Matokeo chanyA+ online




Thursday, April 14, 2022

KINANA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CHINA HAPA NCHINI, JIJINI DAR ES SALAAM


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana wakifurahi katika mazungumzo na Balozi  wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe.Chen Mingjian, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Aprili 14 2022.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana akimsindikiza Balozi  wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe.Chen Mingjian, wakati akiondoka katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, baada ya mazungumzo yao, leo. Kushoto ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana wakifurahi katika mazungumzo na Balozi  wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe.Chen Mingjian, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Aprili 14 2022.
Picha ya Pamoja ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana pamoja na Balozi  wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe.Chen Mingjian, alipowasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Aprili 14 2022.
 

BALOZI KATANGA AKUTANA NA WAZIRI WA NCHI WA U.A.E

 

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Hussein Katanga katika picha ya pamoja na Waziri wa nchi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E) Mhe. Sheikh Shakhboot Nahyan Al Nahyan na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam



Waziri wa nchi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E) Mhe. Sheikh Shakhboot Nahyan Al Nahyan, akieleza jambo wakati wa mazungumzo baina yake na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Hussein Katanga, Ikulu Jijini Dar es Salaam

*************************

Na Mwandishi Wetu, Dar

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Hussein Katanga amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa nchi Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E) Mhe. Sheikh Shakhboot Nahyan Al Nahyan, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Balozi Katanga amekutana na ugeni huo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Sulluhu Hassan. Viongozi hao pamoja na mambo mengine, wamejadili masuala mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E) katika nyanja za biashara na uwekezaji pamoja na Ulinzi na Usalama.

Balozi Katanga amemhakikishia Waziri huyo kuwa Tanzania inayo mazingira mazuri ya biashara na salama kuwekeza.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Mhe. Sheikh Shakhboot Nahyan Al Nahyan ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano ambao imekuwa ikiutoka kwa Umoja huo wakati wote.

Waziri wa Nchi wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Mhe. Sheikh Shakhboot Nahyan Al Nahyan amewasili nchini leo kuja kushiriki Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu kati ya Tanzania na Umoja wa Falme za Kiarabu.

RAIS SAMIA AWASILI WASHINGTON MAREKANI

 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Viongozi, Watumishi  wa Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania pamoja na Baadhi ya Wawakilishi kutoka nchi za SADC  waliofika kumpokea alipowasili Jijini Washington Nchini Marekani kwa ajili ya kuanza ziara ya Kikazi  tarehe 13 April 2022

KITETO WANUFAIKA NA MILIONI 80 ZA MAJOSHO




Jamii ya wafugaji wa Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara, wanatarajia kunufaika na majosho matano ya kuogeshea mifugo yao baada ya Serikali kuwapatia sh80 milioni za kuwajengea majosho hayo.

Mbunge wa jimbo la Kiteto, Wakili msomi Edward Kisau Ole Lekaita amesema majosho hayo yatajengwa katika vijiji vya Makame, Mwitikira, Loolera, Katikati na Ngabolo.

"Lengo ni kwa ajili ya kuboresha afya za mifugo na tumepatiwa sh80 milioni fedha hizo kutokana na ziara ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega aliyoifanya mwanzoni mwa mwaka huu mifugo ilipokufa kwa ukame," amesema.

Amesema fedha walizopata ni za ujenzi wa josho la kijiji cha Loolera kata ya Loolera sh16 milioni, josho la kijiji cha Mwitikira kata ya Kiperesa sh16 milioni na josho la kijiji cha Katikati kata ya Makame sh16 milioni.

Amesema ujenzi wa josho Kijiji cha Ngabolo kata ya Ndedo ni sh16 milioni na josho la kijiji cha Makame kata ya Makame sh16 milioni.

"Kwa niaba ya wananchi wa jimbo la Kiteto, tunamshukuru sana Rais mama yetu mpendwa Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote Serikalini kwa kugusa maisha yetu wana Kiteto," amesema Ole Lekaita.

