Matokeo chanyA+ online




Friday, October 8, 2021

BASHE AITAKA TAASISI YA UTAFITI WA VIUATILIFU (TPRI) KUSHIRIKIANA NA WIZARA YA KILIMO KUTEKETEZA MAGUGU YANAYOHARIBU ARDHI YA KILIMO NA UFUGAJI

 

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) nje kidogo ya jiji la Arusha wakati alipotembelea Taasisi hiyo ili  kuona shughuli mbalimbali za kiutafiti zinazofanywa na taasisi hiyo jana , Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa (TPRI). Dkt. Efrem Njau

Waziri Bashe ameitaka Taasisi hiyo kuhakikisha inashirikiana na Wizara ya Kilimo  pamoja na wadau wengine ili kuteketeza magugu ambayo yamekuwa yakisambaa karibu nchi nzima yanayosababisha uharibifu wa ardhi ya kilimo na ufugaji.

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akisisitiza jambo wakati akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) nje kidogo ya jijini Arusha wakati alipotembelea Taasisi hiyo ili kuona shughuli mbalimbali za kiutafiti zinafanyika katika taasisi hiyo.

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akimsikiliza Dkt. Efrem Njau Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) alipokuwa akiwasilisha taarifa ya taasisi hiyo nje kidogo ya jijini Arusha wakati alipotembelea maabara za Taasisi hiyo ili kuona shughuli mbalimbali za kiutafiti zinafanyika katika taasisi hiyo.

Afisa  Mtendaji Mkuu wa TAHA Bi. Jaquiline Mkindi akielezea gharama ambazo wakulima wa mashamba makubwa ya Maua na mbogamboga pamoja na matunda wanagharamia ili kufanyiwa tafiti za ardhi, maji na anga kwa kutumia  wataalam kutoka nje ya nchi.

Kikao kikiendelea katika ya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe na Menejimenti ya Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) 

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akiongozana  na viongozi wa Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) nje kidogo ya jijini Arusha wakati akikagua maabara za taasisi hiyo ili  kuona shughuli mbalimbali za kiutafiti zinafanyika katika taasisi hiyo jana.

Afisa  Mtendaji Mkuu wa TAHA Bi. Jaquiline Mkindi akiongozana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Kilimo Bw. Hudson Kamoga pamoja na baadhi ya wakuu wa vitengo vya  Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) wakati Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe  alipotembelea taasisi hiyo jana.

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akimsikiliza Baraka Sendeka Mchambuzi wa Viatilifu katika maabara za  Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) nje kidogo ya jijini Arusha alipokuwa akitoa maelezo kuhusu moja ya mashine zinazotumika kufanya utafiti wakati alipotembelea Taasisi hiyo ili  kuona shughuli mbalimbali za kiutafiti zinavyofanyika , Kushoto ni Dkt. Efrem Njau Kaimu Mkurugenzi wa (TPRI).

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akimsikiliza Dkt. Efrem Njau Kaimu Mkurugenzi wa (TPRI) wakati akitembelea katika maabara za  Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) nje kidogo ya jijini Arusha alipokuwa akitoa maelezo kuhusu moja ya mashine zinazotumika kufanya utafiti wakati alipotembelea Taasisi hiyo kulia ni Jaquiline Mkindi Aisa Mtendaji Mkuu wa TAHA.

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akimsikiliza Venace Kasenene Mchambuzi wa Viuatilifu katika maabara ya Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) nje kidogo ya jijini Arusha wakati alipotembelea Taasisi hiyo ili kuona shughuli mbalimbali za kiutafiti zinafanyika katika taasisi hiyo.

Moja ya majengo ya taasisi hiyo.

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akisisitiza jambo wakati akizungumza alipokuwa akitembelea maabara za Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI) nje kidogo ya jijini Arusha wakati alipotembelea Taasisi hiyo ili kuona shughuli mbalimbali za kiutafiti zinavyofanyika katika taasisi hiyo kutoka kushoto ni Dkt. Efrem Njau Kaimu Mkurugenzi wa (TPRI), Ndeninsia Meena Mchambuzi wa Viuatilifu katika maabara na kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TAHA Jaquiline Mkindi.

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akimsikiliza Bw. Tano Hangali Mkuu wa Kitengo cha Utunzaji wa Viuatilifu na Mazingira TPRI wakati akielezea namna ya kutuza   viuatilifu na mazingira katika njia bora.

Muonekano wa moja ya maabara za taasisi hiyo

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe akizungumza na wafanyakazi wa taasisi hiyo mara baada ya kufanya ukaguzi katika maabara kulia ni Profesa Elinangaya Kweka Mkurugenzi wa Utafiti (TPRI).

Picha mbalimbalizikionesha baadhi ya wafanyakazi wakiwa katika kikao hicho wakimsikiliza Mhe.Naibu Waziri Hussein Bashe hayupo pichani

No comments:

Post a Comment