Matokeo chanyA+ online




Sunday, January 14, 2018

YALIYOJIRI  JANUARI 14, 2018 KATIKA MAZUNGUMZO YA RAIS WA JMT, DKT. JOHN POMBE MAGUFULI  NA RAIS WA RWANDA MH. PAUL KAGAME KATIKA ZIARA YAKE YA KIKAZI NCHINI TANZANIA.

#Rais wa Rwanda, Mh. Paul Kagame amewasili majira ya saa 4 asubuhi tarehe 14/1/2018 katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa JMT, Dkt. John Pombe Magufuli.

#Rais wa Rwanda, Mh. Paul Kagame yuko Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku moja ikiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Rwanda.

#Nimemuhakikishia kuwa Watanzania tutampa ushirikiano wa kutosha katika nafasi yake ya Uenyekiti wa Umoja wa Afrika - Rais Magufuli.

#Tumekubaliana kukuza biashara kati ya Rwanda na Tanzania kwa kutengeneza mazingira mazuri ya biashara - Rais Magufuli.

#Juhudi za kukuza biashara kati ya Rwanda na Tanzania zilishaanza, mwaka 2017 mizigo iliyofika katika Bandari ya Tanzania kutoka Rwanda ilifikia tani 950,000 - Rais Magufuli.

#Tumekubaliana na Rais Kagame kujenga reli ya kisasa kutoka Isaka, Tanzania hadi Kigali, Rwanda ili kuchochea maendeleo ya nchi hizi mbili - Rais Magufuli.

#Naomba Mawaziri wa Rwanda na Tanzania wanaohusika katika sekta ya miundombinu wakutane wiki hii ili kupanga juu ya ujenzi wa reli hiyo - Rais Magufuli.

#Tunataka ndani ya mwaka huu tuweke mawe ya msingi katika ujenzi wa reli hiyo ya kisasa ili ujenzi huo uanze rasmi - Rais Magufuli.

#Napenda kumpongeza Rais Kagame kwa hatua anazozichukua katika kuiletea maendeleo nchi ya Rwanda - Rais Magufuli.

#Nampongeza Mkuu wa Majeshi wa nchini Rwanda kwa kushirikiana na Mkuu wa Majeshi wa Tanzania katika kuimarisha usalama wa nchi zote mbili - Rais Magufuli.

#Wananchi wa Rwanda wanataka kufanya biashara na watanzania hivyo hii itapelekea kudumisha amani na umoja wetu na kuinua uchumi wa nchi zetu - Rais Kagame.

#Naahidi kuendelea kutembelea nchi ya Tanzania ili kupata ushauri kuhusu mambo mbalimbali yatakayotuletea maendeleo katika nchi zetu - Rais Kagame.

#Tatizo la ajira ni changamoto kwa Afrika nzima hivyo kila nchi inahitaji kukuza biashara na uwekezaji ili kuongeza upatikanaji wa ajira - Rais Kagame.

#Pia jukumu kubwa linabaki kwa vijana namna ambavyo wanaweza kutumia elimu na ujuzi walionao katika kujitafutia ajira - Rais Kagame.







                                    IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI - MAELEZO.

No comments:

Post a Comment