Amesema majosho hayo yatasaidia kuboresha sekta ya mifugo kama ilivyoelekezwa kwenye ilani ya CCM 2020-2025 ya kujenga Majosho katika Vijiji vyenye mifugo kama ilivyoelezwa katika ukurasa wa 51 Ibara ya 40 (c) ( ix) ilani CCM ya mwaka 2020/2025.

Amesema ahadi yao kwa Rais Samia ni kuzisimamia Fedha zilizotengewa zionyeshe matokeo makubwa yenye ufanisi na tija kwa wananchi wa Kiteto.

Amesema fedha hizo zimeshalipwa kwa wazabuni na kazi za kujenga majosho zinatarajiwa kuanza wakati wowote hivi karibuni. 

MRADI WA MAJI WA BILIONI 69 UNATEKELEZWA MWANZA


Na Mohamed Saif

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel ameridhishwa na hatua za ujenzi wa mradi wa chanzo kipya cha maji katika eneo la Butimba wenye thamani ya shilingi bilioni 69 na utakaonufaisha zaidi ya wakazi 400,000.

Mhandisi Gabriel ameeleza hayo Aprili 12, 2022 wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi inayotekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu ikiwemo mradi huo wa chanzo hicho kipya cha majisafi cha Butimba.

“Nimeridhishwa na shughuli inayoendelea hapa; ikumbukwe kwamba huu ni mradi wa kimkakati ambao Serikali imewekeza fedha nyingi ili kutatua adha ya upungufu wa upatikanaji wa huduma ya majisafi kwa wakazi wa Jiji la Mwanza,” alisema Mhandisi Gabriel.

Alisema anatambua uwepo wa mgawo wa huduma ya maji kutokana na hali halisi ya mahitaji ambayo ni makubwa kuliko uzalishaji wa maji wa sasa wa MWAUWASA; hata hivyo alibainisha jitihada mbalimbali za Serikali ya awamu ya sita inayooongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha huduma ya majisafi inaimarika zaidi.

“Tunamshukuru sana Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa dhamira yake ya dhati ya kumtua mwanamke ndoo ya maji kichwani, fedha za miradi zipo na zinafika kwa wakati na miradi inaendelezwa kwa kasi,” alisema Mhandisi Gabriel.

Mhandisi Gabriel alisema wananchi wamekuwa na hofu ya muendelezo wa ujenzi wa miradi na hivyo kupitia ziara yake hiyo kwenye mradi wa chanzo kipya cha maji eneo la Butimba anawathibitishia hatua za kimapinduzi zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya sita.

“Niwasihi wananchi waendelee kuwa na subira kwa niliyoyashuhudia hapa ninasema yajayo yanafurahisha. Mkandarasi nimemkuta site, kazi zinaendelea na mradi ni mkubwa ninawapongeza sana Wizara ya Maji kupitia MWAUWASA; ninaiona Mwanza yenye majisafi ya kutosha ni suala la muda tu, kazi inaendelea,” alisema Mhandisi Gabriel.

Akizungumzia utekelezwaji wa mradi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi Leonard Msenyele alisema mradi unatekelezwa na Mkandarasi Kampuni ya SOGEA SATOM na VINCI GRAND PROJETS kutoka Ufaransa.

“Shughuli za usanifu na ujenzi zilianza rasmi Februari, 2021 na tunatarajia ifikapo Februari 2023 mradi utakuwa umekamilika,” alibainisha Mhandisi Msenyele.

Mhandisi Msenyele alisema mradi unahusisha ujenzi wa chanzo kipya na kituo cha tiba ya maji chenye uwezo wa kusafisha na kuzalisha majisafi kiasi cha lita milioni 48 kwa siku.

“Chanzo hiki kitakapokamilika kitaboresha huduma ya upatikanaji wa majisafi kwa wakazi zaidi 400,000 katika jiji la Mwanza na maeneo ya pembezoni kama vile Usagara, Kisesa, Buhongwa Mashariki, Lwanhima, Sahwa, Fumagila, Kishiri, Igoma na Buswelu,” alisema Mhandisi Msenyele.

