Matokeo chanyA+ online




Thursday, April 28, 2022

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ASHIRIKI KATIKA UZINDUZI WA FILAMU YA TANZANIA THE ROYAL TOUR

 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi mara baada ya kuwakabidhi msaada wa vyakula pamoja na mafuta kwa vituo mbalimbali 27 vya Watoto hao tarehe 28, Aprili, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati akitoa misaada ya Vyakula mbalimbali pamoja na mafuta kwa vikundi 27 vya Watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira hatarishi Mkoani Arusha tarehe 28, Aprili, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwandishi wa Habari Maarufu wa Marekani ambaye ndiye mtayarishaji wa Filamu ya Tanzania The Royal Tour Peter Greenberg mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Arusha International Conference Centre AICC Jijini Arusha kwa ajili ya uzinduzi wa Filamu hiyo tarehe 28, Aprili, 2022.


Viongozi pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa Filamu ya Tanzania The Royal Tour uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Arusha International Conference Centre AICC Jijini Arusha tarehe 28, Aprili, 2022.

 








Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa Filamu ya Tanzania The Royal Tour uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Arusha International Conference Centre AICC Jijini Arusha tarehe 28, Aprili, 2022.



No comments:

Post a Comment