Matokeo chanyA+ online




Sunday, June 23, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI ATOA MKONO WA POLE KWA NAIBU KATIBU MKUU WA CCM ZANZIBAR KWA KUFIWA NA MKE WAKE JIJINI DAR


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  Dkt. Abdallah Sadala (Mabodi) Mikocheni jijini Dar es salaam ambaye amefiwa na mkewe Dkt. Badria Abubaker Gunar aliyefariki dunia June 22, 2019 jijini Dar es salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiomba dua maalumu na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  Dkt. Abdallah Sadala (Mabodi) pamoja na familia yake nyumbani kwao Mikocheni jijini Dar es salaam kumuombea marehemu Dkt. Badria Abubaker Gunar(Mke wa Naibu katibu mkuu CCM Znz) aliyefariki dunia June 22, 2019 jijini Dar es salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu wa Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa pili wa Rais wa Znz Balozi Sefu Ali Idd, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mhe. Ali Hassan Mwinyi  na Viongozi mbalimbali wa  Serikali na Chama cha Mapinduzi wakimuombea dua marehemu Dkt. Badria Abubaker Gunar Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  Dkt. Abdallah Sadala (Mabodi) aliyefariki dunia June 22, 2019 jijini Dar es salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akimsikiliza Gavana wa Benki Kuu Profesa Frolence Luoga akizungumza mara baada ya dua maalumu ya kumuombea marehemu Dkt. Badria Abubaker Gunar Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt. Abdallah Sadala (Mabodi) ambaye pia alikuwa ni mtumishi wa Benki Kuu (BOT) ,aliyefariki dunia June 22, 2019 jijini Dar es salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiwa msibani wakati wa dua maalumu ya kumuombea marehemu Dkt. Badria Abubaker Gunar Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt. Abdallah Sadala (Mabodi) ambaye pia alikuwa ni mtumishi wa Benki Kuu (BOT) ,aliyefariki dunia June 22, 2019 jijini Dar es salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiagana na mdau wa Michezo Mzee Kilomoni  pamoja na waombolezaji wengine mara baada ya dua maalumu ya kumuombea marehemu Dkt. Badria Abubaker Gunar Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt. Abdallah Sadala (Mabodi) ambaye pia alikuwa ni mtumishi wa Benki Kuu (BOT) ,aliyefariki dunia June 22, 2019 jijini Dar es salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akiagana na  Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  Dkt. Abdallah Sadala (Mabodi) mara baada ya kumpa pole kufuatia kifo cha  mkewe Dkt. Badria Abubaker Gunar Mikocheni Jijini Dar es salaam, aliyefariki dunia June 22, 2019 jijini Dar es salaam.PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment