Matokeo chanyA+ online




Tuesday, April 30, 2019

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI TEMEKE LAZINDUA KAMPENI YA NINACHO, NAJUA KUKITUMIA

Kamanda wa Viwanja vya Ndege wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini (ACF) Maria Kulaya, akisalimiana na Katibu Tawala Wilaya ya Temeke Bi. Bupe Mwakibete (kulia), alipowasili katika viwanja vya Mwembe Yanga, kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Ninancho, Najua kukitumia, iliyofanyika katika viwanja hivyo Temeke Dar es salaam mapema leo asubuhi tarehe 30/04/2019
Katibu Tawala Wilaya ya Temeke Bi. Bupe Mwakibete akitoa hotuba kwa wananchi na wakazi wa Wilaya ya Temeke, kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Ninancho, Najua kukitumia iliyofanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es salaam, mapema leo asubuhi.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kizimamoto Temeke (ASF) Puyo Nzalayaimisi, akihutubia wananchi na wakazi wa Wilaya ya Temeke, kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Ninancho, Najua kukitumia iliyofanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es salaam mapema leo asubuhi.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mbeya akitoa salamu kwa niamba ya Makamanda wa Mikoa na Kumkaribisha Mgenia Rasmi Katibu Tawala wa Wilaya ya Temeke, kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Ninancho, Najua kukitumia iliyofanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es salaam mapema leo.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Temeke Bi. Bupe Mwakibete (kulia) akimsikiliza Sajini wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Lugendo Rashidi (kushoto), alipotembelea Banda la kutolea elimu, kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Ninancho, Najua kukitumia iliyofanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es salaam, mapema leo. (Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji Makao Makuu)

No comments:

Post a Comment