Mhandisi Msenyele alisema mradi unatekelezwa kwa mfumo wa kusanifu na kujenga na kwamba hadi kufikia Machi 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 90 kwa kazi ya usanifu na asilimia 12 kwa shughuli ya ujenzi. 


Ujenzi wa Machujio ya Maji katika Mradi wa Maji Butimba
Hatua mbalimbali za ujenzi wa chanzo kipya cha maji zikiendelea
   Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel (wa pili kushoto) akiwasili kwenye eneo la ujenzi wa chanzo kipya cha maji cha Butimba. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi MWAUWASA, Mhandisi Leonard Msenyele

ANWANI ZA MAKAZI KUTUNZA HISTORIA YA NCHI, WATAKAOHARIBU MIUNDOMBINU KUSHUGHULIKIWA

 



Rai hiyo ameitoa jana tarehe 13 Aprili, 2022 wakati wa ziara yake katika mikoa ya Ruvuma, Mtwara na Lindi kukagua na kuhamasisha kasi ya utekelezaji wa mfumo wa Anwani za Makazi

Amesema kuwa, “Zoezi hili litumike kulinda historia ya nchi yetu, tusiache ikapotea tutumie majina ya viongozi mashuhuri pamoja na watu mashuhuri ili watoto wetu na vizazi vijavyo watakaokuja kutumia mfumo huu wakiuliza kwanini jina fulani basi wapatiwe historia ya jina husika “.

Ameongeza kuwa upo mwongozo mdogo wa uundaji wa majina ya barabara, mitaa na njia unaoruhusu wananchi kukubaliana na kuchagua jina la barabara na mtaa lakini sio vibaya katika baadhi ya maeneo wakitumia majina ya viongozi mashuhuri na watu mashuhuri ili kulinda historia ya nchi

Katika hatua nyingine, Waziri Nape amezielekeza sekretarieti za mikoa kuandaa mifumo madhubuti ya kulinda miundombinu ya Anwani za Makazi dhidi ya uharibifu unaoweza kufanywa na watu wasiothamini maendeleo ya nchi

“Tuweke mifumo ya kulinda miundombinu ya mfumo huu, kwasababu kuna watu wanaweza kuiharibu kwa makusudi kwa kuitoa na kwenda kuiuza chuma chakavu, hivyo tuandae mifumo madhubuti ya kuilinda na kuwashughulikia waharibifu wa miundombinu hii”, amesisitiza Waziri huyo

Aidha, Waziri Nape ameridhishwa na utekelezaji wa mfumo huo katika mikoa ya Ruvuma, Mtwara na Lindi ikiwa ni mikoa iliyopo katika kumi bora kwenye utekelezaji wa Operesheni hiyo kwa mujibu wa taarifa zinazopatikana katika mfumo wa kidijitali wa Anwani za Makazi

“Sio kwamba hatuziamini sekretarieti za mikoa katika kutekeleza operesheni hii, ukweli ni kuwa mnafanya kazi nzuri lakini Wizara ninayoisimamia ina wajibu wa kufika na kukagua namna utekelezaji wa operesheni hii unavyoendelea na vibao vinavyowekwa ili ifikapo mei 22 mwaka huu wa 2022 tuukabidhi mfumo ukiwa salama, kamili na tayari kutumika”, amesisitiza Waziri Nape

Naye Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema utekelezaji wa operesheni hiyo katika mkoa wake umefikia asilimia 97 na katika mkoa huo zoezi linakwenda vizuri na litakamilika kabla ya tarehe 30 Aprili mwaka huu

Kwa upande wa Brigedia Jenerali Marco Gaguti, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, amesema utambuzi umekwishakamilika kwa asilimia 100, zoezi lililobaki ni kuingiza taarifa kwenye mfumo wa kidijitali na kusimika nguzo za majina ya barabara na mitaa na kabla ya tarehe 30 mwezi huu wa Aprili zoezi litakuwa limekamilika

Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Clarence Ichwekeleza ametolea ufafanuzi kwa maeneo ambayo yamepimwa lakini bado hayajaendelezwa kuwa ni lazima yatapewa namba na taarifa zake zitaingizwa kwenye mfumo

“Msingi wa anwani yeyote ni kiwanja hata kama hakijajengwa taarifa zake ni lazima ziingizwe kwenye mfumo wa utambuzi wa kidijitali wa Anwani za Makazi ili hapo baadae patakapoendelezwa mfumo wa utaonesha nyumba hiyo au jengo hilo ni namba ngapi”, amesisitiza Mhandisi Ichwekeleza



Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akikagua kibao chenye anwani ya Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Mjini katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.




Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akiwa na Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma wakati wa ziara yake katika mkoa huo kukagua utekelezaji wa operesheni ya  Anwani za Makazi.

Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Clarence Ichwekeleza akizungumza na baadhi ya watendaji wa Mkoa wa Lindi (hawapo pichani), wakati wa ziara ya Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Nape Nnauye (kulia) katika mkoa hio kukagua utekelezaji wa operesheni ya Anwani za Makazi
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (kulia) akisimika nguzo yenye jina la barabara ya Uhuru katika mkoa wa Lindi.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (kulia) akibandika  jina la barabara ya Chikongola kwenye nguzo kabla ya kuisimika katika moja ya barabara za mkoa wa Mtwara.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (kulia) akisimika nguzo yenye jina la barabara ya Chikongola mkoani Mtwara. Kushoto ni Brigedia Jenerali Marco Gaguti, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akikagua kibao chenye anwani ya Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Mjini katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma. Aliyeambatana naye ni Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

BALOZI MBEGA AWATAKA WAFANYABIASHARA WA INDIA KUWEKEZA TANZANIA

Balozi wa Tanzania nchini India,  Anisa Mbega ametoa wito kwa wafanyabiashara wa nchi hiyo kuja kuwekeza Tanzania kwenye sekta mbalimbali za uwekezaji.       

Alitoa wito huo katika kongamano kubwa la biashara na uwekezaji (Tanzania India Trade Conference) lililofanyika katika jiji la Chennai, India tarehe 11 na 12 Aprili 2022.

Kongamano hilo lililoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Ubalozi wa Tanzania nchini India na Taasisi ya Uchumi na Biashara ya India (Indian Economic Trade Organization) lilitoa fursa kwa taasisi mbalimbali zinazohusika na masuala ya uwekezaji na biashara ikiwepo Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana nchini.

Balozi Mbega alisema licha ya India kuwekeza nchini mtaji wa kiasi cha Dola za Marekani Bilioni 3.7 na kuifanya nchi hiyo kuwa ya tano kwa uwekezaji, lakini bado nchi hiyo ina fursa kubwa ya kuongeza uwekezaji wake nchini.

Kongamano hilo lilihudhuriwa na wafanyabiashara na wawekezaji takribani 110 ambapo waliweza kufahamishwa fursa za biashara kwa bidhaa za mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi na fursa za uwekezaji katika sekta za Miundombinu, Madini, Ujenzi wa majumba, viwanda vya madawa, mitambo ya viwandani, nguo, Elimu na Afya.

Kutokana na kongamano hilo, tayari wawekezaji mbalimbali wa India wameonesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania ambapo kundi la kwanza la wawekezaji kwenye sekta ya ujenzi wa viwanda vya madawa ya binadamu na vifaa tiba kutoka India, linatarajiwa kutembelea Tanzania kuanzia tarehe 19 Aprili 2022 ili kukutana na wadau na kuanza taratibu za kuwekeza Tanzania.

Wafanyabiashara wengine walioshiriki Kongamano hilo wameonesha nia ya kushiriki maonesho ya 46 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam ambayo  yataanza tarehe 28 Juni hadi 13 Julai 2022. Ushiriki huo utawawezesha kukutana na wafanyabiashara na kuona bidhaa zinazozalishwa nchini Tanzania.

