Matokeo chanyA+ online




Wednesday, July 31, 2019

UHAMIAJI YAFUNGUKA SUALA LA KUSHIKILIWA MWANDISHI.

Kamishina wa Uraia na Pasipoti, Gerald Kihinga Akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo) Pichani kuhusu kushikiliwa kwa Mwanahabari, Erick Bendera,  katika Mkutano uliofanyika Ofisi za Idara ya Uhamiaji kanda ya Dar es Salaam.(PIcha na Mpiga picha Wetu).

Serikali kupitia Idara ya Uhamiaji imetoa ufafanuzi kuhusu Mwandishi wa kujitegemea Erick Kabendera baada ya kusambaa kwa taarifa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, kuwa amekamatwa na anahojiwa kuhusu uraia wake na Idara ya Uhamiaji Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Uraia na Pasipoti wa Idara ya Uhamiaji Gerald Kihinga, amesema kuwa  Erick Kabendera ameshikiliwa na Jeshi la Polisi na Uhamiaji Jijini Dar es Salaam kwa mahojiano zaidi ili kuweza kupata taarifa juu ya uraia wake.
Kamishna huyo wa Uhamiaji amesema Idara ya Uhamiaji inadhamana kubwa ya kusimamia na kutekeleza Sheria ya uraia wa Tanzania sura ya 357 rejeo la 2002, inayotoa mamlaka kwa taasisi hiyo kuchunguza na kuthibitisha uraia wa mtu yeyote.
“Idara ya Uhamiaji ni chombo kilichopewa dhamana kubwa ya kutekeleza na kusimamia uraia wa Tanzania, kwa hiyo siyo mara ya kwanza kufanya hivyo, sisi tunamshikilia Kabendera kwa mahojiano kuhusu uraia wake, na siyo yeye tu aliyefanyiwa hivyo, idara ya Uhamiaji inatimiza matakwa ya sheria ya uraia nchini na wala si vinginevyo” Alisema.
Alieleza kuwa idara ya Uhamiaji ilipata taarifa za Erick Kabendera kutoka kwa raia wema na ikaamua kumtafuta ili kufanya naye maojiano lakini hakuwa tayari kutoa ushirikiano ikiwa ni pamoja na kukataa kufika ofisi za Uhamiaji, hali iliyopelekea kukamatwa na sasa anaendelea kuhojiwa.
Mkuu huyo wa masuala ya uraia na Pasipoti alifafanua kuwa, kushikiliwa huko kwa Erick Kabendera na kuendelea na mahojiano ni swala ambalo limekuwepo kwa raia wote ambao uraia wao una utata, wakiwemo watu wa kawaida,  watu mashuhuri na wengine wowote ambao kutaonekana uhitaji.
Amesema kumekuwa na ushirikiano baina ya Uhamiaji na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ikwemo Polisi, ili kutekeleza majukumu mbalimbali ya kiusalama kwa nchi hivyo kukamatwa kwa Kabendera siyo jambo geni bali Idara inatimiza majukumu yake chini ya Sheria ya uraia wa Tanzania sura ya 357 rejeo la 2002.


Tuesday, July 30, 2019

WAZIRI WA NISHATI AAGIZA MKANDARASI KUTOA AJIRA 50 KWA VIJANA WA KARATU

Na Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha

Waziri wa Nishati Dk.Medard Kalemani amemwagiza Mkandarasi wa Kampuni ya Nipo Group Mhandisi Shija Magese kuhakikisha anatoa ajira kwa vijana 50 wa Kijiji cha khusumay Wilayani Karatu, ili wasaidie kazi za uwekaji umeme kwenye Vijiji 39 vya wilaya hiyo.

Alitoa agizo hilo jana alipotembelea Wilaya hiyo na kuzindua Rea awamu ya tatu, iliyofanyika kiwilaya katika Shule ya Sekondari ya Baray Khusumay na kuhudhuriwa na wananchi wa Wialaya hiyo.

Alisema ameagiza utoaji wa ajira hiyo kwa sababu mkandarasi huyo amepewa kumaliza kazi ya uwekeaji miundombinu ya umeme na kuwaunganishia wananchi nishati hiyo kwa muada wa miezi 24, lakini mpaka sasa bado nusu ya kazi hajamaliza.

