Matokeo chanyA+ online




Thursday, December 31, 2020

IDADI YA WAPIGA KURA IRAMBA HAIKUTOSHA KWA RAIS MAGUFULI KUTOKANA NA MAENDELEO ALIYOYAFANYA


Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye Kikao cha Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kiomboi tarehe 29 Disemba 2020. (Picha Zote Na Mathias Canal)
Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Kulia) akipokea cheti cha pongezi kwa mchango wake wa kuimarisha chama kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama Cha mapinduzi wilaya ya Iramba Ndg Ashery Joel wakati wa Kikao cha Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kiomboi tarehe 29 Disemba 2020. 
Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye Kikao cha Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kiomboi tarehe 29 Disemba 2020.

Sehemu ya wajumbe wa Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba wakifatilia Kikao cha Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya hiyo kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kiomboi tarehe 29 Disemba 2020.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida Mhe Emmanuel Luhahula akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye Kikao cha Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kiomboi tarehe 29 Disemba 2020.

Na Mathias Canal, Iramba-Singida


Idadi ya wapiga kura ya asilimia 30.34% ya wananchi waliojitokeza kupiga kura katika uchaguzi Mkuu wa Disemba 29, 2020 Jimbo la Iramba Magharibi Mkoani Singida imetajwa kuwa ilikuwa ni ndogo ikilinganishwa na wapiga kura waliojiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.

Idadi ya wananchi waliojiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura wilayani Iramba ni 141,521 lakini waliopiga kura hawafiki hata nusu ya idadi ya wananchi hao waliojiandikisha.

Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameyasema hayo tarehe 20 Disemba 2020 wakati akizungumza kwenye Kikao cha Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kiomboi.

Mhe Mwigulu amesema kuwa hilo ni jambo la kufanyiwa kazi kwa haraka kwani katika tathmini za kiushindani linapaswa kupatiwa majibu ikiwemo kubaini chanzo cha tatizo hilo.

“Tumeshinda kwa kiwango kikubwa kwenye nafasi ya Mgombea Urais, Mbunge na Madiwani lakini kuna kiporo cha kukifanyia kazi kwani idadi ya watu waliojitokeza kupiga kura ni wachache kuliko idadi ya wanachama waliojiandikisha” Mhe Mwigulu

Katika kikao hicho Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba ametunukiwa vyeti viwili vya pongezi ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake wa kuimarisha chama namna ya ushiriki wake kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Katika hatua nyingine Dkt Mwigulu amewasihi watanzania kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli.

Amesema kuwa watanzania wamelipa fadhila kwa uchache dhidi ya Rais Magufuli kwani idadi ya waliojitokeza kumpigia kura sio sawa kabisa na idadi ya wananchi waliojiandikisha.

Ameongeza kuwa rekodi ya utendaji kazi iliyofanywa na Rais Magufuli kwa wananchi wa Tanzania katika huduma mbalimbali za kijamii ni ya kifani na itatumika kama somo Duniani kote.

“Ingekuwa imepitishwa kuwa na Rais mmoja wa Afrika ni wazi kuwa Tanzania tungekuwa tumetoa Rais huyo ambaye ni Dkt John Pombe Magufuli kutokana na mambo makubwa aliyoyafanya” Amekaririwa Mhe Mwigulu

No comments:

Post a Comment