Matokeo chanyA+ online




Wednesday, March 18, 2020

UKARABATI WA RELI YA KATI DAR ES SALAAM - NGERENGERE UMEFIKIA ASILIMIA 89.14

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema kuwa Serikali imendelea  kukarabati reli ya kati ikijumuisha njia  ya reli, madaraja na ujenzi wa makalavati kwa vipande vya Dar es Salaam – Ngerengere (km 145) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 89.14.

Aidha amesema kuwa kwa upande wa Ngerengere - Kilosa (km 138) ujenzi umefikia asilimia 59.43, ambapo Kilosa - Itigi (km 343) ni asilimia 82.57 na Itigi - Isaka (km 344) umefikia asilimia 82.05.

Akizungumzia ukarabati wa reli ya Tanga – Arusha (km 439) amesema kuwa ujenzi umeendelea ambapo ukarabati wa kipande cha reli ya Tanga – Moshi (km 353) umekamilika na kuanza kusafirisha abiria na mizigo ambapo ukarabati wa kipande cha Moshi – Arusha (km 86) umeendelea kwa kubadili reli na mataruma na kurejesha madaraja na makalavati, kukarabati stesheni na kufungua mifereji ya maji ya mvua ambapo utekelezaji umefikia asilimia 90

No comments:

Post a Comment