“Sasa naagiza ajiri vijana 50 wa eneo hili ili muda wako tuliowekeana mkataba umalize ni Juni mwaka 2020, lakini nataka umalize kazi hii Desemba 30 mwaka huu, sasa hawa vijana watakusaidia na wakati huo watanufaika na ajira na Meneja wa Wilaya simamia hawa,”alisema

Dk.Kalemani aliahidi kurudi kijijini hapo kufuatilia kama kazi hiyo imeisha kwa wakati muafaka ili wananchi wapate umeme na kuzalisha viwanda vidogovidogo.

Aidha aliagiza Meneja wa Wilaya hiyo Tanesco, Edward Mwakapuja kufungua vituo kwenye vijiji husika ili wananchi wapate unafuu wa kuwafikia na kulipa Sh.27,000 ili waunganishiwe umeme huo wa Rea.

Pia aliwataka Wafanyakazi wa Tanesco kuhakikisha wanafanya kazi za kuhudumia wananchi na kuepuka kuvaa suti kama wanakwenda Kanisani.

“Nimepiga marufuku wafanyakazi Tanesco kuvaa suti labda kama mnaenda kanisani Jumapili, sababu hapa kazi tu, suti na kazi wapi na wapi acheni kabisa pigeni kazi,”alisema Aliwasisihi pia wanachi hao kutunza miundombinu ya umeme wakiwekewa ili waendelee kunufaika nao na kupata maendeleo.

Dk.Kalemani aliwaagiza wanafunzi wa Shule yya Sekondari ya Baray Khusumay kuhakikisha wanafanya vizuri masomo yao na kufaulu vizuri kwa sababu umeme wameshapata.“Someni usiku na msachan lakini pia umeme huu utawamulika msifanye maovu maana shule hii ya wavulana na wasichana mkisimama kwa yale mambo yenu umeme huu utawamulika, someni mfaulu na shule hii mpya,”alisema

Kuhusu suala la kukatika kwa umeme aliagiza Tanesco kuhakikisha wanamaliza tatizo hilo harka, sababu umeme upo wa kutosha hadi ziada.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu Theresia Mahongo alishukuru serikali kwa kuwafikishia umeme kijiji hicho ambacho tangu Uhuru hakijawahi pata umeme, lakini aliomba Waziri kufuatilia changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara wilayani humo.

“Tunaamini tatizo hili litaisha baada ya uzinduzi wa Rea awamu ya tatu kufanyika, sababu kukiwa na umeme tunaamini usalama utakuwa juu na hata ufaulu kwenye shule utaongezeka,”aisema

Akijibu suala la kukatika kwa umeme, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Arusha, Mhandisi Herin Mhina alisema sababu ya kukatika kwa umeme huo kulitokana na utengenezaji wa nguzo zaidi ya 600 ambazo zimewekwa mpya.

Kwa upande wake Mkandarasi wa kampuni ya Nipo Group Shija Magese, aliahidi kumaliza kazi hiyo Desemba mwaka huu na mpaka sasa kati ya Vijiji 39 anavyotakiwa kuweka umeme wa Rea, vijiji 23 ameshajenga miundombinu ya kuweka umeme na kati ya hivyo nane ameshawasha umeme. 
Wafanyakazi kutoka kampuni ya Booygues Energies &services wakiendelea na Mradi wa ujenzi wa njia za kusafirisha umeme Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP)ZTK wa laini kubwa ya msongo wa kilovolti 400 inayoanzia Singida unapita Babati nakuja mkoa wa Arusha hadi Namanga ,ujenzi huo unaendelea katika kijiji cha Kisongo jijini Arusha (Picha na Woinde Shizza, Arusha 
WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani akiongea na wananchi .
WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani alipotembelea Wilaya ya Karatu na kuzindua Rea awamu ya tatu, iliyofanyika kiwilaya katika Shule ya Sekondari ya Baray Khusumay 
WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani akiongea na viongozi wa Tanesco pamoja na mkuu wa wilaya ya karatu wakati alipotembelea kituo cha Tanesco cha wilaya hiyo .

MKUTANO WA SADC NCHINI TANZANIA

#SIW2019 

MAKAMU WA RAIS AZINDUA MRADI WA KUTOKOMEZA UNYANYASAJI DHIDI YA WANAWAKE

Na Charles James, MICHUZI TV

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amezindua mradi wa kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji dhidi ya Wanawake na Watoto kwenye masoko na kushauri elimu iendelee kutolewa kupitia mikutano ndani ya Mitaa na Kata.

Hayo ameyasema leo jijini Dodoma wakati wa uzinduzi huo ambapo amesema katika kupambana na vitendo hivyo vya kikatili Serikali imeimarisha utendaji wa madawati 417 ya jinsia na watoto yaliyopo katika vituo vya Polisi nchini kwa lengo la kuwezesha huduma stahiki kwa watu wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia.

