Matokeo chanyA+ online




Monday, December 30, 2019

TCAA WAZINDUA MFUMO WA KIDIGITALI WA KUSAIDIA KUTUA NDEGE KATIKA KIWANJA CHA NDEGE CHA MPANDA - KATAVI

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe na Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania,Mizengo Pinda kwa pamoja wakikata utepe kuasharia kuuzindua mfumo wa kidigitali utakaowezesha ndege kutua salama katika Kiwanja cha Ndege Mpanda, Mkoani Katavi. Afisa Muongoza Ndege Mwandamizi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania TCAA Sunday Walinda akimpatia Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe maelezo ya kitaalamu kuhusu mfumo wa kidigitali utakaowezesha ndege kutua salama katika Kiwanja cha Ndege Mpanda, Mkoani Katavi. Rubani wa Shirika la ndege la Tanzania Rubani Hamza akielezea namna mfumo huo ulivyorahisisha hatua za utuaji ndege katika uwanja wa ndege wa Mpanda, Katavi. Viongozi walioketi meza kuu wakipungia ndege ya Shirika la ndege la Tanzania kama ishara ya kuitakia safari njema ilipokuwa ikipaa kutoka uwanja wa ndege wa Mpanda, Katavi. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania, Hamza Johari akielezea mchakato mzima ukinzia na tafiti na hatimaye kubuniwa kwa mfumo huu wa kidigitali wa kuziwezesha ndege kutua salama katika uwanja wa ndege wa Mpanda, Katavi. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe, akielezea kufurahishwa na jitihada zilizofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kufanikisha mfumo huu kukamilika sambamba na kuipongeza mamlaka hiyo kwa kutumia wataalamu wazawa waliobuni mfumo huu katika Kiwanja cha Ndege Mpanda, Mkoani Katavi. Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh Juma Zuberi Homera ameipongeza TCAA kwa kubuni mfumo huu na kusisitiza kuwa wananchi wa Mpanda watumie fursa hii ya ujio wa ndege mara tatu kwa wiki kujiimarisha katika kuwekeza kwani milango ya biashara na wageni zaidi kufika mpanda kwa usafiri wa anga sasa imerahisishwa. Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Mh. Mizengo Pinda akiwachagiza wanaMpanda kuitumia fursa hii ya ujio wa ndege katika wilaya hiyo kujinufaisha kiuchumi.

Thursday, December 26, 2019

BRELA YAFANYA BONANZA LA MICHEZO KWA ZAIDI YA VIKUNDI 48 JIJINI DAR ES SALAAM

Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF Anna Makinda ambaye alikuwa mgeni rasmi katika bonanza la Brela akikagua timu ya mpira wa miguu iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF Anna Makinda (katikati) akiwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Loy Watson Mhando ( wa kwanza kushoto) wakifuatilia bonanza la michezo lililoandaliwa na BRELA jijini Dar es Salaam.

Katika kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) wamefanya bonanza la michezo kwa vikundi 48 vya mpira wa miguu likiwa na lengo wa kujenga afya na kuimarisha uhusiano baina ya wafanyabiashara.
Bonanza hilo lilofanyika pia lilikuwa na lengo la kuwaelezea umuhimu wa bima ya afya kwa dereva wa bodaboda na wananchi kwa ujumla.
Akizungumza Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Loy Watson Mhando amesema kuwa wamefurahishwa na jinsi watu walivyojitokeza kushiriki mazoezi na kupima afya zao jambo linalisaidia kupunguza wagonjwa.
Bonanza hilo lilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF Anna Makinda (katikati) ambaye alikuwa mgeni rasmi limefanikiwa kwa asilimi 100 kwa kuweza kufikisha malengo yake.

Sunday, December 22, 2019

WATANZANIA TUSHEREKEE SIKUKUU YA KRISMAS KWA AMANI NA UPENDO MKUBWA - RAIS MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsalimia mtoto Zioni nje ya kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita mara baada ya kushiriki Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote. Disemba 22, 2019.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amejumuika pamoja na waumini wengine wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita katika Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote.  Disemba 22, 2019.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 22 Desemba, 2019 ameungana na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Chato Mkoani Geita kusali Dominika ya 4 ya Majilio na ametumia nafasi hiyo kuwatakia heri ya Krismasi na Mwaka Mpya Watanzania wote.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amejumuika pamoja na waumini wengine wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita katika Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote.  Disemba 22, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amejumuika pamoja na waumini wengine wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita katika Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote.  Disemba 22, 2019.

Katika salamu hizo, Mhe. Rais Magufuli amesema tunapoelekea katika sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya Wakristo na Waumini wa madhehebu mengine mbalimbali wanalo jukumu la kuendelea kuombea amani, upendo na umoja kwa wanadamu wote bila kubaguana.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijiandaa kupokea Sakramenti Takatifu, alipoungana na waumini wengine wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita katika Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote. Disemba 22, 2019.