Kupitia kongamano hilo, wazalishaji wa bidhaa za Ngozi na korosho wa Tanzania wameunganishwa na wafanyabiashara wa India ambapo watapata fursa ya kuuza bidhaa hizo katika soko la India.

Sambamba na kongamano hilo, Ubalozi pia ulishiriki katika hafla ya uzinduzi wa ofisi ya uhamasishaji na uratibu wa biashara na uwekezaji inayojulikana kwa jina la INDIA TANZANIA TRADE COMMISSION (ITTC) iliyopo katika jengo laJJ Diamonds Mart No. 85, Barabara ya Gopathi Narayanas wani Chetty Chennai katika eneo la Thyagaraya Nagar ambalo ni kitovu cha biashara jijini Chennai. Ofisi hiyo itaongozwa na kusimamiwa na Dkt. J. Shrenik Naharkama Kamishna wabiashara wa ITTC.

Uwepo wa ITTC utasaidia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa haraka wa taarifa sahihi za biashara na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania, kwa kuwa ITTC itakuwa na mawasiliano ya moja kwa moja na taasisi zinazosimamia masuala ya biashara na uwekezaji za nchini Tanzania.

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe Anisa Mbega akifungua Kongamano la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na India Jijini Chennai, India.


Baadhi ya washiriki wa Kongamano la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na India wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa kongamano hilo.

Mada kuhusu fursa zilizopo nchini Tanzania

Picha ya pamoja
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe Anisa Mbega akiweka Saini kitabu cha wageni alipowasili katika hafla ya ufunguzi rasmi wa ofisi ya uratibu wa biashara na uwekezaji  ITTC
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega akikata utepe na kuwasha mshumaa kuashiria uzinduzi rasmi wa ofisi ya uratibu wabiashara na uwekezaji ITTC.

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe Anisa Mbega akiongoza kikao baada ya uzinduzi rasmi wa ofisi ya uratibu wa biashara na uwekezaji ITTC


Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe Anisa Mbega akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa masuala ya biashara na uwekezaji kutoka Tanzania na India katika hafla ya uzinduzi rasmi wa ofisi ya uratibu wabiashara na uwekezaji ITTC

Wednesday, April 13, 2022

KAMATI YA PAMOJA WATAALAM WA MIPAKA TANZANIA NA KENYA YAKAGUA MPAKA


Muonekano wa alama ya mwisho wa mpaka ardhini (BP MWISHONI) eneo la Kirongwe lililopo wilaya ya Rorya mkoani Mara na Muhuru Bay iliyopo Kaunti ya Migori upande wa Kenya.

 Na Munir Shemweta, WANMM SERENGETI

 

Timu ya Wataalamu wa Mipaka kati ya Tanzania na Kenya imetembelea na kujionea kazi ya uimarishaji mipaka wa Kimataifa wa nchi hizo iliyofanywa kwa lengo la kukagua na kushauri namna bora ya kuendelea na kazi zinazofuta.

 

Ukaguzi wa mipaka hiyo ulifanyika tarehe 12 April 2022 na ni sehemu ya kikao cha pamoja cha Wataalam wa Mipaka wa nchi hizo kilichoanza juzi kwa ajili ya kupokea  mawasilisho ya kazi iliyofanyika sambamba na kutoa muongozo wa namna bora ya kutekeleza kazi iliyobaki. 

Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Hamdouny Mansoor akionesha muelekeo wa mpaka kati ya Tanzania na Kenya eneo la Serengeti wakati timu ya wataalam wa mipaka kutoka Kenya na Tanzania ilipotembelea mpaka huo tarehe 12 April 2022. Wa pili kulia ni Mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya Balozi Joseph Vungo na katikati ni Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Mipaka ya Kimataifa nchini Kenya (KIBO) Juster Nkoroi.

 

Wataalam hao wakioongozwa na Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Hamdouny Mansoor pamoja na Juster Nkoroi Mtendaji Mkuu Ofisi ya Mipaka ya Kimataifa nchini Kenya (KIBO) walitembelea mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Kirongwe wilayani Rorya kwa upande wa Tanzania na Muhuru Bay katika Kaunti ya Migori nchini Kenya pamoja na ule mpaka wa nchi hizo eneo la Serengeti/Masai Mara ili kukagua kazi ya uwandani.