Mama Samia ameitaka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Ofisi ya Rais-TAMISEMI kushirikiana na Jumuiya ya Tawala za Mitaa ambao ndio waratibu wa mradi huo katika kuhakikisha afua zinazotekelezwa kupitia mradi huo zinakua endelevu hata pale utekelezaji wa mradi unapofikia mwisho.

" Ndugu zangu kila mmoja wetu ana haki ya kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia, hivi vitendo havikubaliki na wala haviruhusiwi kisheria. Yeyote atakayethubutu kumdhalilisha mwanamke au mtoto tutamchukulia hatua kali.

" Ni jambo la aibu kuona tunatumia viungo vya wanawake kama matusi, huyu mwanamke unayemdhalilisha tukumbuke ni kama mama zetu majumbani mwetu, hatuwezi kuwa na Taifa lenye amani kama tutaruhusu vitendo hivi, tuungane katika kupiga vita na kutokomeza ukatili wa kijinsia, " amesema Mama Samia.

Akizungumzia ombwe la watoto wadogo kufanya biashara kwenye masoko, Mama Samia amezitaka kamati za masoko kuhakikisha zinashirikiana na mamlaka husika katika kuzuia watoto kufanya biashara sokoni na badala yake wawahimize kwenda shule na kuwaripoti wazazi wanaowatuma watoto wao kufanya biashara.

" Serikali yenu ya awamu ya tano iliwaahidi elimu bure kwa shule ya msingi hadi kidato cha nne. Tunapoona watoto wetu hawaendi shule na wanafanya biashara sokoni tunakua hatumtendei haki Rais wetu Dk John Magufuli kwa zawadi ya elimu bure aliyotuletea. Tuwazuie watoto kufanya biashara sokoni na tushirikiane kuwapeleka shule," amesema Mama Samia.

Aidha katika kutekeleza mradi huo, Mhe Makamu wa Rais amekabidhi Pikipiki 14 kwa ajili ya wataalam wa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Dodoma kwa Kata za Halmashauri ya Chamwino na kuielekeza Wizara kuendeleza utaratibu huo wa kupatia wataalamu hao usafiri ili iwe rahisi kwao kuwafikia wanawake wengi hususani wa vijijini na kuwaunganisha na fursa za kiuchumi.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe Ummy Mwalimu amemshukuru Makamu wa Rais kwa kuzindua mradi huo ambao utakua msaada mkubwa katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia.

" Mhe Makamu wa Rais kama Wizara tumejipanga katika kuhakikisha tunaongeza elimu zaidi kwa wananchi iki tuzidi kupunguza wimbi la vitendo hivi, lengo letu ni kutokomeza kabisa vitendo hivi ili kuwa na Taifa imara ambalo litakua na mshikamano na amani baina yetu bila kujali huyu ni Mwanaume au Mwanamke," amesema Waziri Ummy.

Nae Mwenyekiti wa ALAT Mhe Gulamhafeez Mukadam amesema kuna changamoto kwenye dira ya pamoja juu ya utokomezaji wa vitendo vya ukatili wa kijinsia jambo ambalo linaleta athari ya maendeleo ya wanawake na hivyo kuzorotesha uchumi wa Nchi.

" Nimpongeze Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Mhe Godwin Kunambi kwa namna ambavyo amekua msaada kwa akina Mama wa Jiji hili kwa kuwapatia mikopo inayowawezesha kufanya biashara zao. Serikali za Mitaa jukumu lao ni kuwawezesha wananchi wao kuzipata fursa.

" Lakini pia kuna changamoto ya masoko, lugha chafu kwa wanawake sokoni hizi changamoto zinapaswa kushughulikiwa na kutokomezwa kabisa. Tukiwawezesha wanawake na kuwaepusha na vitendo vya unyanyasaji tutakua tunatengeneza Taifa imara na madhubuti na kuweza kufikia azma ya Mhe Rais ya uchumi wa kati kupitia viwanda," amesema Mhe Mukadam.
 Makamu wa Rais Mhe Mama Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria ufunguzi wa mradi wa kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika maeneo ya masoko. Uzinduzi huo umefnyika jijini Dodoma.
 Wananchi waliohudhuria uzinduzi wa mradi wa kutokomeza vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake wakimsikiliza mgeni rasmi ambaye ni Makamu wa Rais Mhe Mama Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) jijini Dodoma.
Maafisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino wakiwa na pikipiki walizokabidhiwa na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan jijini Dodoma. Pikipiki hizo zimelenga kuwasaidia katika kuwafikia kundi kubwa la wanawake ambao wanafanyiwa unyanyasaji wa kijinsia.

