Matokeo chanyA+ online




Monday, October 30, 2017

MHESHIMIWA SAMIA SULUHU HASSAN, MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA HAFLA YA UZINDUZI WA SERA YA TAIFA YA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA YA MWAKA 2016 NA MKAKATI WA UTEKELEZAJI WA SERA HIYO TAREHE 23 OKTOBA, 2017 DODOMA


Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan  amezindua Sera ya Taifa ya huduma ndogo za fedha ya mwaka 2017 pamoja na mkakati wa utekelezaji wa mwaka 2017/2018 hadi 2027/2028 huku akizitaka taasisi za fedha nchini kuangalia kwa kina suala la riba linalokuwepo kwenye mikopo kwa kuwa limekuwa likiwaumiza wananchi wa hali ya chini.


RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE.DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AWASILI JIJINI MWANZA NA KUFUNGUA DARAJA LA JUU LA WATEMBEA KWA MIGUU LILILOPO FURAHISHA JIJINI MWANZA,OKTOBA 30,2017.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Bw.John Mongela Mkuu wa mkoa wa Mwanza mara baada ya kuwasili katika Uwanaja wa Ndege wa Mwanza uliopo Jijini Mwanza oktoba 30,2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Viongozi wa Mkoa wa Mwanza mara baada ya kuwasili Jijini Mwanza oktoba 30,2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Mwanza katika ufunguzi wa daraja la watembea kwa miguu lililopo eneo la Furahisha Jijini Mwanza oktoba 30,2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaMhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja na viongozi mbalimbali akivuta utepe kwenye jiwe la ufunguzi kuashiria ufunguzi wa wa Daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha liliopo jijini Mwanza Oktoba 30,2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mikono wananchi wa Mwanza mara baada ya kufungua daraja la watembea kwa miguu lililopo eneo la Furahisha Jijini Mwanza oktoba 30,2017.
Wanachi waliojitokeza kumshangilia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa kufungua daraja la watembea kwa miguu lililopo eneo la Furahisha Jijini Mwanza oktoba 30,2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma ya mchelemchele ya Jijini Mwanza mara baada ya kufungua daraja la watembea kwa miguu lililopo eneo la Furahisha Jijini Mwanza oktoba 30,2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimsalimu mtoto mwanafunzi mara baada ya kufungua daraja la watembea kwa miguu lililopo eneo la Furahisha Jijini Mwanza oktoba 30,2017.
PICHA NA IKULU

Thursday, October 26, 2017

NDEGE ILIYOBEBA WATALII YAANGUKA SERENGETI

Ndege ya Kampuni ya Coastal Aviation  iliyobeba watalii 10 imeanguka na kujeruhi watalii wawili na rubani ilipokuwa ikitua katika uwanja wa Lobo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

 Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, William Mwakilema amesema ajali hiyo imetokea jana Jumatano Oktoba 25,2017 saa tisa alasiri ilipokuwa ikitua.

Amesema taarifa za awali zinasema chanzo cha ajali hiyo ni mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha iliyosababisha uwanja kujaa maji.
Mwakilema amesema wakati rubani akitua ndipo ndege ilianguka na kusababisha watalii hao wawili kujeruhiwa.

“Waliojeruhiwa ni wawili na rubani ambao walipelekwa jijini Arusha na baadaye Nairobi kwa matibabu. Wengine walikuwa na maumivu kidogo ambao walipatiwa huduma na daktari wetu na baadaye wakasafirishwa kwenda Arusha,” amesema.
  
Amesema wanashukuru katika tukio hilo ndege haikuungua na kwamba, ilipokuwa ikiserereka iligonga mti na kusimama.

Mhifadhi huyo amesema mbele kulikuwa na mawe, hivyo ingeyagonga na kulipuka ingesababisha madhara makubwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Mohamed Jafari hajapatikana ili kuzungumzia tukio hilo.

Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu amesema wanaendelea kulifuatilia na kwamba, wanasubiri taarifa kutoka kwa vyombo vya uchunguzi.

UZALENDO NI KUJITOLEA KWA KILA HALI KULIFIA TAIFA LAKO