Matokeo chanyA+ online




Friday, February 28, 2020

RAIS DKT MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSTUKIZA KUKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MSIKITI WA BAKWATA KINONDONI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akisindikizwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamiz wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) baada ya kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo Ijumaa 28, 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishiriki katika dua na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamizi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) alipofanya ziara ya kustukiza
kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo Ijumaa 28, 2020
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Februari, 2020 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Msikiti mkubwa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) unaojengwa Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Msikiti huo unajengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohammed VI wa Morocco baada ya kuombwa na Mhe. Rais Magufuli alipofanya ziara rasmi hapa nchini Oktoba 2016.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamizi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) akitembezwa kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo Ijumaa 28, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea machache na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamiz wa Baraza Kuu la Waislamu
Tanzania (BAKWATA) baada ya kufanya ziara ya kustukiza kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo
Ijumaa 28, 2020

Akiongozwa na Mufti wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zubeir bin Ally, Mhe. Rais Magufuli amejionea kazi za ukamilishaji wa jengo jipya la Msikiti na jengo la ofisi ya Taasisi ya Mfalme Mohammed VI wa Morocco zikiendelea kukamilishwa, na ameelezea kufurahishwa kwake na ubora na uzuri wa Msikiti huo.
Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mfalme Mohammed VI wa Morocco kwa kutekeleza ombi alilomuomba la kuwajengea Waislamu Msikiti mkubwa kuliko yote hapa nchini, na amempongeza Mufti wa Tanzania na Waislamu wote kwa kujengewa nyumba nzuri ya Ibada.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamizi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) akitembezwa kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo Ijumaa 28, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamizi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) akitembezwa kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo Ijumaa 28, 2020

Mufti wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zubeir bin Ally amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwajali Waislamu na kuwaombea msaada wa kujengewa Msikiti huo ambao ujenzi wake umefikia asilimia 97.
Akiwa na viongozi wenzake wa BAKWATA, Sheikh Mkuu Aboubakar Zubeir bin Ally ameongoza Dua ya kumuombea Mhe. Rais Magufuli na kuliombea Taifa ili Mwenyezi Mungu aiepushe Tanzania dhidi ya maradhi ya homa ya virusi vya corona, kudumisha amani na utulivu na kuombea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu ufanyike vizuri na kwa amani.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamizi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) akitembezwa kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo Ijumaa 28, 2020


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akisindikizwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally na viongozi wengine waandamiz wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) baada ya kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Msikiti wa Bakwata unaojengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco Kinondoni jijini Dar es salaam leo Ijumaa 28, 2020

No comments:

Post a Comment