RAIS MAGUFULI ATOA POLE KWA FAMILIA KIFO CHA MEJA JEN MSTAAFU ALBERT LAMECK MBOWE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuwasili nyumbani kwa Marehemu Salasala kwa ajili ya kutoa pole kwa Familia Julai 30,2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa pole kwa Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ikiongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu mara baada ya kutoa pole kwa Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza na Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ikiongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiomba dua maalumu na Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam iliyoongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza baada ya kuomba dua maalumu na Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam iliyoongozwa na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu pole kwa Familia ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alipowatembelea nyumbani kwao Salasala Dsm kwaajili ya kutoa pole kufuatia msiba huo. Julai 30,2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiagana na Waombolezaji wengine akiwa ameambatana na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutoa pole kufuatia msiba huo nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiagana na Mhe. Freeman Mbowe Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni kaka wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Albert Lameck Mbowe aliyefariki dunia julai 28,2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutoa pole kufuatia msiba huo nyumbani kwao Salasala Dsm. Julai 30,2019.

Saturday, July 27, 2019

WAZIRI MKUU ATAKA RUVUMA IONDOE VIKWAZO VYA UWEKEZAJI

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa mkoa wa Ruvuma uendelee kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo na kuondoa vikwazo vyote ili kuvutia wawekezaji zaidi.

“Mkoa wa Ruvuma kama ilivyo mikoa mingine, unazo fursa ambazo zikiendelezwa, zitaleta tija na kusaidia kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa Taifa letu. Nitoe rai kwa mkoa uendelee kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo sambamba na kuondoa vikwazo vyovyote vya uwekezaji na biashara ili kuvutia zaidi wawekezaji wa ndani na nje,” amesema.

Ametoa wito huo leo mchana (Alhamisi, Julai 25, 2019) wakati akifungua Kongamano la Biashara na Uwekezaji mkoani Ruvuma linaloendelea kwenye uwanja wa Majimaji, Manispaa ya Songea. Pia amezindua Mwongozo wa Uwekezaji wa mkoa huo.

Amesema katika ustawi wa uchumi, nchi nyingi hapa duniani zimeweza kukuza uchumi wao kupitia ujenzi wa viwanda na zikafanikiwa kupunguza umasikini katika jamii zao. Amezitaja nchi hizo kuwa ni Marekani, China, Japani, Korea ya Kusini na Ujerumani.

“Tunapaswa kuiga kutoka wa wenzetu. Ndiyo maana Tanzania pia tunahamasisha ujenzi wa viwanda kuanzia ngazi ya vijiji mpaka mikoa ili tulete mageuzi ya kiuchumi yatakayowezesha upatikanaji wa ajira na hatimaye kuondoa umaskini,” amesema Waziri Mkuu na kuongeza:

“Kongamano hili ambalo kaulimbiu yake ni “Ruvuma itavuma kwa uchumi wa viwanda, wekeza sasa,” imelenga kutangaza fursa za uwekezaji na biashara zilizopo mkoani humu, na  inajipambanua vema na kuendana na azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kujenga uchumi wa kati unaoongozwa na viwanda ifikapo 2025.”

Amesema mchango wa sekta ya viwanda kiuchumi na kijamii nchini ni pamoja na kuongeza pato la Taifa na kupandisha hali ya maisha ya wananchi; kusaidia nchi isiyumbe kiuchumi ikizingatiwa kuwa viwanda vingi havitegemei hali ya hewa kama kilimo; kuboresha urari wa biashara (improve balance of trade) kwa sababu tija yake ni kubwa na hasa zikiuzwa bidhaa nyingi nje ya nchi na kupunguza uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi.

Amezitaja faida nyingine kuwa ni kuchangia maendeleo ya sekta nyingine kama za kilimo, uvuvi, elimu na madini; kutengeneza ajira kwa wananchi; kuchagiza na kuharakisha maendeleo ya teknolojia na rasilimali watu na kuwezesha matumizi mazuri ya maliasili zilizopo kwa faida zaidi.

Nyingine ni kuleta uhakika wa soko la mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi, misitu na madini kwa sababu hutumika kama malighafi na kuwepo kwa uhakika wa kuingiza fedha za kigeni nchini kupitia mauzo ya bidhaa nje ambapo husaidia kuagiza mitambo, malighafi na bidhaa nyingine ambazo hazizalishwi nchini.

