kwa mafanikio dhidi ya wahalifu wa dawa za kulevya.

Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji mkubwa alioufanya katika miundombinu, mitambo ya kisasa, vifaa vya maabara na rasilimali watu, hali ambayo imeongeza kasi na ufanisi wa uchunguzi wa sampuli za ushahidi.

Kauli mbiu: "Wekeza kwenye Kinga na Tiba dhidi ya dawa za kulevya"

#DCEA
#OktobaTunatiki

No comments:

Post a Comment