Matokeo chanyA+ online




Saturday, July 31, 2021

RAIS SAMIA APOKEA UJUMBE MAALUM KUTOKA KWA RAIS TSHISEKEDI WA CONGO

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkaribisha Mjumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, ambaye ni Waziri wa Fedha wa Nchi hiyo Mhe. Nicolas Kazadi Kadino, mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika mazungumzo na Mjumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, ambaye ni Waziri wa Fedha wa Nchi hiyo Mhe. Nicolas Kazadi Kadino, mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Antoine Tshisekedi ulioongozwa na Waziri wa Fedha wa Nchi hiyo Mhe. Nicolas Kazadi Kadino, ulipowasili Ikulu Jijini Dar es Salaam  tarehe 30 Julai, 2021. Picha na Ikulu

Wednesday, July 28, 2021

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA CHANJO YA UVIKO 19 JIJINI DAR ES SALAAM

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Chanjo ya Uviko 19 katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam leo Julai 28,2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionesha Cheti cha Uthibitisho wa Chanjo muda mfupi baada ya kuzindua Chanjo ya Uviko 19 katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam leo Julai 28,2021.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akipata Chanjo ya Uviko 19 katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam leo Julai 28,2021. Picha na Ikulu.

RAIS SAMIA AKUTANA NA MKURUGENZI WA KITUO CHA KUDHIBITI NA KUZUWIA MAGONJWA BARANI AFRIKA (CDC)


 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mkurugenzi wa Kituo cha kudhibiti na kuzuia Magonjwa Barani Afrika (CDC) Dkt. John Nkengasong, Wakati Dkt. John alipofika  Ikulu Jijini Dar es salaam leo Julai 27,2021. (Picha na Ikulu).


Tuesday, July 27, 2021

WAZIRI MKUU MAJALIWA: HAKUNA MTU ALIYELAZIMISHWA KUCHANJA CHANJO YA UVIKO 19,WANANCHI WAPUUZE UPOTOSHWAJI UNAONDELEA MITANDAONI.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali haijamlazimisha na wala haitamlazimisha mwananchi kuchanjwa chanjo ya ugonjwa wa UVIKO 19, hivyo amewataka Watanzania wapuuze upotoshaji unaosambazwa kupitia mitandao ya kijamii.

"Hakuna aliyelazimishwa kuchanja chanjo hiyo na wala hakuna mahali palipoandikwa kwamba lazima wananchi wachanjwe. Chanjo ni hiari tusipotoshane kwa sababu hakuna Serikali inayoweza kuandaa mpango wa kuwaangamiza wananchi wake."

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 27, 2021) wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Ruangwa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Nandagala ambapo amewasisitiza waendelee kuchukua tahadhari na kujikinga na UVIKO 19.

Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali imeleta chanjo hiyo ili kutoa fursa kwa Watanzania watakaohitaji kuchanjwa kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa wa UVIKO 19 waweze kuipata kwa ukaribu na urahisi zaidi na si vinginevyo.

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amewasisitiza Watanzania waendeleze tabia ya kunawa mikono mara kwa mara na maji safi yanayotiririka na sabuni, watumie vitakasa mikono pamoja na kuvaa barakoa zilizothibitishwa na mamlaka husika.

Mbali na maelekezo hayo, Pia Waziri Mkuu amesema ni vema kwa sasa wananchi wakajiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima na inapolazimu basi wazingatie kukaa umbali wa mita moja au zaidi kutoka mtu mmoja hadi mwingine lengo likiwa ni kujikinga na UVIKO 19.

Mheshimiwa Majaliwa amesema wananchi wanatakiwa wafanye mazoezi ya mara kwa mara kulingana na afya zao pamoja na mazingira yanayowazunguka, pia amewasihi wazingatie lishe bora.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amewahakikishia wananchi wa wilaya ya Ruangwa kwamba Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika wilaya yao na Tanzania kwa ujumla, hivyo waendelee kuiamini Serikali yao.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatekeleza kampeni ya kumtua mama ndoo kichwani ili kuhakikisha wananchi wote nchini wanapata huduma hiyo karibu na maeneo yao ya makazi. Amewataka waendelee kuiamini Serikali yao kwa sababu imedhamiria kuwatumikia.