Mapema, akitoa salamu kwa niaba mabalozi wengine, Mwakilishi wa Balozi wa China, Bw. Xian Bing alisema ana uhakika kuwa kongamano hilo litafanikiwa kuleta mabadiliko mkoani humo kwa sababu wana bidii ya kazi.

“Ninaahidi kuleta wawekezaji kutoka China kwa sababu tunataka waje kuleta teknolojia mpya, wafanye kazi pamoja na Watanzania na wawafundishe teknolojia hizo mpya. Tunataka hapa Ruvuma iwe model (mfano) kwa mikoa mingine,” alisema.

Akielezea kwa kifupi kuhusu mwongozo uliozinduliwa na Waziri Mkuu, mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Hoseana Lunogelo alisema walitumia mfumo shirikishi ili kupata mwongozo unahusisha wawekezaji wa ndani.

“Mwongozo huu umezingatia Dira ya Taifa ya 2025 katika kutimiza azma ya Serikali ya kuwa nchi ya uchumi na viwanda, tumeshirikisha wananchi wa mkoa wa Ruvuma ili wasibakie kuwa watazamaji,” alisema.
PMO_9503
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na wananchi, baada ya kufungua maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji mkoani Ruvuma, Julai 25.2019.. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
PMO_9487
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akimsikiliza Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa China Tanzania, Bwana Xian Ding, wakati alipoipongeza Serikali ya awamu ya tano katika kuwaletea wananchi wake maendeleo, kwenye maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji,yaliyofanyika katika Mkoa wa Ruvuma, Julai 25.2019.
PMO_9525
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizindua kitabu cha muongozo wa uwekezaji katika Mkoa wa Ruvuma, kwenye maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji mkoani Ruvuma. Julai 25.2019. Tokea kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje John Ndumbalo na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
PMO_5143
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa amebeba mkaa wa mawe, wakati akikagua mabanda kwenye banda la TANCOAL, katika  maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji mkoani Ruvuma, Julai 25.2019. Tokea kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme na kulia ni Mkuu wa Jiolojia TANCOAL.
PMO_5164
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiangalia mkaa wa mawe, uliyotengenezwa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na wajasiriamali wa kikundi cha Mbalawala Women Group, wakati akikagua mabanda kwenye maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji mkoani Ruvuma, Julai 25.2019. Tokea kulia ni Meneja wa Fedha wa kikundi hicho, Esta Silas na Msimamizi wa Mradi, Hajra Yakub.
PMO_5127
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme (kushoto), akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Mbinga Coffee Curing Company, kabla ya kufungua maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji mkoani Ruvuma, Julai 25.2019.
PMO_5004
PMO_5027
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme, akiangalia na vikundi vya ngoma, kwenye maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji mkoani Ruvuma, Julai 25.2019.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.SHEIN AWASILI ZANZIBAR AKITOKEA NCHINI UINGEREZA KWA ZIARA MAALUM

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, alipowasili Uwanja wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea Nchini Uingereza kwa ziara Maalum.(Picha na Ikulu) 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Zanzibar, alipowasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea Nchini Uingereza, alipokuwa na ziara Maalum.,(Picha na Ikulu) 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein,, akisalimiana na Wananchi waliofika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar kumpokea akitokea Nchini Uingereza kwa ziara Maalum.(Picha na Ikulu)

Friday, July 26, 2019

HIFADHI MPYA YA MWL.NYERERE KUKUZA UTALII SELOUS.



Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameitaka wizara ya Maliasili na Utalii kutenganisha eneo la uwindaji Selou (Hunting block) kwa kutengeneza Hifadhi ya Taifa ambayo itaitwa Hifadhi ya taifa ya Mwalimu Julius Nyerere.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa mto Rufiji mkoani Pwani utakaozalisha megawatt 2,115, Rais Magufuli amesema kuwa eneo la uwindaji la Selou ni eneo ambalo limezunguka mradi huo mkubwa wa umeme na lina urefu wa kilomita za mraba elfu 57.

“Eneo la Selou ni eneo kubwa ambalo linachukua takribani kilomita 50, hivyo ni lazima Wizara itenge eneo ambalo litatengenezwa na kuwa Hifadhi kuweza kukidhi mahitaji ya utalii na kukisaidia kizazi kijacho kuendelea kuenzi mambo ambayo ameyafanya baba wa Taifa,” amesema Rais Magufuli.

