Matokeo chanyA+ online




Wednesday, March 29, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akimpokea Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam tarehe 29 Machi 2023 kuanza ziara nchini Tanzania






 

Rais Mhe. Samia akutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Misaada ya Kibinadamu la Katoliki la Marekani (Catholic Relief Services) Bw. Sean Callahan Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Misaada ya Kibinadamu la Katoliki la Marekani (Catholic Relief Services)  Bw. Sean Callahan aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Misaada ya Kibinadamu la Katoliki la Marekani (Catholic Relief Services)   Bw. Sean Callahan pamoja na Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania TEC Padri Charles Kitima mara baada ya mazungumzo Ikulu Jijini Dar es Salaam

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Misaada ya Kibinadamu la Katoliki la Marekani (Catholic Relief Services)   Bw. Sean Callahan pamoja na ujumbe wake mara baada ya mazungumzo Ikulu Jijini Dar es Salaam

 


 

SUA KUJA NA MAPENDEKEZO YA SERA BORA ZA BIASHARA YA MAZAO YA KILIMO NA NYAMA PORI NCHINI

Kaimu Rasi wa Ndaki ya Uchumi Kilimo na stadi za Biashara Dkt. Zena Mpenda akifungua warsha ya Wadau wa Mradi wa TRADE HUB kujadili matokeo ya utafiti. 

Na Amina Hezron,Morogoro 

WADAU wa zao la Soya kahawa miwa na nyama pori wametakiwa kushiriki kikamilifu kwenye kutoa mapendekezo  na maoni yao kwenye Mradi wa Utafiti wa Biashara,Maendeleo na Mazingira (TRADE Hub) ili matokeo yatakayopatikana yaweze kuinua tija ya mazao hayo nchini.

Hayo yameelezwa na Kaimu Rasi wa Ndaki ya Uchumi Kilimo na stadi za Biashara Dkt. Zena Mpendu aliyemuwakilisha Rasi wa Ndaki hiyo Dkt Damas Philip katika  warsha iliyoandaliwa na mradi huo ili kuwasilisha matokeo ya awali ya utafiti wao kwa wadau ili kupata maoni yao  juu ya namna bora ya kufanya biashara ya haki na endelevu.

Amewataka wadau hao kuzingatia kuwa tasnia hizo zinagusa kwa namna moja ama nyingine maisha na maendeleo ya wadau mbalimbali pamoja na uchumi na maendeleo ya nchi kwa ujumla hivyo watumie fursa hiyo kwa makini kutoa maoni yao ya namna bora ya kuboresha biashara  katika tasnia hizo zote za Nyama pori na Mazao ya kilimo.

“Ni vizuri tunaposikiliza hizi mada zinazotolewa tuangalie inaelezea kweli ile hali halisi kwenye maeneo yetu ili tuweze kuboresha yale ambayo tumeyaona lakini pia tuweze sasa kuangalia mapendekezo yanayotoka tuone hayo mapendekezo yatafanyika yanawezekana ili tukitoka hapa tuwe na mapendekezo ambayo ni bora zaidi”, alisema Dkt. Zena.

Dkt. Zena ameeleza kuwa Serikali imekuwa ikiboresha mara kwa mara Sheria, taratibu na Kanuni kuhakikisha kwamba biashara hizo hazisababishi ongezeko la uharibifu wa mazingira na upotevu wa baionuai hivyo ni muhimu kama wadau wa biashara kuhakikisha wanaingia kwenye mikataba ya kijani kwenye biashaa zao ili kuwe na biashara endelevu kwaajili ya watu na ulimwengu pia.

Akieleza malengo ya warsha hiyo Mratibu wa Utafiti na Machapisho SUA Prof. Japhet Kashaigili amesema kuwa ni kuwasilisha kwa wadau matokeo ya tafiti kadhaa ambazo mradi huo umeyapata ili wapate nafasi ya kuyajua, kuyajadili na kutoa mapendekezo ili kuona ni namna gani yanaweza kuchangia kwenye maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

“Lengo lingine la pili la warsha yetu hii na mradi ni kutengeneza mpango au njia itakayotupeleka nchi mahali fulani kuptia ufanyaji wa biashara yenye haki na endelevu nchini Tanzania lakini pia bidhaa zetu ziweze kuhimili ushindani kwenye masoko ya kimataifa na kukuza uchumi”, alifafanua Prof. Kashaigili.

Aidha amesema dhumuni kubwa linalobeba mradi huo ni kuhakikisha biashara ya mazao na nyama pori inakuwa ni injini ya ukuaji wa uchumi jumuishi,Kuondoa umasikini na kama mbinu ya kutekeeleza maendeleo endelevu kama ilivyosisitizwa kwenye Mpango wa maendeleo endelevu bila kuchangia uharibifu wa mazingira.