Amesema tatizo la maji wilayani Ruangwa linaenda kuwa historia kwa sababu Serikali inatekeleza ujenzi wa mradi wa maji wa Mbwinji ambao unatoa maji Ndanda hadi Ruangwa. “Mradi huu mkubwa utapunguza tatizo la upatikanaji wa maji wilayani Ruangwa.”

Kwa upande wake, Waziri wa Maji Jumaa Aweso amemuhakikishia Waziri Mkuu kwamba atasimamia ipasavyo kuhakikisha mradi wa maji wa Mbwinji-Ruangwa unakamilika kwa wakati ili wananchi wa wilaya hiyo waweze kuondokana na tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama.

Aweso amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika maeneo yote nchini, amewaomba wananchi waendelee kuwa na subra.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Thursday, July 22, 2021

RAIS DKT.MWINYI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WASANII WA BONGO FLEVA IKULU ZANZIBAR.






Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wasanii wa Muziki wa Bongo Fleva walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.(Picha na Ikulu).

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva Faustina Charles ( Nandy ) akizungumza wakati walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi.(hayupo pichani) mazungumzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar, akiwa Zanzibar katika onesho lake la Tamasha la Muziki la Nandy lililofanyika jana usiku 21-7-2021 katika Uwanja wa Mao Zedung Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Wasanii wa Muziki wa Bongo Fleva walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu, wakiwa Zanzibar wakishiriki katika Tamasha la Muziki la Nandy lililofanyika jana usiku 21/7/2021 katika Uwanja wa Mao Zeding.(Picha na Ikulu)



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Wasanii wa Muziki wa Bongo Fleva ukiongozwa na Mwanamuzi Nandy, walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar, wakiwa Zanzibar katika Tamasha la Muziki la Nandy lililofanyika jana usiku 21/7/2021. Katika uwanja wa Mao Zedung Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na Wasanii wa Muziki wa Bongo Fleva, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

RC SINGIDA AWATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA KUTOKA TAASISI YA PASS

Mkoa Singida Dkt.Binilith Mahenge, akizungumza na wadau wa kilimo wakati akifungua mkutano wa wadau hao jana ulioandaliwa na Taasisi ya mikopo ya Pass inayojishughulisha na utoaji wa mikopo na udhamini kwa wakulima.
Meneja Maendeleo ya Biashara wa Taasisi hiyo,  Hamisi Mmomi akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa Taasisi hiyo kwenye mkutano huo.
Meneja wa Kanda ya Kati wa Taasisi hiyo,  Hadija Seif  akizungumza kwenye mkutano huo.
Wadau wa kilimo wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Wadau wa kilimo wakiwa kwenye mkutano huo.
 



Na Dotto Mwaibale, Singida

Mkuu wa Mkoa Singida Dkt.Binilith Mahenge amewataka wananchi wa mkoa huo kuchangamkia ujio wa Taasisi ya mikopo ya Pass inayojishughulisha na utoaji wa mikopo na udhamini kwa wakulima kama fursa kwao katika kilimo cha alizeti.

Dkt. Mahenge aliyasema hayo mjini hapa jana wakati akifungua mkutano wa wadau wa kilimo cha zao la alizeti ulioandaliwa na taasisi hiyo.

"Nawahasa wananchi wangu wa  Singida muichukulie taasisi ya Pass kuwa ni fursa moja wapo itakayowawezesha kuharakisha kuwaletea maendeleo," alisema Mahenge.

Alisema Serikali mkoani hapa itawapa Pass ushirikiano wa kutosha ili wananchi wapate huduma hizo muhimu zitakazo wainua kiuchumi kupitia kilimo cha alizeti.