Amesema maeneo ya uwindaji wa wanyama yanafikia 47 katika mbuga ya wanayama Selou hivyo Wizara ya Maliasili lazima itenge eneo la hifadhi na la uwindaji, ili kuimarisha utalii na kuvutia watalii wengi katika mbuga hiyo

Rais Magufuli alisisitiza kuwepo kwa utaratibu kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kuangalia maeneno ambayo yanavitalu wa uwindaji ili kuhakikisha kuwa Serikali inafaidika na maeneno hayo, pia aliagiza barabara ya kutoka Fuga kilomita 60 kwenda mahari ambapo mradi unajengwa ianze kutengenezwa kwa rami ili kufungua sekta ya utalii katika Mbuga ya wanayama Selous.

Aidha, Rais Magufuli amesema kuwa mradi wa kufua umeme wa mto Rufiji ni mradi ambao unaweza kudumu kwa muda wa miaka 60 ambapo utasaidia kuzalisha umeme wa kutosha na kusaidia Tanzania kuweza kutekeleza malengo ya milenia ya maendeleo endelevu.

Amesema mradi wa mto Rufiji utasaidia kuchochea maendeleo katika sekta ya viwanda ambapo wewekezaji wataweza kupata umeme wa uhakika na kwa bei nafuu na wenye kuaminika ili kuweza kuzarisha bidhaa zenye ubora.

“Mradi huu wa umeme wa mto Rufiji unaweza kudumu kwa muda wa miaka 60 na kusaidia watanzania kupata umeme wa uhakika na wenye gharama nafuu ambao utasaidia wawekezaji kupata huduma ya umeme kwa uhakika bila mgao ili kuweza kuzarisha bidhaa zenye ubora na kuweza ushindano kwenye masoko mbalimbali ya kimataifa,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli alisisitiza kuwa katika utekelezaji wa mradi huo, mkandarasi anatakiwa kutumia wafanyakazi walioko karibu kwa kazi ambazo siyo za kitaalamu, akasisitiza ajira zitolewe kwa wenyeji wa maeneo ya mradi kwa mikoa ya Morogoro na Pwani, na amewataka wananchi kuchangamkia fursa kwa miezi hiyo 36 ya ujenzi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema kuwa Ndoto ya Rais Magufuli ya kuenzi mambo makubwa ya Baba wa Taifa, Mwl.Julias Nyerere ikiwemo utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la kufua umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji.

“Mhe. Rais, ndoto yako leo imeanza kupata mafanikio, ndoto yako ni kupeleka umeme hadi kule kijijini kwa wananchi wa kawaida na umetoa agizo kuwa kila nyumba ya mtanzania iwe ya bati, nyasi au tembe lazima iwake umeme, kwa hiyo umeme huu ambao ujenzi wake umezinduliwa leo ni kukamilisha azma yako bila kujali maisha ya watanzania”, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu alisema kuwa kampuni zinazojenga mradi huo mkubwa wa kufua umeme Tanzania, Els weldey na Arab Contructors, zinafanya kazi nzuri kwa hiyo zitatekeleza mradi huo kwa weledi mkubwa, kama zinavyofanya kule Misri.

Naye Waziri wa Nishati amesema mradi huo unabainisha mambo mawili ya kumuenzi Rais wa kwanza Tanzania, hayati Julius Nyerere, ambayo Rais Magufuli anatekeleza likiwemo kuhamisha makao makuu ya nchi kwenda Dododma, ambayo tayari yanatekelezwa, likiwemo la ujenzi wa Bwawa la Rufiji.

“Naomba niwakumbushe watanzania Mhe. Rais ametengeneza mambo makubwa mawili ya ndoto ya baba wa Taifa ikiwemo kuhamisha makao makuu ya nchi kwenda Dododma na utekelezaji wa mradi mahususi wa bwawa la kufua umeme, mradi mkubwa wa kwanza Tanzania, Afrika Mashariki na wa nne barani Afrika, huku ukiingia kwenye mabwawa 70 makubwa duniani yakuzarisha umeme,” Waziri Kalemani.

Aidha Waziri Kalemani amesema kuwa mradi huu utekelezaji wake utachukua miezi 42 ambapo hadi sasa miezi sita imeshapita na kubaki miezi 36 kukamilisha ujenzi wa mradi huo ambao unategemewa kukamilika Juni 13, 2022.

Waziri Kalemani aliongeza kuwa katika ujenzi wa mradi huo kazi kubwa ya mkandarasi ni pamoja na ujenzi wa bwawa kubwa litakaloweza kuhifadhi maji ya mita za ujazo billioni 33.2, ujenzi wa Power house itakayokuwa na mashine tisa zenye kuzalisha megawati 235 kwa kila mashine na kazi ya mwisho ni kujenga substation yenye kilovolt 400, ambapo ni umeme mkubwa utakaotumika kwenye uchumi wa viwanda.

