Matokeo chanyA+ online




Tuesday, August 22, 2023

RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AMPOKEA RAIS WA JAMHURI YA INDONESIA JIJINI DAR ES SALAAM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana  na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo wakati alipowasili katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuanza Ziara ya Kikazi hapa nchini tarehe 22 Agosti, 2023.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo wakati wakielekea kwenye Viwanja vya mapokezi ya Viongozi Ikulu Jijini Dar es salaam wakati wa Ziara ya Kikazi ya Rais huyo hapa nchini tarehe 22 Agosti, 2023.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo wakati Wimbo wa Taifa wa Tanzania na Indonesia ukipigwa katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam kwenye mapokezi rasmi kwenye Ziara ya Kikazi ya Rais huyo hapa nchini tarehe 22 Agosti, 2023.





Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo akikagua Gwaride la Heshima mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam kwa Mapokezi rasmi wakati wa Ziara yake ya Kikazi hapa nchini tarehe 22 Agosti, 2023.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo Ikulu Jijini Dar es salaam wakati wa Ziara yake ya Kikazi hapa nchini tarehe 22 Agosti, 2023.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko  Widodo wakati wa Ziara yake ya Kikazi hapa nchini Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 22 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 22 Agosti, 2023.


 

No comments:

Post a Comment