Mahenge aliitaka  taasisi hiyo kupanua wigo wa kujenga uelewa kwa kufanya mikutano mbalimbali kuanzia ngazi ya wilaya jambo litakalosaidia kuharakisha upatikanaji wa huduma bora kwa kutumia fursa ya uwepo wa Taasisi hiyo na mabenki kwa ufanisi zaidi.

Pia alisema itawezesha kutengeneza mazingira mazuri ya kuibua changamoto nyingi na kuendelea kuweka mazingira rafiki ya kukabiliana nazo ili kuyafikia mapinduzi ya kilimo.

Alisema wakulima wengi ni wadogo na bado wanatumia teknolojia duni lakini kupitia taasisi  kama hiyo wataweza kuweka mazingira rafiki ya kuwafikia wadau wengi wa sekta ya kilimo kundi ambalo kwa muda mrefu limekuwa haliwezi kuzifikia taasisi za kifedha kwa ufanisi.

Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Taasisi hiyo Hamisi Mmomi akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa Taasisi hiyo alisema tangu taasisi hiyo ianzishwe hadi kufikia mwezi Desemba mwaka jana tayari wamekwisha wakopesha wakopaji zaidi ya 46,000 na kudhamini mikopo ya Trioni 1.08.

Alisema katika wakopaji hao 46,000 wanufaika wa moja kwa moja ni zaidi ya milioni 1.6 kwa sababu wakopaji wengine kama vyama vya ushirika kuna wanachama kuanzia 50, 100 hadi 200 hivyo kufikisha idadi hiyo.

Alisema mikopo hiyo imetengeneza ajira zaidi ya milioni 2.5 kutokana na wakulima kuajiri wakulima na kuwa mikopo hiyo wakopaji wamekuwa wakiirejesha kwa wakati kutokana na utaratibu mzuri waliouweka wa kuipitia  miradi walioikopea fedha hizo.

WAZIRI MKUU AITAKA BODI YA KOROSHO KUTAFUTA MASOKO YA UHAKIKA

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameiagiza Bodi ya Korosho Tanzania ihakikishe inatafuta masoko ya uhakika ya zao hilo na yatakayotoa bei nzuri na kuwanufaisha wakulima.

 Pia, Waziri Mkuu ameitaka bodi hiyo isimamie mwenendo wa ujenzi wa viwanda vidogo na vikubwa vya kubangulia korosho katika maeneo yote yanayolima zao hilo ili kuondokana na uuzwaji wa korosho ghafi.

 Mheshimiwa Majaliwa ametoa maagizo hayo leo (Alhamisi, Julai 22, 2021) wakati akizungumza na Wakuu wa mikoa ya Lindi, Pwani, Mtwara na Ruvuma, Mrajisi wa Ushirika, Viongozi wa vyama Vikuu vya Ushirika wa Korosho katika kikao kilichohusu upatikanaji wa pembejeo za korosho kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa mkoani wa Lindi.

 Amesema lazima bodi hiyo ambayo ameizindua lazima iwajibike ipasavyo katika kuhakikisha inaongeza uzalishaji wa zao hilo na iwapo itashindwa Serikali haitosita kuivunja. 

 "Lazima mfuatilie na kuufahamu mwenendo wa zao mnalolisimamia na mjue mfumo unaotumika katika mauzo yake. Pia muwe na takwimu za wakulima na ukubwa wa mashamba yao ili kuweza kuwahudumia kwa urahisi."

 Waziri Mkuu amesema bodi hiyo inatakiwa iandae kalenda maalumu inayoonesha hatua zote zinazopaswa kufuatwa katika kilimo cha zao hilo kuanzia hatua za uandaaji wa shamba hadi mavuno kwa kuzingatia hali ya hewa ya eneo husika na ipelekwe kwa wakulima.

