Matokeo chanyA+ online




Wednesday, September 30, 2020

VIJIJI 73 KATI YA 77 VYA WILAYA YA MISENYI VYAPATIWA UMEME

Vijiji 77 kati ya vijiji 73 vya wilaya ya Missenyi mkoani Kagera vimepelekewa huduma ya umeme na vijiji 4 bado havina umeme.

Hayo yamesemwa jana (Jumanne, Septemba 29, 2020) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Kassambya, katika mikutano uliofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa, wilayani Missenyi, mkoani Kagera.



Amevitaja vijiji ambavyo havina umeme na vipo kwenye mpango wa kupelekewa umeme kuwa ni vijiji vya Buchurago, Katano, Kakunyu na Bugango.

Akizungmzia sekta ya mifugo ambayo imetajwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 hadi 2025 kuanzia ukurasa 47-52, Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeisimamia vizuri sekta ya mifugo ili kuhakikisha wafugaji wanapata manufaa.
“Shilingi milioni 23 zimetumika kukarabati machinjio ya Bunazi hapa Misenyi, pia tumerahisisha uuzaji wa mazao ya mifugo kwa kufuta tozo kero 114 katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi na kuimarisha masoko ya mazao ya mifugo kwa kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo,” alisema.

Alisema Serikali imepanga kuanzisha vituo vya kisasa vya uchunguzi wa magonjwa ya mifugo katika mikoa 18 ambayo haina vituo, kuimarisha huduma za tiba za mifugo kwa kuhakikisha kila wilaya ina maabara, kliniki na daktari wa mifugo.

Mheshimiwa Majaliwa ambaye yuko mkoani Kagera kumuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli alitumia fursa hiyo kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Nkenge, Dkt. Florent Kyombo na wagombea udiwani 13 wa CCM wa kata za wilaya hiyo. Mgombea udiwani wa kata ya Kassambya, Bw. Yusuph Jumbe na wenzake sita, wamepita bila kupingwa.

Kuhusu barabara, Mheshimiwa Majaliwa alisema sh. bilioni 3.57 zilitolewa kupitia Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara za wilaya hiyo zikiwemo barabara za Bukwali-Kashenye-Bushango, Ngorogoro-Kyabugombe, Mabuye –Itara na Ruzinga - Mugongo.

Alizitaja barabara nyingine kuwa ni za Gera – Ishozi – Ishunju, Nyankele – Kilimilire, Mabale–Mwemage-Kyaka, Nyankele-Nyamilembe–Kenyana na Kituntu–Bwengabo. Alisema mwaka 2020/2021, sh. milioni 711.6 zimetolewa kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara kwa muda maalum.

MGOMBEA MWENZA WA KITI CHA URAIS KWA TIKETI YA CCM SAMIA SULUHU HASSAN, AZUNGUMZA NA WANANCHI WA HAYDOM MKOANI MANYARA

Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia mkutano wa kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM  katika Uwanja wa Haydom Mkoani Manyara leo Septemba 30,2020

 


Umati wa Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wananchi wa Haydom Mkoani Manyara wakimsikiliza Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,  alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM katika Uwanja wa Haydom Mkoani Manyara leo Septemba 30,2020.


Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana Viongozi Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wananchi wa Haydom Mbulu Vijijini Mkoani Manyara alipowasili katika uwanja wa Haydom kwa ajili ya kuhutubia mkutano wa kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM  leo Septemba 30,2020.





Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wananchi wa kijiji cha Labai na Dinamu Wilaya Hanang alipokuwa njiani akielekea Wilaya ya Hanang kwa ajili ya kuhutubia mkutano wa  kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM leo Septemba 30,2020.

MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM, RAIS DKT. JOHN MAGUFULI AHUTUBIA WANANCHI WA MBEYA MJINI



 

Sehemu ya Wananchi wa Mbeya wakiwa wamefurika katika viwanja vya Airport mjini Mbeya kumsikiliza Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia leo 30 Septemba 2020




Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Maelfu ya Wananchi wa Mbeya mjini katika Mkutano wa Kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM uliofanyika leo tarehe 30 Septemba 2020 katika uwanja wa Airport mkoani Mbeya

 



Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Maelfu ya Wananchi wa Mbeya mjini katika Mkutano wa Kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM uliofanyika leo tarehe 30 Septemba 2020 katika uwanja wa Airport mkoani Mbeya

MAJALIWA: SERIKALI YATEKELEZA MIRADI 1,423 YA MAJI

  • Kayanga ni miongoni mwa mji 28 iliyonufaika na sh. tril. 1.2 za miradi hiyo

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kassim Majaliwa amesema Serikali imetekeleza miradi ya maji 1,423 ikiwemo mradi wa kupeleka maji kwenye miji 28 unaotekelezwa kwa sh. trilioni 1.2.

