Matokeo chanyA+ online




Monday, March 30, 2020

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA HOSPITALI WILAYA YA KIBAHA ILIYOTENGWA KUWAHUDUMIA WAGONJWA WA CORONA

Waziri Mkuu, Kaasim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  (wa tatu kulia) wakati alipokagua hospitali ya wilaya ya kibaha iliyopo eneo la Lulanzi  ambayo imetengwa kwa ajili ya kuwahuduma kwa wagonjwa wa Coroma, Machi 28, 2020.  Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo  na wa pili kushoto ni  Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Bakari.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua wodi za hospitali ya wilaya ya Kibaha  iliyopo eneo la Lulanzi  ambayo imetengwa  kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa Corona Mchi 28, 2020. Kushto ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilio. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu 
 
Na.WAMJW-Kibaha

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ametembelea Hospitali mpya ya Halmashauri ya Wilaya Kibaha ambayo itatumika kulaza  watakaobainika kuwa na Virusi vya ugonjwa wa Corona (Covid19).

Mhe.Kassim Majaliwa amesema  hospitali hiyo itatumika kulaza watu walioambukizwa ugonjwa huo  na kwamba itatumika kwa muda na baada ya ugonjwa huo kwisha itaanza kutoa huduma nyingine za afya.

Waziri Mkuu aliwaeleza wananchi wa Wilaya ya Kibaha kuwa watu wenye maambukizi ya VIRUSI vya  COVID 19 watalazwa katika hospitali hiyo kwa muda wa siku 14 na baada ya uchunguzi ikibainika hawana ugonjwa huo wataruhusiwa kurejea nyumbani.

Mhe. Kassim Majaliwa amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya Corona na amezikumbusha familia kuwa na utaratibu wa kunawa mikono mara kwa mara kwa kutumia maji tiririka na sabuni au  kutumia vitakasa mikono (sanitizer).

Awali, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu alimweleza Waziri Mkuu kwamba hospitali hiyo ilipokea kiasi cha shilingi milioni 394 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa hospitali hiyo.
 

No comments:

Post a Comment