 Amesisiza kwamba utaalamu lazima ufuatwe na uzingatiwe katika kilimo hilo kwa lengo la kuongeza tija kwa wakulima. Pia, Waziri Mkuu ameitaka bodi hiyo ihakikishe pembejeo ikiwemo miche bora na viuatilifu vinapatikana kwa urahisi.

 Kadhalika, Waziri Mkuu ameigiza bodi ya korosho iweke mkakati wa utoaji wa elimu kwa wakulima kuhusu kilimo cha zao hilo ikiwa ni pamoja na faida ya kulima zao la korosho. "Tumieni magari maalumu kwa ajili ya kwenda kuwafuata wakulima katika maeneo yao na kuwapa elimu."

 Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema tayari mchakato wa kuviwezesha vyama vya wakulima kuanza ubanguaji wa korosho umeanza ambapo katika msimu wa mwaka huu TANECU imepata mkopo kutoka CRDB na itaanza kubangua tani 2,500.

 Amesema vyama vingine vitakavyofuata utaratibu huo baada ya TANECU ni TAMCU, MAMCU na RUNALI ambavyo vyote vinampango wa kuanzisha viwanda vyenye uwezo wa kuchakata tani 2,5000 za korosho kwa mwaka.

 Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho, Brigedia Jenerali Mstaafu Aloyce Mwanjile amesema wamepokea maelekezo na maagizo yote kwamba watayafanyia kazi kwa kusirikiana na wajumbe wa bodi hiyo na Menejimenti na kwamba hawatafanyakazi kwa mazoea.





 

KIVUKO CHA MV. MAFANIKIO KUREJEA MTWARA BAADA YA WIKI TATU

 

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akimuonyesha kitu Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Marine Khalid Songoro kulia wakati wakikagua moja ya milango ya kivuko cha MV. MAFANIKIO kinachofanyiwa ukarabati na Kampuni ya Songoro Marine katika yadi yake iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Kivuko hicho kinachotoa huduma kati ya Msangamkuu na Msemo Mkoani Mtwara kinatarajiwa kurejea Mtwara baada ya wiki tatu kuendelea kutoa huduma. Katikati ni Mkuu wa Kivuko Magogoni Kigamboni Mhandisi Samuel Chibwana

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (wa tatu kushoto) akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Marine Khalid Songoro (wa tatu kulia) wakati akikagua maendeleo ya kivuko cha MV. MAFANIKIO ambacho kimeletwa katika yadi ya Songoro Kigamboni jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanyiwa ukarabati. Kivuko hicho kinachotoa huduma kati ya Msangamkuu na Msemo Mkoani Mtwara kinatarajiwa kurejea Mtwara baada ya wiki tatu kuendelea kutoa huduma.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Marine Khalid Songoro (wa pili kulia) na Mkuu wa Kivuko Magogoni Kigamboni Mhandisi Samuel Chibwana kulia wakikagua kivuko cha MV. MAFANIKIO kinachofanyiwa ukarabati na Kampuni ya Songoro Marine katika yadi yake iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Kivuko hicho kinachotoa huduma kati ya Msangamkuu na Msemo Mkoani Mtwara kinatarajiwa kurejea Mtwara baada ya wiki tatu kuendelea kutoa huduma.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Marine Khalid Songoro akimuonyesha kitu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle wakati akikagua kivuko cha MV. MAFANIKIO kinachofanyiwa ukarabati na Kampuni ya Songoro Marine katika yadi yake iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Kivuko hicho kinachotoa huduma kati ya Msangamkuu na Msemo Mkoani Mtwara kinatarajiwa kurejea Mtwara baada ya wiki tatu kuendelea kutoa huduma. Kulia ni Mkuu wa Kivuko Magogoni Kigamboni Mhandisi Samuel Chibwana

 

PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO (TEMESA DAR ES SALAAM)