 

“Kayanga imepata sh. bilioni 58, ni miongoni mwa miji 28 iliyopata fedha za mradi wa maji kitaifa ambao unajumuisha mikoa mingi,” amesema.

 

Ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Septemba 29, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Kayanga, katika mikutano uliofanyika kwenye uwanja wa Changarawe, wilayani Karagwe, mkoani Kagera.

Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Kata ya Kayanga, wilayani Karagwe, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa akipiga magoti ya kuwaomba wananchi wa jimbo la Karagwe kupigia kura wagombea wote wa Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba 28, 2020, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika  uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwakabidhi nakala ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020-2025 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa (kushoto) na Mgombea Udiwani Kata ya Kayanga, Germanus Byabusha (katikati), katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Kayanga, wilayani Karagwe, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

 

 

Mikoa inayohusika na mradi huo miji yake kwenye mabano ni Tanga (Handeni/Korogwe, Muheza na Pangani); Njombe (Njombe, Wanging’ombe na Makambako); Kagera (Kayanga); Mtwara (Nanyumbu na Makonde); Singida (Manyoni); Ruvuma (Songea); Tabora (Sikonge, Urambo-Kaliua); Mbeya (Rujewa na Chunya); Kigoma (Kasulu); Lindi (Kilwa Masoko); Mara (Mugumu, Rorya/Tarime); Geita (Geita na Chato); Singida (Singida Mjini na Kiomboi); Katavi (Mpanda); Dodoma (Chamwino na Chemba); Iringa (Mafinga); na Morogoro (Ifakara).


Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amewataka watanzania wamchague Dkt. John Pombe Magufuli kwa sababu anatoka katika chama ambacho kina mikakati inayotokana na mawazo ya wananchi.

 

"Dkt. Magufuli anatoka kwenye Chama ambacho kina utaratibu katika kuendesha nchi, chama ambacho kinaratibu kero za wananchi, ambacho kinasikiliza wananchi mpaka ngazi ya chini," amesema.

 

Ametoa wito huo leo (Jumanne, Septemba 29, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Nkwenda, akiwa njiani kuelekea Isingiro wilayani Kyerwa, mkoani Kagera.

 

"Tumemjaribu na amefanya mambo makubwa katika wizara alizoziongoza na ndiyo maana namleta kwenu Dkt. Magufuli na kumuombea miaka mingine mitano ili alete maendeleo zaidi."

 

Mheshimiwa Majaliwa ambaye yuko mkoani Kagera kumuombea kura mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. Magufuli alitumia fursa hiyo kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Kyerwa, Bw. Innocent Bilakwate, mgombea udiwani wa kata ya Nkwenda, Bw. Edward Katunzi na wagombea wa CCM wa kata za jirani.

 

Amesema CCM ni chama kinachoongozwa na Ilani ya Uchaguzi na kuna mambo yamethibitika katika ilani inayoishia 2020. "Leo tunaleta kitabu kingine cha Ilani ya 2020 - 2025. Kama tuliweza kufanya makubwa ndani ya miaka mitano na kile kitabu kidogo, je huko tuendako itakuwaje?"

 

Akiwa Isingiro kwenye mkutano wa hadhara, Mheshimiwa Majaliwa alisema Serikali ilibadilisha sheria tangu mwaka 2017 na ikazuia uuzaji wa madini ya bati nje ya nchi kwa kutumia njia za panya.

 

"Sheria inatutaka tutenge ekari kadhaa kwa ajili ya wachimbaji wadogo. Leo hii ekari 38,000 zimetolewa kwa wachimbaji wadogo wa madini mbalimbali. Pia tumeanzisha masoko ya madini 26 na vituo vidogo 28 vya kuuzia madini," alisema.