Umeme huo utasafirishwa kutoka Rufiji kwenda Chalinze umbali wa kilomita 127 kwa dola za kimarekani 188 Chalinze mpaka Dar es Salaam na Dodoma na ndio umeme utakao tumika kuendesha Treni ya kisasa (SGR), lengo la Serikali ni kufikisha megawati 10,000 ifikapo mwaka 2025 kwahiyo mradi huu mkubwa ni kichocheo kikubwa sana kuelekea uzarishaji wa hizo megawati.

Kwa upande wake Waziri wa nishati na umeme kutoka Misri Dkt. Mohamed Shaker amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo unaimarisha mahusiano ya Tanzania na Misri katika sekta mbalimbali, ikiwemo ya nishati.

“Ujenzi wa mradi huu mkubwa ni moja ya hatua kubwa katika mahusiano ya nchi mbili ambayo itahamasisha zaidi utekelezaji wa miradi mingine ya undugu kati ya Tanzania na Misri, hususani kwenye nyanja ya umeme, nipende kusisistiza kwamba mradi huu wa umeme Rufiji unaungwa mkono na Rais wa Misri, Abdel Fattah El-Sisi” Waziri Shaker.

Nchi ya Misri itaendelea kushirikiana na Tanzania katika utoaji wa mafunzo ya teknolojia ya kuzalisha umeme, kwani ina vituo 22 vya kutolea mafunzo hayo na imetoa nafasi 50 kwa wataalamu kutoka Tanzania kwenda kujifunza masuala ya ufuaji na uzalishaji umeme.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia eneo la bonde katika mto Rufiji mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa umeme.

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA KUFUA UMEME WA MAJI KATIKA MTO RUFIJI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi mradi wa Ujenzi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji katikati ya Morogoro na Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker mara baada ya kuweka Jiwe la Msingi mradi wa Ujenzi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji katikati ya Morogoro na Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia pamoja na viongozi wengine mara baada ya tukio hilo la uwekaji wa Jiwe la Msingi.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker, Waziri wa Nishati Medard Kalemani pamoja na viongozi wengine akisikiliza namna mradi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji utakavyokuwa ukifanya kazi mara baada ya kukamilika.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia michoro ya ujenzi huo mkubwa wa kufua umeme.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker wakati wakielekea kwenda kuweka jiwe hilo la msingi.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mitambo itakayotumika katika mradi huo mkubwa wa kufua umeme.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia eneo la bonde katika mto Rufiji mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa umeme.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi mara baada ya kuwasili katika eneo la Mradi.
Eneo la mto Rufiji ambalo litatumika katika ujenzi huo wa kufua umeme kama linavyoonekana. PICHA NA IKULU.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Julai, 2019 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme katika mto Rufiji Mkoani Pwani ambao utakamilika Juni 2022 na kuzalisha megawati 2,115.

Sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la mradi huo zimefanyika kando ya eneo litakapojengwa bwawa la maji na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Nishati wa Misri Mhe. Dkt. Mohamed Shaker, Mawaziri na Naibu Mawaziri wa Tanzania, Wabunge, Viongozi Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, Viongozi wa Dini, Viongozi wa vyama vya siasa na viongozi wa taasisi mbalimbali za Serikali.

Ujenzi wa mradi huo utagharimu shilingi za Kitanzania Trilioni 6.5 na bwawa litakalojengwa litakuwa la kwanza kwa ukubwa Afrika Mashariki na la nne kwa ukubwa Barani Afrika, na Mhe. Rais Magufuli amependekeza bwana hilo liitwe Bwawa la Nyerere ikiwa ni kutambua na kuenzi maono ya Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyetaka kujenga bwawa hilo wakati wa uongozi wake.

Katika hotuba yake, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kusimamia utekelezaji mradi huo na ameeleza kuwa Serikali imechukua hatua za kujenga bwawa hilo ili kuongeza uzalishaji wa umeme nchini kutoka megawati 1,601 zinazozalishwa hivi sasa, hadi kufikia megawati 10,000 ifikapo mwaka 2025.

Mhe. Rais Magufuli amesema pamoja na kutekeleza mradi huo, Serikali itajenga mradi wa kuzalisha umeme katika mto Ruhudji utakaozalisha megawati 359, mradi wa Lumakali megawati 222, mradi wa kakono megawati 87, Rusumo megawati 80 na mingine itakayotumia nishati ya gesi, makaa ya mawe, jua, jotoardhi, upepo na urani.