“Niwaombe ndugu zangu wa Chato na Watanzania kwa ujumla, tusherehekee sikukuu ya Krismasi kwa amani na upendo mkubwa, lakini pia tuukaribishe Mwaka Mpya kwa amani na upendo mkubwa wa Kristo, mwaka unaokuja uwe mwaka wa mafanikio, uwe mwaka wa maendeleo, uwe mwaka wa kujenga umoja wetu kwa Watanzania wote, uwe mwaka wa amani na upendo na uwe mwaka wa kuendeleza Taifa letu katika maendeleo ya kweli” amesema Mhe. Rais Magufuli.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijiandaa kupokea Sakramenti Takatifu, alipoungana na waumini wengine wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita katika Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote. Disemba 22, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waumini  wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita wakati wa  Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote . Disemba 22, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Padre Henry Mulinganisa Paroko wa kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita nje ya kanisa hilo mara baada ya kushiriki Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote. Disemba 22, 2019.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza Waumini wa Parokia ya Bikira Maria Chato kwa kazi kubwa ya upanuzi wa Kanisa wanayoendelea nayo ambayo naye alichangia upanuzi wake mwaka 2016.

Misa Takatifu hiyo imeongozwa na Paroko wa Parokia hiyo Padre Henry Mulinganisa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Padre Henry Mulinganisa Paroko wa kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita alipozungumza na Waumini wa Kanisa wakati wa Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko huyo, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote . Disemba 22, 2019.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waumini  wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita wakati wa  Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote . Disemba 22, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waumini  wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita wakati wa  Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote . Disemba 22, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Padre Henry Mulinganisa Paroko wa kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita nje ya kanisa hilo mara baada ya kushiriki Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote. Disemba 22, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono Waumini nje ya kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita mara baada ya kushiriki Misa Takatifu ya Dominika ya nne ya Majilio iliyoongozwa na Paroko wa kanisa hilo Padre Henry Mulinganisa, ambapo Mhe. Rais amewatakia heri ya Krismas na Mwaka mpya  Watanzania wote. Disemba 22, 2019.PICHA NA IKULU

Friday, December 20, 2019

TUME YA MADINI YATANGAZA ZABUNI UNUNUZI WA MAENEO YENYE LESENI HODHI ZA MADINI

Tume ya Madini  imetangaza zabuni kwa ajili ya ununuzi wa maeneo  10 yenye leseni hodhi za madini  na yenye ukubwa wa kilomita za mraba 381.89 yaliyopo katika maeneo ya Ngara – Kagera, Kahama- Shinyanga, Chunya- Mbeya, Bariadi na Busega – Simiyu, Morogoro, Nachingwea – Lindi ambayo awali leseni hodhi zake zilikuwa zimerudishwa Serikalini.
 