*****************************

Huduma za Kivuko kwa wakazi wa Msangamkuu na Msemo Mkoani Mtwara zinatarajiwa kurejea baaada ya takribani wiki tatu kutoka sasa, hayo yamebainishwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle leo wakati alipotembelea eneo la Yadi ya Songoro Marine Kigamboni jijini Dar es Salaam kukagua maendeleo ya ukarabati huo unaofanywa na kampuni ya Songoro.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kukagua ukarabati wa kivuko hicho, Mtendaji Mkuu Maselle amesema kivuko hicho kipo mbioni kukamilika kwani Mkandarasi ametakiwa kukamilisha kazi hiyo ndani ya muda mfupi ili wakazi wanaotegemea kivuko hicho Mkoani Mtwara waweze kurejeshewa huduma zake mapema iwezekanavyo.

‘’Tumekisafirisha kivuko hiki kutoka Mtwara kuja hapa Dar es salaam kwakuwa ni gharama ndogo kukileta hapa kuliko kusafirisha vifaaa vyote vya matengenezo kwenda kufanyia Mtwara ndio maana mkandarasi akaamua kukivuta kivuko hiki kije hapa ili muda wa matengenezo uwe mfupi zaidi’’.

Mhandisi Maselle amesisitiza kuwa utaratibu wa kufanya matengenezo kwa vivuko vya TEMESA ni muhimu sana kwa vyombo vya maji kwakuwa maji ya bahari yana chumvi nyingi na kali hivo kama kivuko kitakuwa hakijafanyiwa ukarabati kwa muda mrefu kitakuwa kinaharibika na kitashindwa kufanya kazi kwani chuma chake kitaliwa na maji ya chumvi na hivyo kushindwa kudumu kwa muda mrefu.

‘’Ni utaratibu wa kawaida kwa TEMESA kila ambapo kivuko kinafikia muda wake wa matengenezo kinga, lazima kitolewe na kupelekwa kufanyiwa ukarabati na matengenezo na hii ni hatua mojawapo ambayo tumefanya na tunaendelea na ukarabati wa vivuko vingine  ambavyo muda wake wa ukarabati umefika’’. Alisema Mhandisi Maselle ambapo amewaomba wakazi wa Mtwara wavumilie wakati kivuko hicho kikiendelea kufanyiwa ukarabati ambapo wakazi hao wamepelekewa boti mbili za MV. TANGAZO na MV. KUCHELE ambazo zinatoa huduma kwa sasa kwa wakazi hao.

 Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Marine Khalid Songoro akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya tukio hilo la ukaguzi amesema, ukarabati wa kivuko hicho umefikia asilimia 85% na ameongeza kuwa wanatarajiwa kumaliza ukarabati wake ifikapo Tarehe 15 mwezi Agosti.

‘’Kazi kubwa zote tulizozifanya ziko kwenye hatua ya mwisho ili kuweza kukamilisha ukarabati wa kivuko hicho,’’ amesema Songoro.

Kivuko cha MV. MAFANIKIO kina uwezo wa kubeba abiria 100 na magari 6 sawa na tani 50 na kinatoa huduma zake kati ya Msangamkuu na Msemo Mkoani Mtwara mjini.

RAIS SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA TONY BLAIR WAZIRI MKUU MSTAAFU WA UINGEREZA


 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza Mhe. Tony Blair wakati Mhe. Blair alipofika  Ikulu Jijini Dar es salaam leo Julai 22,2021. (Picha na Ikulu) 
 
Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza Mhe. Tony Blair wakati Mhe. Blair , akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipofika  Ikulu Jijini Dar es salaam leo Julai 22,2021. 

(Picha na Ikulu)

Tuesday, July 20, 2021

DAWASA YAPONGEZWA KWA MATUMIZI MAZURI YA FEDHA ZA MAPATO YAO



Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema mamlaka ya maji  safi na usafi wa mazingira DAWASA imepiga hatua kubwa katika usimamizi wa miradi ya maji nchini ikiwemo matumizi mazuri ya fedha zinazopatikana katika Mamlaka hiyo kwa kuwekeza kiasi cha Shilingi Bilioni 17.8 katika Miradi wa Maji wa Ruvu Juu mpaka Msoga itakayotatua kero ya Maji kwa Wananchi zaidi ya 122,000 wa maeneo hayo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ziara hiyo, Naibu Waziri, Mhandisi Maryprisca Mahundi amewapongeza DAWASA kwa kujituma kutekeleza Miradi hiyo ya kimkakati ili kutatua kero ya Maji katika sehemu mbalimbali za mkoa wa Dar es Salaam na Pwani.