Amewataka wakandarasi wanaojenga mradi (Arab Contractors na Elsewedy Electric za Misri) kukamilisha mradi huo kabla ya Juni 2022 hasa ikizingatiwa hakuna tatizo la fedha ili Watanzania waanze kunufaika mapema.

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Medard Kalemani amesema tayari wakandarasi wanaojenga mradi huo wamelipwa asilimia 15 ya fedha zote za mradi huo ambayo ni sawa na shilingi Trilioni 1.007 na kwamba ujenzi utahusisha bwawa la maji lenye uwezo wa kukusanya mita za ujazo Bilioni 33.2, Jengo la mitambo ya kuzalisha umeme litakalokuwa na mitambo 9, kituo cha umeme na njia ya kusafirishia umeme yenye urefu wa kilometa 135 hadi kufika Chalinze.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson amesema Wabunge wanampongeza Mhe. Rais Magufuli kwa utekelezaji wa mradi huo na wanaamini kuwa umeme utakaozalishwa utawasaidia Watanzania na pia kufanikisha miradi mikubwa inayotekelezwa katika awamu hii ikiwemo ujenzi wa reli na ujenzi wa viwanda.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amesema kuanza kwa ujenzi wa mradi huo ni mafanikio makubwa ya Mhe. Rais Magufuli ambaye amedhamiria kuhakikisha kila nyumba ya Mtanzania inapatiwa umeme.

Waziri wa Nishati wa Misri amewasilisha salamu za Rais wa Misri, Mhe. Abdel Fattah El- Sisi ambaye ameahidi kufuatilia ujenzi wa mradi huo unaofanywa na kampuni za Misri na pia ameahidi kuwa nchi hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali ikiwemo kutoa udhamini wa masomo ya nishati jadidifu kwa wanafunzi 50 ambao watasaidia juhudi za kuongeza uzalishaji wa umeme hapa nchini.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania kujivunia mafanikio haya makubwa ya kuongeza uzalishaji wa umeme nchini na kutoyumbishwa na wanaopinga utekelezaji wa mradi huo kwa kigezo cha uharibifu wa mazingira kwani mradi huo utasaidia zaidi kutunza mazingira kwa watu kutumia umeme badala ya kuni na mkaa zinazotokana na ukataji wa miti, na pia utasaidia kuwepo uvuvi, kilimo cha umwagiliaji na kuinua utalii kutokana na Wanyama wengi kupata maji ya uhakika.

“Kwenye hili pori la Selous kuna hoteli za kitalii za gharama kubwa, kuna vitalu vya utalii 47 na kuna uwindaji unaendelea, sasa haiwezekani sisi tukitaka kujenga bwawa la kuzalisha umeme tuambiwe tunaharibu mazingira wakati eneo tunalotumia ni chini ya asilimia 3 ya pori la Selous.

Mradi huu umekumbana na upinzani mkali wa ndani na nje ya nchi, lakini kwa kuwa sisi ni Taifa huru na sio masikini kama watu wanavyodhani, tumeamua kutekeleza mradi huu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ameagiza kumegwa kwa sehemu ya Pori la Akiba la Selous ili iwe Hifadhi ya Taifa na amependekeza iitwe Hifadhi ya Nyerere na sehemu yenye vitalu vya uwindaji iendelee, lengo likiwa kuimarisha zaidi uhifadhi wa maliasili katika eneo hilo na kupata manufaa zaidi.

Ameagiza barabara ya kuunganisha eneo la mradi huo mpaka Fuga ianze kujengwa kwa kiwango cha lami hatua kwa hatua ili kurahisisha mawasiliano ya eneo hilo.Pamoja na kutaka wananchi wa Morogoro na Pwani wapewe kipaumbele katika ajira wakati wa mradi huo, Mhe. Rais Magufuli ameagiza mradi huo kukatiwa bima ya Taifa, utoaji wa vibali vya kazi kwa wafanyakazi wa kutoka nje ya nchi ufanyike haraka na vyombo vya ulinzi na usalama vya Morogoro na Pwani vishirikiane kuulinda.

Pia amewataka viongozi na wananchi wa Mikoa yote yenye vyanzo vya maji vinavyomwaga maji yake katika mto Rufiji kuhakikisha wanavitunza vyanzo hivyo ili viendelee kuchangia maji mengi katika mto Rufiji.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Rufiji
26 Julai, 2019