Matokeo chanyA+ online




Friday, April 30, 2021

MKUTANO MKUU MAALUMU WA CCM WAMCHAGUA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KUWA MWENYEKITI WA CCM LEO JIJINI DODOMA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM baada ya kupigiwa kura zote za Ndiyo na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika Mkutano Mkuu wa CCM ambao Wajumbe wake Walimchagua kwa Kura zote za Ndiyo kuwa Mwenyekiti Mpya wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.



Mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha Mapinduzi (CCM) umempitisha Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Mwenyekiti wa Sita wa CCM kwa  kura za ndiyo 1862 sawa na asilimia 100.

Rais Samia amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho na Rais wa Tanzania, Hayati Dk John Magufuli kilichotokea Machi 17 2021, jijini Dar Es Salaam mwaka huu.

Akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti wa uchaguzi huo ambaye pia ni Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema kura zilizopigwa ni 1,862 ambapo kura za ndiyo zilikua  zote 1,862 ikiwa ni asilimia 100 ya kura zote.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika Mkutano Mkuu wa CCM ambao Wajumbe wake Walimchagua kwa Kura zote za Ndiyo kuwa Mwenyekiti Mpya wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa ameshikilia Tuzo yake ya Heshima na Pongezi aliyopewa na Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT) mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima kutoka kwa Mwenyekiti wa UWT Gaudensia Kabaka mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.



 
 

Viongozi mbalimbali pamoja na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi wakifurahia ndani ya Ukumbi wa Mkutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 Jijini Dodoma. PICHA NA IKULU

 


 

No comments:

Post a Comment