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dodoma kwenye mkutano wake wenye lengo la kutangaza zabuni kwa ajili ya ununuzi wa maeneo  10 yenye leseni hodhi za madini tarehe 19 Desemba, 2019
Uamuzi huo umetangazwa  tarehe 19 Desemba, 2019 na Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula kupitia mkutano wake na waandishi wa habari  uliofanyika  jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Kamishna wa Tume ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeki, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya pamoja na watendaji wengine wa Tume ya Madini.
Profesa Kilula alifafanua kuwa, awali mwaka 2017 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha marekebisho ya Sheria ya Madini Sura Namba 123 na kanuni zake ambapo  pamoja na mambo mengine, zilizokuwa leseni  hodhi za madini ( retention licence) zilirudishwa  Serikalini .
Alisema baada ya marekebisho hayo maeneo yote 10  yenye ukubwa wa kilomita za mraba 381.89 yalirudishwa Serikalini na kuongeza kuwa, wachimbaji wa madini wengi wamekuwa wakiulizia maeneo hayo mara kwa mara lengo likiwa ni kuomba leseni za uchimbaji madini.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa  Shukrani Manya (kushoto) akielezea vigezo vinavyohitajika kwenye zabuni za ununuzi wa maeneo yenye leseni hodhi za madini. Katikati ni Mwenyekiti wa Tume ya Madini Profesa Idris Kikula na kulia ni Kamishna wa Tume ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeki.
 Aliendelea kusema kuwa, baada ya uchambuzi wa kina kufanyika, Serikali kupitia  Tume ya Madini, maeneo yote 10 yaliyokuwa na leseni hodhi yatatolewa kwa zabuni na kukaribisha kampuni za uchimbaji wa madini na watu binafsi  wenye uwezo wa fedha na utaalam katika miradi ya uchimbaji wa madini  na wenye nia ya kuendeleza miradi ya madini ya nickel, dhahabu na rare earth elements kuomba zabuni hizo.
Aliongeza kuwa, mwekezaji atakayeonesha nia ya kuwekeza katika maeneo hayo atakuwa na jukumu  la kufanya kazi na kuwaendeleza wachimbaji wadogo wa madini.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa  Shukrani Manya (kushoto) akifafanua jambo katika mkutano huo.
Wakati huo huo, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya akielezea hatua zinazochukuliwa kwa wamiliki wa leseni  wasioendeleza maeneo yao, aliwataka wamiliki  na waombaji wote wa leseni  za utafutaji na uchimbaji wa madini  wenye mapungufu kurekebisha mapungufu  hayo ndani ya  siku 30 kuanzia sasa.
Alifafanua mapungufu hayo kuwa ni pamoja na leseni ambazo hazifanyiwi kazi, leseni ambazo hazijalipiwa ada ya pango la mwaka, maombi ambayo hayajalipiwa ada ya maombi na maombi yaliyokosa viambatisho muhimu kwa mujibu wa sheria.
Profesa Manya alitaja mapungufu mengine kuwa ni pamoja na waombaji waliokidhi vigezo vya kupewa leseni lakini hawajalipa ada ya maandalizi na wamiliki ambao leseni zao zimeshatolewa lakini hazijachukuliwa.
Alifafanua kuwa mpaka sasa leseni zaidi ya 134 za utafutaji na uchimbaji wa kati wa madini hazijachukuliwa na zaidi ya maombi 450 ya leseni za utafutaji yana mapungufu.
Akielezea hatua zitakazochukuliwa kwa kampuni au watu binafsi walioaminiwa na Serikali na kupewa leseni lakini wameshindwa kutekeleza masharti ya leseni kwa mujibu wa Sheria ya Madini,  alisema leseni ambazo hazijalipiwa ada ya pango kwa mwaka, leseni ambazo hazifanyiwi kazi na leseni ambazo zimekwishatolewa lakini hazijachukuliwa zitaandikiwa hati ya makosa na yasiporekebishwa zitafutwa kwa mujibu wa sheria.

Watendaji wa Tume ya Madini wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya (hawapo pichani).
Aidha alisema kuwa, maombi yote ya leseni za utafutaji na uchimbaji wa kati yenye mapungufu yataondolewa kwenye mfumo wa utoaji wa leseni ili waombaji wengine wenye sifa pamoja na wachimbaji wadogo waweze kuomba maeneo hayo.
Aliendelea kusema kuwa, maombi ambayo yamekidhi vigezo vya kupewa leseni lakini hayajalipiwa ada ya kuandalia leseni yataondolewa kwenye mfumo ili waombaji wengine wenye sifa waweze kuomba maeneo hayo.
Alisisitiza kuwa tangazo la zabuni husika linapatikana katika tovuti ya Wizara ya Madini ambayo ni (www.madini.go.tz)  Tume ya Madini (www.tumemadini.go.tz) magazeti ya Habari Leo na Daily News ya tarehe 20 Desemba, 2019 pamoja na blogs na mitandao ya kijamii.

KONGAMANO LA TATU LA SIKU MBILI LA KIMATAIFA LA KISWAHILI LAFUNGULIWA ZANZIBAR

Balozi Seif akiangalia baadhi ya Vitabu vya Kiswahili na kuridhika na kazi kubwa ilivyofanywa na Magwiji wa Lugha ya Kiswahili kutoka pembe mbali mbali za Dunia.
Mzee Mwinjuma Kirobo kutoka Kikundi cha Wajasiriamali cha Tulikotoka kutoka Bweleo akimpatia maelezo Balozi Seif jinsi Kikundi hicho kinavyoendelea na uratibu wa kuhifadhi vitu vya Aslimu vilivyokuwa vikitumiwa na Waswahili wa enzi zilizopita.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akilifungua Kongamano la Tatu la Siku Mbili la Kimataifa la Kiswahili kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein hapo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni.

Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa ZanzibarMabaraza, Taasisi pamoja na Wataalamu wanaoshughulikia Kiswahili wana wajibu wa kusimama kidete kuhakikisha kuwa Lugha ya Kiswahili inaendelezwa na kutumiwa katika usahihi wake kulingana na Utamaduni wa Waswahili kwa vile Lugha ni kipengele muhimu cha Utamaduni wa Jamii.
Washirika hao lazima waone fahari ya mafanikio ya Lugha ya Kiswahili kwamba sasa imekuwa sio Lugha ya Waswahili wazawa wachache peke yao bali imeshaenea kuwa Lugha ya Kimataifa yenye utambulisho wa kujivunia kama nembo ya Afrika.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein alitanabahisha hayo wakati akilifungua Kongamano la Tatu la Siku Mbili la Kimataifa la Kiswahili katika Hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni.
Alisema hiyo ni hatua muhimu ya kupanda hadhi kwa Lugha ya Kiswahili jambo ambalo halitotokea kwa sadfa, bali litatokana  na dhamira ya dhati ya Watu wenye mapenzi na Lugha hii adhimu na wanaoishughulikia.
Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar {BAKIZA} Dr. Muhammed Seif Khatib akitoa salamu za kuwakaribisha Waswahili kutoka pembe zote za Dunia waliohudhuria Kongamano la Tatu la Kimataifa la Kiswahili hapo Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil.  
Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Balozi Ali Aman Karume akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kulifungua Kongamano hilo la Siku mbili la Kiswahili. 
Balozi Seif  pamoja na Viongozi wengine wa Kitaifa na Baraza la Kiswahili wakiwaonyesha Washiriki wa Kongamano wa Tatu la Kimataifa la Kiswahili nakala ya Kitabu akichokizindua kilichotungwa na Gwiji wa Kiswahili wa uandishi wa Vitabu Duniani Mzee Haji Gora Haji na kupewa jina la Shuwari.


Alisema Lugha ya Kiswahili kama zilivyo Lugha nyengine Duniani ina Utamaduni wake uliopevuka na kuimarika pamoja kusheheni masuala mbali mbali ya Mila, Desturi na Silka za Waswahili mambo ambayo ni rasilmali kubwa inayohitajika kuenziwa.
Dr. Shein alisema kutokana na mahitaji makubwa ya Lugha ya Kiswahili kukidhi kama daraja la mawasiliano katika shughuli mbali mbali za Kitaifa na Kimataifa, Lugha hii sasa imekuwa ni bidhaa inayouzika katika soko la Kimataifa kwa vile tayari hutumika kupitishia maafira tofauti.
Alieleza kwamba Wataalamu na watumiaji wa Lugha ya Kiswahili wanayo nafasi ya kuzitumia njia za kisasa za Teknolojia ya Mawasiliano, ili kuchangamkia fursa zilizopo za soko la Lugha hiyo kwa upande wa Fasihi na Isimu katika Mataifa mbali mbali Duniani kwa lengo la kujiongezea kipato.
Alifahamisha kwamba hadhi ya Lugha ya Kiswahili hivi sasa ni bidhaa muhimu katika kukuza Maendeleo ya Kiuchumi na Kiutamaduni Ulimwenguni. Hivyo inachopaswa kuzingatiwa kwa sasa ni jinsi gani itakavyopangwa Mikakati ya kuzitumia fursa zinazotokana na Kiswahili.
Balozi Seif na viongozi wengine wa Serikali wakikagua Vitabu mbali mbali vilivyoandikwa kwa Lugha ya Kiswahili na Waandishi Mahiri waliobobea kwenye Maonyesho ya Kongamano la Kimataifa la Kiswahili. 
Na Othman Khamis/Rashida Abdi wa OMPR, ZNZ

Rais wa Zanzibar alieleza kwa lengo la kuzidi kupiga hatua za kuiendeleza Lugha ya Kiswahili na kuweza kuzitumia fursa tofauti zinazozidi kujitokeza za kunufaika na Lugha hii adhimu, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekiagiza Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar {SUZA} kifanye maandalizi ya kuanzisha Skuli ya Tafsiri na Ukalimali.
Alisema hatua hiyo itawezesha kuandaliwa mapema Wataalamu waliobobea  wa fani za tafsiri na ukalimali wanaohitajika kwa wingi katika maendeleo mbali mbali ya Mawasiliano ikiwemo katika Mikutano ya Kimataifa ambako Lugha ya Kiswahili tayari inatambulika hivi sasa.
Dr. Shein alielezea matumaini yake kwamba jambo hilo kwa Zanzibar ni stahiki yake na linawezekana kutokana na uzoefu uliopo wa kuwasomesha Wageni Lugha ya Kiswahili kwa kipindi kirefu katika iliyokuwa Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni Zanzibar {TAKILUKI}.
“ Serikali pamoja na kuongeza vifaa na vivutio vyengine maalum vya kuwafanya wageni imeshakiagiza Chuo Kikuu cha SUZA kuiimarisha Skuli hiyo ya Kiswahili na Lugha za Kigeni kuwa Kitivo Kikuu cha kuifanya Zanzibar kuwa Center of Exicellence wanaotaka kujifunza lugha washawishike kujiunga”. Alisisitiza Dr. Shein.
Alisema kama lilivyowezekana suala la kuanzisha Shahada ya Uzamivu na Uzamili za Kiswahili jambo hili litawezekana kwa vile Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iko tayari kukata pua, kuunga wajihi katika kulifanikisha suala hilo kama ilivyowahi kufanya katika kufanikisha masuala mengine yenye maslahi kwa Taifa.