Kwa upande wake Mkuu wa mradi huo Prof. Reuben Kadigi amesema warsha hiyo ya wadau ni muhimu sana katika kupata maoni na mapendekezo ambayo yatawasaidia watafiti kuweza kutengeneza andiko la sera ambalo litawasilishwa Serikalini ili kusaidia kufikia malengo yaliyokusudiwa.

“Kila mchango wa mdau unaotolewa andika mahali kila ushauri andika ili mwisho wa siku tupate kitu kizuri kifupi cha kuwasilisha serikalini baada ya kufanya uchambuzi wa kina kulingana na matokeo tuliyoyapata maana mwisho wa siku hatuwezi kupeleka kwa watunga sera kitu kinacholeweka nawaweze kukifanyia kazi kwa ustawi wa biashara nchini”, alieleza Prof. Kadigi.

Kwa upande wake Dkt. Charles Malaki aliyemuwakilisha Kaimu Rasi wa Ndaki hiyo amewashukuru wadau waliojitokeza katika warsha hiyo na amewataka kutoa maoni na mapendekezo ya kuboresha matokeo ya tafiti hizo ili kuisaidia Serikali baadae kupata sera bora zitakazosaidia kuwa na uendelevu katika biashara ambayo inajali Mazingira,Nyama pori pamoja na watu.

Mradi wa Utafiti wa Biashara,Maendelo na Mazingira (TRADE Hub)ni mradi wa miaka mitano unaotekelezwa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na washirika wengine kutoka katika nchi kumi na tano  za Afrika, Asia, Uingereza na Brazil kuanzia Februari 2019 hadi Machi 2024.

 Mratibu wa Utafiti na Machapisho (SUA) ambaye pia ni mtafiti kwenye mradi huo Prof. Japhet Kashaigili akieleza malengo ya Warsha hiyo na kazi ambazo mradi huo umefanya hadi sasa.
Mkuu wa mradi wa TRADE HUB, Prof. Reuben Kadigi akitoa neno la ukaribisho kwa Wadau hao kutoka nchi nzima kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua warsha hiyo.
 Dkt. Charles Malaki akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi na wadau.
 Picha ya pamoja ya washiriki wa warsha hiyo kutoka SUA na Mikoa mbalimbali ambao ni wadau wa Mazao ya Soya, Kahawa, Mpunga, Parachichi na wawakilishi wa Halmashauri na Makampuni yaliyo kwenye mnyororo wa thamani ya mazao hayo.
Wadau wa Mradi wa TRADE HUB wakifuatilia mawasilisho ya matokeo ya tafiti mbali mbali zilizofanywa kwenye mzao ya Soya, Kahawa,Parachichi,Miwa na Nyama Pori.
Mkutano ukiendelea.
Wadau wakiwa kwenye mkutano huo.
Wadau wa Mradi wa TRADE HUB wakifuatilia mawasilisho ya matokeo ya tafiti mbali mbali zilizofanywa kwenye mzao ya Soya, Kahawa,Parachichi,Miwa na Nyama Pori.
Wadau wa Mradi wa TRADE HUB wakifuatilia mawasilisho ya matokeo ya tafiti mbali mbali zilizofanywa kwenye mzao ya Soya, Kahawa,Parachichi,Miwa na Nyama Pori.
Mkutano ukiendelea.
 

Monday, March 13, 2023

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAFUNZO KWA WAKUU WA WILAYA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akisalimiana na viongozi mbalimbali wakati akiwasili katika Ukumbi wa Mikutano wa Jiji la Dodoma uliopo Mtumba kufungua Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Wilaya  tarehe 13 Machi 2023






Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akihutubia Wakuu wa Wilaya wanaoshiriki Mafunzo ya Uongozi wakati wa ufunguzi wa Mafunzo hayo yanayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jiji la Dodoma uliopo Mtumba  tarehe 13 Machi 2023.

 






Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akiwa na Waziri wa TAMISEMI Angellah Kairuki, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Jenista Mhagama,Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Daniel Chongolo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule katika picha ya pamoja na Wakuu wa Wilaya wanaoshiriki mafunzo ya uongozi mara baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo katika Ukumbi wa Mikutano wa Jiji la Dodoma uliopo Mtumba  tarehe 13 Machi 2023.

 

Saturday, March 11, 2023

Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amuapisha Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Dkt. Wilson Mahera Charles kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 11 Machi, 2023.

 

Tuesday, March 7, 2023

WANAWAKE TANESCO, SUWASA SINGIDA WAPANDA MITI KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Wanawake watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Singida wakionesha furaha yao kabla ya kwenda kupanda miti kwenye chanzo cha maji cha Mwankoko kilichopo nje kidogo ya Manispaa ya Singida ikiwa ni shamra shamra kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani, kesho Machi 08,2023. 

Na Dotto Mwaibale, Singida

 

WANAWAKE watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na wenzao wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Singida (SUWASA) katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Machi 08, 2023, wamepanda miti katika chanzo za maji cha Mwankoko kilichopo nje kidogo ya Manispaa ya Singida ikiwa ni moja ya kazi ya upandaji miti ili kuimarisha uoto wa asili utakaosaidia upatikanaji wa mvua na hivyo kuimarisha vyanzo vya maji kwa ajili ya kuzalisha umeme mwingi.