Pia amepongeza Watumishi, Wasimamizi wa Miradi yote ya DAWASA wakiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Cyprian Luhemeja katika kufanikisha utekelezaji wa Miradi hiyo takribani 27 sehemu mbalimbali ya Dar es Salaam na Pwani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA, Mhandisi Ramadhani Mketo amesema Mradi wa Maji wa Ruvu Juu hadi Mboga ni Mradi utakaosaidia kuondoa kero ya Maji katika maeneo ya Mlandizi, Chalinze na Mji Mdogo wa Mboga, pia Mradi huu wanalaza mabomba kwa umbali wa Kilometa 59  katika Mitambo ya Ruvu Juu hadi Chalinze, Mji wa Mboga.

Amesema pia mradi huo utatatua kero ya Maji katika Bandari Kavu ya Kwara na kwenye Mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR Kwara, amesema Lita 9,300,000 za Maji zitatumika kwa siku baada ya kukamilika Mradi huo.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Mhe. Ridhwan Kikwete amesema ujio wa Naibu Waziri wa Maji katika Maeneo hayo itasidia katika utekelezaji wa Miradi hiyo ya Maji na kuondoa kero kwa Wananchi wake.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mketo akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kuhusu ulazaji wa Bomba za inchi 10 zinazolazwa kutoka Ruvu Juu mpaka Mboga yenye kilometa 58.9 kwenye Mradi wa Chalinze- Mboga unaotekelezwa na DAWASA. Wa kwanza kushoto ni Msimamizi wa Mradi wa DAWASA, Mhandisi Ishmael Kakwezi
Muonekano wa Bomba la inchi 16 linalolazwa kutoka Ruvu Juu mpaka Mboga litakalokuwa na kilometa 58.9 
Kazi ikiendelea
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa Mradi wa DAWASA, Mhandisi Ishmael Kakwezi kuhusu ulazaji wa Bomba unavyopita kwenye ramani kuanzia Ruvu Juu mpaka Mboga kilichopo Wilaya ya Bagamoyo  wakati wa Ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na DAWASA.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akikagua mradi wa ulazaji wa mabomba ya inchi 16 katika eneo la Kitongoji cha Mbala kilichopo Kijiji cha Chamakweza wakati wa Ziara yake ya kukagua Miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.
Kazi ikiendelea 
Msimamizi wa Mradi wa DAWASA, Mhandisi Ishmael Kakwezi akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi pamoja na Mbunge wa Chalinze Riziwani Kikwete kuhusu mradi wa kujenga pampu ya kusukuma maji katika Kijiji cha Chamakweza wakati wa Ziara ya naibu Waziri wa maji alipotembelea miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.
Msimamizi wa Mradi wa DAWASA, Mhandisi Ishmael Kakwezi akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi pamoja na Mbunge wa Chalinze Riziwani Kikwete kuhusu ujenzi wa pampu ya maji ya Msoga wakati wa Ziara ya Naibu Waziri wa Maji.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi  akiendelea na Ziara yake ya kutembelea miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la ujenzi wa pampu ya maji ya Msoga kuhusu kuridhishwa na miradi inayotekelezwa na DAWASA wakati wa Ziara yake ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa na Mamlaka hiyo.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mketo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa miradi inayosimamiwa na DAWASA wakati wa Ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi.
Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna wanavyosimamia miradi hasa ya maji ili kuondoa hadha kwa wakazi wa Chalinze ambao wanachangamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi alipokuwa anatembelea miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.