Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo katika ukumbi wa TPRI Jijini Arusha, tarehe 16 Machi 2020. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Aidha,
serikali imewataka wafanyakazi wote wa Wizara kuendelea kujengewa
misingi ya uwajibikaji hasa katika kutambua wajibu wao kwa Umma na
kuacha uzembe katika utekelezaji wa majukumu yao huku wakisisitizwa
kutumia muda mwingi katika kufanya shughuli ambazo hazina tija
zinazoathiri utendaji kazi.
Serikali
inayo dhamira ya dhati ya kuondoa uzembe na ubadhirifu miongoni mwa
watumishi wa umma hivyo ni vyema watumishi wajiepushe na matumizi ya
lugha zisizo na staha muda wote wanapotekeleza majukumu yao.
Waziri
wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ametoa rai hiyo wakati akifungua
mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo katika ukumbi wa
TPRI Jijini Arusha l tarehe 16 Machi 2020.
Katika
mkutano huo ambao wajumbe watapata fursa ya kupokea taarifa ya
utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2019/2020 na kujadili na kupitisha
makisio ya bajeti ya mwaka 2020/2021 wametakiwa kota Mawazo muhimu
katika hatua za utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2020/2021 na kujadili kwa
kina na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha bajeti ya Wizara kwa
Mwaka ujayo wa fedha.
Amesema
kuwa Wizara ya Kilimo inalo jukumu kubwa katika Maendeleo ya nchi hasa
kwa kuzingatia kuwa zaidi ya Watanzania asilimia 65.5 wameajiriwa katika
kilimo, asilimia 28.7 ya pato la taifa, zaidi ya asilimia 30 ya fedha
za kigeni, asilimia 65 ya malighafi za viwanda, asilimia 100 ya chakula
chote nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Ndg Gerald Kusaya akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwa ajili ya ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo katika ukumbi wa TPRI Jijini Arusha, tarehe 16 Machi 2020.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb), na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Ndg Gerald Kusaya wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo katika ukumbi wa TPRI Jijini Arusha, tarehe 16 Machi 2020.
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Arusha
Pamoja na mambo mengine Waziri Hasunga amewataka wajumbe hao kukumbuka kuwa wizara inawajibika na masuala yote yanayohusu Uendelezaji wa Sekta ya Kilimo hususani; Kuongeza Tija na Uzalishaji wa Mazao ya Kilimo; Kuwezesha Upatikanaji wa Masoko ya Bidhaa za Kilimo; Kuwezesha Uongezaji wa Thamani ya Mazao ya Kilimo; Kuimarisha Mfumo wa Ukusanyaji na Uhifadhi; Uchambuzi na Usambazaji wa Takwimu; Kusimamia Sera, Sheria, Kanuni na Mikakati katika Sekta ya Kilimo; Kuboresha Uratibu katika Sekta ya Kilimo; Kuboresha Uwezo wa Wizara wa kutoa huduma, kuwezesha na kuimarisha Ushirika na Asasi za Wananchi katika Kilimo na Sekta nyingine na Kuzingatia Masuala Mtambuka katika Kilimo.
Mhe Hasunga amesema kuwa katika kutambua uzito na umuhimu wa majukumu hayo kila mmoja katika sehemu yake ya kazi anatakiwa kuwajibika na kufanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake ya kukuza uchumi na kuondoa umaskini kwa wananchi.
No comments:
Post a Comment