Mbali na upandaji miti wanawake hao wa TANESCO wametoa msaada wa unga, mafuta ya kula, sabuni na vitu vingine kwa watoto yatima wa Kituo cha Upendo Home for Street Children, ikiwa ni shamrashamra kuelekea maadhimisho ya siku hiyo ambayo duniani kote yatafanyika kesho.

Zoezi hilo la upandaji miti limefanyika leo Machi 7, 2023 kwa kuwashirikisha wakuu wa idara wa taasisi hizo mbili za Serikali mkoani hapa. 

Akizungumza katika zoezi hilo la upandaji miti Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa  Shirika hilo, Lulu Silungwe alisema TANESCO imekuwa ikitegemea mvua inayotokana na miti kwa ajili ya kusambaza huduma ya umeme hivyo zoezi hilo la upandaji wa miti litasaidia kukabiliana na athari za kimazingira na mvua kuwa nyingi. 

“Tumekutana hapa leo na wenzetu kutoka SUWASA kwa ajili ya kupanda miti chanzo cha maji Mwankoko chini ya kauli mbiyu yetu isemayo Panda Miti, Mvua Ndi, Umeme Ndindindi ikiwa ni moja ya kazi yetu kuelekea maadhimisho ya kilele cha Siku ya Wanawake Duniani ambayo ni kesho” alisema Silungwe. 

Alisema mbali ya kupanda miti pia watawatembelea watoto Yatima wanaolelewa Kituo cha Upendo Home for Street Children, kwa ajili ya kuwapatia zawadi mbalimbali ikiwa ni kazi yao nyingine kuelekea maadhimisho hayo. 

Neema Ntandu ambaye ni mfanyakazi wa shirika hilo alisema wamepanda miti 150 ya aina mbalimbali na kuwa watahakikisha inakuwa na kuimarisha chanzo hicho cha maji cha Mwankoko. 

Mwenyekiti wa Wanawake wa Shirika hilo Mkoa wa Singida, Asiatu Mnanura akizungumza wakati wa kutoa msaada kwa watoto wa kituo hicho alisema wamefurahi kuwatembelea ukizingatia kuwa wao ni wazazi hivyo waliona vizuri jambo hilo liwe ni sehemu ya moja ya kazi yao kuelekea maadhimisho hayo. 

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa SUWASA, Fatina Mbaga alisema ni wajibu kwa kila mwana Singida kupanda miti kwa wingi ili kuhifadhi mazingira jambo litakalosaidi kuhifadhi mazingira na kuwepo kwa mvua nyingi na hivyo kuwa na maji ya kutosha. 

Mratibu wa kituo hicho Afesso Ogenga alishukuru kwa msaada huo na kueleza kuwa kituo hicho kinawapokea watoto kutoka mitaani na majumbani lakini ni baada ya kufanyika utaratibu wa kuwatambua na kujua historia zao kwa kushirikiana na watu wa ustawi wa jamii.

Furaha ikiendelea kutamalaki kwa wanawake hao watumishi wa Tanesco Mkoa wa Singida.

Wanawake watumishi wa Tanesco Mkoa wa Singida wakifanya maandamano kuelekea katika zoezi hilo la kupanda miti.

 Mratibu wa Kituo cha  Home for Street Children, Afesso Ogenga akizungumza baada ya kukabidhiwa msaada huo.

Wanawake watumishi wa Suwasa Mkoa wa Singida wakipanda ngazi kuingia kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda kupanda miti.

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Suwasa, Fatina Mbaga, akizungumzia kuhusu zoezi hilo la upandaji miti.
Wanawake watumishi wa shirika hilo wakiwa wameshika miche ya miti tayari kwa kuipanda.
Kaimu Meneja wa Tanesco Mkoa wa Singida, Mhandisi , Ramadhan Mwanga akipanda mche wa mti eneo la chanzo cha maji Mwankoko.
Miche ya miti ikipandwa kwenye chanzo hicho cha maji.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Suwasa, Fatina Mbaga, akipanda mche wa mti.
Afisa Rasilimali Watu wa Tanesco Mkoa wa Singida, Angelina Kaarata (kulia) na Afisa wa shirika hilo, Neema Ndaskoy wakipanda mche wa mti katika eneo hilo., 
Yusra Nicholaus akipanda mche wa mti.
Salama Juma akipanda mche wa mti kwenye chanzo hicho cha maji.
Neema Ntandu ambaye ni mfanyakazi wa shirika hilo, akizungumzia umuhimu wa kupanda miti katika vyanzo vya maji.
Picha ya pamoja wakati wa kukabidhi msaada kwa watoto Yatima wa Kituo cha 
Zawadi kwa kituo hicho cha Yatima zikitolewa.