Matokeo chanyA+ online




Tuesday, February 28, 2023

BALOZI SHELUKINDO ASISITIZA UMUHIMU WA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akipokea maua mara baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023. Balozi Shelukindo aliapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuushika wadhifa huo tarehe 27 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Fatma Rajab wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Alex Mfungo wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Naimi Aziz wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Caesar Waitara wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkaguzi Mkuu wa Ndani, Bw. Japhary Kachenje wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. Haji Janabi wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bi. Talha Waziri wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Samwel Shelukindo ajitambulishe kwa menejimenti ya Wizara wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo (kushoto) akiongoza kikao cha Menejimenti kilichofanyika kwa lengo la kujitambulisha katika ofisi za Wizara jijini Dododma tarehe 28 Februari 2023. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Fatma Rajab. 

Mkurugenzi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Alex Mfungo na Mkurugenzi Idara ya Sera na Mipango, Bw. Haji Janabi wakifatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Mkurugenzi Idara ya Afrika, Balozi Naimi Aziz akijitambulisha kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo katika hafla ya mapokezi yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.


Mkurugenzi wa Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Caesar Waitara (kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Noel Kaganda wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Kutoka kulia ni Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Swalehe Chondoma na Bw. Haji Janabi wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.


Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati, Bw. Leonce Bilauri na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji wakifuatilia kikao cha utambulisho cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrka Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo.

Sehemu nyingine ya wajumbe wa managementi wakifuatilia kikao.

Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama, Bw. Amani Mwatonoka na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Salma Baraka wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dododma tarehe 28 Februari 2023.

Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Dkt. Isaac Kalumu  na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bi. Talha Waziri wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dododma tarehe 28 Februari 2023.

Mwakilishi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Ally Kondo (Kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Biashara za Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi, Bw., Francis Berege wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akiwasili katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo (kulia) akisalimiana na sehemu ya madereva walioshiriki hafla ya mapokezi katika ofisi za Wizara jiji Dodoma tarehe 28 Februari 2023

Picha ya Pamoja






CHANGAMOTO BANDARI YA MALINDI INASABABISHWA NA KUWA NA GATI MOJA DOGO ...

Saturday, February 25, 2023

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Dk. Condoleezza Rice na mfanyabiashara Bill Gates wameungana na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. George W. Bush katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Ijumaa Februari 24, 2023



Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. George W. Bush na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Dk. Condoleezza Rice wakiwa kwenye mjadala katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023




Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa 66 wa Mambo ya Nje wa Marekani Dk. Condoleezza Rice katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) katika ukumbi jijini Washington DC Februari 24, 2023


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mfanyabiashara Bill Gates katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. George W. Bush katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) wa Marekani Bi Alice Albright katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023


Sherehe hiyo, iliyoandaliwa na Taasisi ya George W. Bush inafanyika  katika Taasisi ya Amani ya Marekani. Watatu hao watashiriki katika mjadala  maalumu utaoendeshwa na Dkt. Rice kuhusu kuanzishwa kwa PEPFAR, mafanikio yake  makubwa, na jinsi programu hiyo inavyofanikiwa katika  nchi washirika na kwa sera ya kigeni za Marekani.


Kwa Mujibu  wa taarifa kutoka Taasisi ya George W. Bush, katika maadhimisho hayo, Mke wa Rais Mstaafu wa Marekani George W. Bush, Bi. Laura Bush, atatoa maelezo mafupi na kuwatambulisha Tatu Msangi na Faith Mang'ehe, Mabalozi wa Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation kutoka Tanzania waliohudhuria wakati wa kutolewa hotuba ya Hali ya Muungano  (State of the Union) katika Congress ya Marekani, kuhusu mpango huo wa PFEPFAR mwaka 2008. 

 

Katika kuadhimisha miaka hiyo 20 ya mafanikio ya PEPFAR, licha ya kwamba Mpango huo unatekelezwa katika nchi mbalimbali Afrika na Asia, Taasisi ya George Bush Foundation wameamua kumualika Dkt. Kikwete kwa kutambua mchango wake mkubwa katika kuufanya Mpango huo kuwa na mafanikio.


Kwa mujibu wa Taasisi ya George W. Bush Foundation, Tanzania imekua ni nchi ya kupigiwa mfano kwa namna ilivyofanya jitihada za kupambana na ugonjwa wa UKIMWI kwa juhudi zake yenyewe kama nchi na kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kimataifa kama vile PEPFAR.


Taasisi hiyo inasema kwamba tangu mwaka 2003, PEPFAR imesaidia Tanzania kupunguza vifo vinavyotokana na UKIMWI kwa karibu 80% na maambukizi mapya kwa karibu 60%. Mpango huo ulipoanza, chini ya Watanzania 1,000 walikuwa wakipata matibabu ya VVU. Hivi sasa, zaidi ya Watanzania milioni 1.5 wanapokea matibabu haya ya kuokoa maisha.


Tangu Rais George W. Bush alipozindua PEPFAR mwaka 2003, serikali ya Marekani imewekeza zaidi ya dola bilioni 100 katika mapambano yake ya kimataifa dhidi ya VVU/UKIMWI, zikiwemo karibu dola bilioni 7 kwa Tanzania, ukiwa ni mchango  mkubwa kuwahi kutolewa na taifa lolote kupambana na ugonjwa mmoja katika historia ya binadamu.


 

Friday, February 24, 2023

SEKTA BINAFSI YA TZ KATIKA SHEREHE ZA UFUNGUZI WA JUKWAA LA EUTZBIASHARA LILILOONGOZWA NA MH DKT PHILIP MPANGO, MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA.








Mbele ya Mh Dkt Philip Mpango, Makamu wa Rais wa #Tanzania, mikataba mitatu yenye thamani ya Euro milioni 353 ilisainiwa kati ya Taasisi za Tanzania na Umoja wa Ulaya.


 

Wednesday, February 22, 2023

MAKAMU WA RAIS AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UMOJA WA ULAYA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akifanya Mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki Manfredo Fanti, Mazungumzo yaliofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam leo tarehe 22 Februari 2023. Kesho tarehe 23 Februari 2023 Makamu wa Rais anatarajia kuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano la Uwekezaji kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya litakalofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania na Jumuiya Afrika Mashariki Manfredo Fanti mara baada ya mazungumzo yao yaliofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam leo tarehe 22 Februari 2023. Kesho tarehe 23 Februari 2023 Makamu wa Rais anatarajia kuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano la Uwekezaji kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya litakalofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.

 



 




Tuesday, February 21, 2023

Bola Tinubu,mgombea wa urais nchini Nigeria kupitia chama tawala cha APC, alifanya kampeni yake ya mwisho katika ngome yake mjini Lagos hapo jana Jumanne na kuahidi mabadiliko iwapo ataibuka mshindi wakati wa uchaguzi wa Jumamosi.

 








Tinubu, ni miongoni mwa wagombea 18 wanaotaka kumrithi rais Muhammadu Buhari anayeondoka madarakani, lakini anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa mgombea mkuu wa upinzani Atiku Abubakar kutoka chama cha PDP na Peter Obi kutoka chama cha Leba.