Matokeo chanyA+ online




Friday, August 30, 2019

BODI MPYA YA WADHAMINI MOI YAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA HUDUMA ZAIDI

Dar es Salaam, 30/08/2019. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MOI Profesa Charles Mkony leo ameongoza kikao cha kwanza cha bodi mpya ya MOI ambapo wajumbe wamepata fursa ya kukutana na menejimenti pamoja na kukagua maeneo ya kutolea huduma.
Prof. Mkony ameongoza wajumbe hao kujadili mipango, mikakati pamoja na kupitia taarifa mbalimbali za Taasisi ambazo zimewasilishwa zinazolenga kuendelea kuboresha utoaji wa huduma bora kwa watanzania.
Pamoja na Mwenyekiti wa bodi hiyo mpya Prof. Charles Mkony na Katibu Dkt Respicious Boniface wajumbe wengine ni Bi Deodatha Makani, Dkt Amani Malima, Bw. Charles Beida, Dkt Pilly Chillo, Dkt Tuhuma Tuli, Dkt Petronila Ngiloi, Dkt Pern Tellya na Dkt Lusisyo Mwakaluka.
Aidha, Prof.Mkony amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kumuamini na kumpa dhamana ya kuongoza bodi ya wadhamini ya Taasisi kubwa ya MOI.
“Ikiwa ni kikao cha kwanza nimshukuru sana Mh Rais kwa nafasi hii, ameonyesha imani kwangu na kwa wenzangu hivyo ni jukumu letu kufanya kazi kwa bidii na kwa weledi ili Taasisi hii tegemeo iendelee kutoa huduma bora” Alisema Prof. Mkony
Kwa upande wake ,Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface amesema ujio wa bodi mpya wa wadhamini MOI utaleta mageuzi makubwa katika utoaji wa huduma pamoja na kuendelea kuboresha na kuanzisha huduma mpya sawa na zile za mataifa ya Ulaya na India.
Baada ya kukamilisha ziara ya kukagua maeneo ya kutolea huduma MOI wajumbe wa bodi mpya ya wadhamini MOI wameipongeza Serikali kwa ukwekezaji mkubwa iliyoufanya kwenye miundombinu, vifaa, majengo na wataalamu na kuahidi kuifanya MOI kuendelea kuwa Taasisi bora zaidi barani Afrika.

No comments:

Post a Comment