 

Timu ya wataalamu wa mipaka kutoka nchi za Tanzania na Kenya tayari imekamilisha uimarishaji mpaka wa kimataifa wa nchi hizo kipande cha Kilomita 83 kutoka hifadhi ya Serengeti/ Masai Mara hadi Ziwa Natron na awamu ya pili ya kipande cha kilomita 110 uimarishaji wake utaendelea baada ya kukamilika kuandaliwa mpango kazi.

 

Wakati wa ufunguzi wa kikao cha pamoja cha Wataalam wa Mipaka wan chi hizo mbili, Mkuu wa wilaya ya Tarime Kanali Michael Mangwela kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara aliwaambia washiriki kuwa, uimarishaji mipaka ulenge kuimarisha mahusiano pia pamoja na kujadili changamoto za maeneo ya mipakani.

 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya Balozi Joseph Vungo alishauri wataalamu wanaoshiriki kikao hicho kuhakikisha wanajadili na kuzitolea maamuzi changamoto kwa amani hasa wakizingatia nchi ya Tanzania na Kenya zimekuwa na mahusiano mazuri.

 

Mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la nchi kavu una ukubwa wa Kilomita 758 na uimarishaji wake utasaidia kuondoa changamoto mbalimbali zilizokuwa zikijotokeza kutoka kwa wananchi wanaofanya shughuli maeneo ya mipakani katika nchi hizo.

 



KINANA ATETA NA BALOZI WA ZIMBABWE NCHINI TANZANIA


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania Mheshimiwa Lt. Jen. (Mst) Anselem Sanyatwe, leo Aprili 13 ,2022 katika Ofisi Ndogo za CCM, Lumumba jijini Dar Es Salaam. 


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania  Mheshimiwa Lt. Jen. (Mst) Anselem Sanyatwe, (kushoto) leo Aprili 13 ,2022 katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar Es Salaam.



Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akimsindikiza  Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania  Mheshimiwa Lt. Jen. (Mst) Anselem Sanyatwe, (katikati) (wa kwanza kushoto) Ndg Ngemela Lubinga Katibu wa Idara ya Siasa Na Uhusiano wa Kimataifa CCM leo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar Es Salaam.


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akimuaga Balozi wa Marekani nchini Tanzania  Mheshimiwa Lt. Jen. (Mst) Anselem Sanyatwe, leo April 13 ,2022 katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar Es Salaam. (Picha zote na Fahad Siraji)
 

Monday, April 11, 2022

KINANA AKUTANA NA BALOZI WA MAREKANI

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania  Dk. Donald J. Wright leo katika Ofisi Ndogo za CCM, Lumumba jijini Dar Es Salaam. (Picha na Fahad Siraji)

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM-Bara), Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, amekutana na Balozi wa Marekani nchini, Donald Wright, jijini Dar es Salaam ambapo wamezungumza mambo mbalimbali ikiwemo kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na nchi ya Marekani.

Akizungumza muda mfupi baada ya balozi huyo kuondoka Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Aprili 11 2022,  Kanali Mstaafu Kinana alisema mazungumzo hayo yalikuwa ya kawaida katika kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na nchi hiyo.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Balozi wa Marekani nchini Tanzania  Dk. Donald J. Wright (kushoto) leo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar Es Salaam. (Picha na Fahad Siraji)

“Mazungumzo yetu yalikuwa ya kawaida, tumezungumzia namna ya kuimarisha uhusiano pamoja na ustawi wa wananchi,” alisema Kanali Kinana.

Alisema miongoni mwa maeneo waliyoyagusia katika mazungumzo yao ni pamoja na kuimarisha huduma za kijamii ikiwamo afya na utoaji haki kupitia mifumo mbalimbali.

Viongozi hao wamekutana zikiwa siku chache tangu balozi huyo alipokutana na Rais Samia Suluhu Hassan.