Matokeo chanyA+ online




Saturday, February 25, 2023

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Dk. Condoleezza Rice na mfanyabiashara Bill Gates wameungana na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. George W. Bush katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Ijumaa Februari 24, 2023



Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. George W. Bush na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Dk. Condoleezza Rice wakiwa kwenye mjadala katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023




Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa 66 wa Mambo ya Nje wa Marekani Dk. Condoleezza Rice katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) katika ukumbi jijini Washington DC Februari 24, 2023


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mfanyabiashara Bill Gates katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. George W. Bush katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) wa Marekani Bi Alice Albright katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Kupambana na UKIMWI (President’s Emergency Plan for AIDS Relief - PEPFAR) jijini Washington DC Februari 24, 2023


Sherehe hiyo, iliyoandaliwa na Taasisi ya George W. Bush inafanyika  katika Taasisi ya Amani ya Marekani. Watatu hao watashiriki katika mjadala  maalumu utaoendeshwa na Dkt. Rice kuhusu kuanzishwa kwa PEPFAR, mafanikio yake  makubwa, na jinsi programu hiyo inavyofanikiwa katika  nchi washirika na kwa sera ya kigeni za Marekani.


Kwa Mujibu  wa taarifa kutoka Taasisi ya George W. Bush, katika maadhimisho hayo, Mke wa Rais Mstaafu wa Marekani George W. Bush, Bi. Laura Bush, atatoa maelezo mafupi na kuwatambulisha Tatu Msangi na Faith Mang'ehe, Mabalozi wa Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation kutoka Tanzania waliohudhuria wakati wa kutolewa hotuba ya Hali ya Muungano  (State of the Union) katika Congress ya Marekani, kuhusu mpango huo wa PFEPFAR mwaka 2008. 

 

Katika kuadhimisha miaka hiyo 20 ya mafanikio ya PEPFAR, licha ya kwamba Mpango huo unatekelezwa katika nchi mbalimbali Afrika na Asia, Taasisi ya George Bush Foundation wameamua kumualika Dkt. Kikwete kwa kutambua mchango wake mkubwa katika kuufanya Mpango huo kuwa na mafanikio.


Kwa mujibu wa Taasisi ya George W. Bush Foundation, Tanzania imekua ni nchi ya kupigiwa mfano kwa namna ilivyofanya jitihada za kupambana na ugonjwa wa UKIMWI kwa juhudi zake yenyewe kama nchi na kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kimataifa kama vile PEPFAR.


Taasisi hiyo inasema kwamba tangu mwaka 2003, PEPFAR imesaidia Tanzania kupunguza vifo vinavyotokana na UKIMWI kwa karibu 80% na maambukizi mapya kwa karibu 60%. Mpango huo ulipoanza, chini ya Watanzania 1,000 walikuwa wakipata matibabu ya VVU. Hivi sasa, zaidi ya Watanzania milioni 1.5 wanapokea matibabu haya ya kuokoa maisha.


Tangu Rais George W. Bush alipozindua PEPFAR mwaka 2003, serikali ya Marekani imewekeza zaidi ya dola bilioni 100 katika mapambano yake ya kimataifa dhidi ya VVU/UKIMWI, zikiwemo karibu dola bilioni 7 kwa Tanzania, ukiwa ni mchango  mkubwa kuwahi kutolewa na taifa lolote kupambana na ugonjwa mmoja katika historia ya binadamu.


 

No comments:

Post a Comment