Matokeo chanyA+ online




Wednesday, March 18, 2020

SERIKALI IMEFANYA KAZI YA KUFUTA NA KUPUNGUZA ADA NA TOZO 54 ILI KUONDOA KERO NA URASIMU KWA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI NCHINI

Serikali imeendelea kufanya kazi ya Uendelezaji wa Viwanda  ambapo kazi zilizotekelezwa ni upanuzi wa Kiwanda cha Ngozi na Bidhaa za Ngozi cha Karanga (Moshi) na kuimarisha Shirika la Nyumbu (Pwani) ili kuongeza uzalishaji ikiwemo magari ya zimamoto.
Bidhaa zinazotengenezwa na kiwanda cha Karanga
 Hayo yemesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango katika taarifa yake ya mapendekezo ya   Serikali ya mpango wa maendeleo wa taifa  na ya kiwango na ukomo wa bajeti ya  Serikali kwa mwaka 2020/21 mjini Dodoma. 

Waziri Mpango amesema kuwa serikali pia imefanyia kazi ya kufutwa na kupunguzwa kwa ada na tozo 54 ili kuondoa kero na urasimu kwa wafanyabiashara na wawekezaji nchini.
 Aidha ameongeza kuwa kuzinduliwa na kuanza uzalishaji katika viwanda saba (7) ambavyo ni kiwanda cha Pipe Industries Co. Limited (Dar es Salaam), kiwanda cha chai cha Kabambe (Njombe), kiwanda cha Yalin Cashewnut Company Ltd (Mikindani – Mtwara), kiwanda cha 21st Century Food and Packaging (Dar es Salaam), kiwanda cha kusaga mahindi cha kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited – MeTL (Dar es Salaam), kiwanda cha bidhaa za plastiki cha Plasco Pipelines Co. Ltd (Dar es Salaam), kiwanda cha kupakia na kuhifadhi parachichi - Rungwe Avocado (Mbeya) na kiwanda cha kuchakata parachichi kwa ajili ya kutengeneza mafuta (KUZA Afrika). 

Ambapo amesema kuwa  jumla ya tani 4,254.1 za korosho zilibanguliwa kupitia viwanda 17 na kuwezesha kuzalishwa kwa fursa za ajira za moja kwa moja 4,066, Na kwa  kipindi cha mwaka 2016/17 - 2019/20, jumla ya viwanda vikubwa 201, vya kati 460, vidogo 3,406 na vidogo sana 4,410 vilianzishwa.

No comments:

Post a Comment