 

Akifafanua kuhusu vitambulisho vya Taifa, Mheshimiwa Majaliwa alisema Tanzania ni nchi ya amani na wengi wanatamani kuja kuishi nchini.

 

Alisema wilaya za Kyerwa, Karagwe na Missenyi ni za mipakani kwa hiyo zina changamoto za uhamijai na masuala ya kiraia. "Ndiyo maana Serikali inakuwa makini katika uhakiki. Tutaimarisha usimamizi ili kila Mtanzania apate kitambulisho.”

 

Pia amewaonya maafisa wanaohusika na utaoaji vitambulisho vya uraia ambao wanapokea hongo na kuwapa vitambulisho hivyo watu wasiostahili.

 

Wakati huohuo, Mheshimiwa Majaliwa amempokea aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Karagwe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Princepius Rwazo ambaye ameamua kurejea CCM. 

 

Akizungumza kwenye mkutano huo, Bw. Rwazo alisema alikuwa mgombea ubunge kwenye uchaguzi mkuu uliopita na aliisumbua sana CCM lakini sasa ameamua kurejea kwani ameona mazuri yanayofanywa na Chama hicho.

 

"CCM imejibu kiu zetu, kimekuwa kama chama cha upinzani, na wapinzani sasa wamelala. Nimerudi CCM, sihitaji cheo chochote, shida yangu ni kujiunga na watu wanaochapa kazi. Nitamuunga mkono Dkt. Magufuli na ndugu yangu Bashungwa," alisema na kushangiliwa.

 

Mheshimiwa Majaliwa anaendelea za ziara yake katika wilaya za Karagwe na Missenyi.

Tuesday, September 29, 2020

MGOMBEA MWENZA WA URAIS KWA TIKETI YA CCM AFANYA KAMPENI BASHNET BABATI VIJIJINI MKOANI MANYARA



 


Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wananchi wa Kijiji cha Ayalagaya Babati Mkoani Manyara wakimsikiliza Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,  alipokuwa akiwasalimia akiwa njiani akielekea Bashnet Babati Vijijini Mkoani Manyara kwa ajili ya kuhutubia mkutano wa  kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM leo Septemba 29,2020.


Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wananchi wa kijiji cha Ayalagaya na Darega Babati  alipokuwa njiani akielekea Wilaya ya Babati Vijijini Mkoani Manyara kwa ajili ya kuhutubia mkutano wa  kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM leo Septemba 29,2020.

Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubi Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wananchi wa Bashnet Wilaya ya Babati Vijijini mkutano wa kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM katika Uwanja wa  Mnadani Bashnet Babati Vijijini Mkoani Manyara leo Septemba 29,2020.  (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)   


Mtoto Hussein Saito (6) Mkaazi wa Kijiji cha Bashnet Wilaya ya Babati Vijijini akiwa na Kuku wake anaemuuza kwa Tshs. 5000 wakati alipokuwa akimsikiliza Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokuwa akihutubia mkutano wa  kampen za Chama cha Mapinduzi CCM katika Uwanja wa Mnadani Bashnet Wilaya ya Babati vijijini Mkoani Manyara leo Septemba 29,2020.
 




Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wananchi wa kijiji cha Dongobesh Babati Vijijini  alipokuwa njiani akielekea Mbulu Mjini kwa ajili ya kuhutubia mkutano wa  kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM leo Septemba 29,2020.

MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM RAIS DKT. JOHN MAGUFULI AZUNGUMZA NA WANANCHI WA MAKAMBAKO MKOANI NJOMBE



Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Makambako mkoani Njombe katika Mkutano wa Kampeni wa CCM leo tarehe 29 Septemba 2020 Makambako mjini

 


Sehemu ya Wananchi wa Makambako waliohudhuria mkutano wa Kampeni wa Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Septemba 2020 Makambako mjini

Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Makambako mkoani Njombe katika Mkutano wa Kampeni wa CCM leo tarehe 29 Septemba 2020 Makambako mjini


 Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili Makambako mjini kwa ajili ya kuwahutubia wananchi wa Makambako leo tarehe 29 Septemba 2020.

 

 Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Makambako mkoani Njombe katika Mkutano wa Kampeni wa CCM leo tarehe 29 Septemba 2020 Makambako mjini


 

Chopa ya CCM ikikatisha katika mji wa Makambako mkoani Njombe kwa ajili ya Kampeni za Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Septemba 2020